Labani og
JF-Expert Member
- Sep 15, 2020
- 22,854
- 32,657
Ameandika Sama Ndambile
KUNA KILA DALILI WAWEKEZAJI WAMEINGIA KWENYE JAMBO WASILOLIFAHAMU
Bilioni 38 kwa Miaka mitano.
Bilioni 5.6 kila mwaka.
Ongezeko la 10% kwa kila mwaka.
FAIDA ZA KIMKATABA.
1. Ujenzi wa Uwanja wa Bunju (Watu Elf10 hadi 12).
2. Gari jipya la Irizar .
3. Studio ya kisiasa.
4. Ujenzi wa ofisi ya klabu.
5. Kukuza Vipaji ( pesa cash kutolewa)
6. Maadalizi ya timu mwanzo wa msimu - Milioni 100
7. Ujenzi wa kituo cha tiba.
8. Simba Day - Milioni 100 kila mwaka.
9. Shughuli za uendeshaji - Milioni 470 kwa mwaka.
10. Uingizaji jezi zenye chapa ya kidunia.
MASWALI
1. Nini masharti ya muwekezaji au yeye kazi yake ni kutoa tu? Hakuna mkataba wa kibiashara wa hivi.
2. Nini nafasi ya mdhamini huyu ndani ya klabu kwa sababu tayari MO yumo ndani? Nini mipaka yao kiutendaji na MO amelipokeaje hili?
3. Hawa Jayrutty Investment East Africa Limited wanauelewa kiasi gani wa mambo ya michezo? Wanazifahamu vizuri changamoto za biashara hii?
4. Mkataba unasemaje iwapo Jayrutty Investment East Africa Limited watashindwa kutekeleza ahadi zao?
5. Jayrutty wataingiza pesa kupitia jezi na bidhaa nyingine pekee kama kofia au kuna chanzo kingine mpaka waahidi yote haya?
6. Jayrutty wametumia kigezo gani kuamini wanakwenda kupata faida kubwa ya kuwawezesha kufanya yote haya kupitia jezi na menkandaizi nyingine pekee? Angeahidi Kassim Dewji, Vunjabei au Sandaland nisingekuwa na mashaka sababu wanaijua vizuri biashara hii.
Angalizo la Mwenyekiti Mangungu kwa Jayrutty na uwasilishaji wa kishabiki wa CEO wa Jayrutty Bw. Joseph Rwegasira vilitosha kunionesha giza lililopo hapo mbele labda kama Jayrutty Investment East Africa Limited tayari Bilioni 38 wanazomkoni + pesa ya uwanja+ hizo nyongeza na wamekuja Simba SC kutoa msaada kama ambavyo tumesikia wamekwisha tupia 30% ya Bilioni 5.6 ambayo hata sijui ni ya msimu upi.
Nimejiuliza maswali tu,nikilipata kabrasha zima la mkataba na kulisoma ndio nitachambua.
Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
KUNA KILA DALILI WAWEKEZAJI WAMEINGIA KWENYE JAMBO WASILOLIFAHAMU
Bilioni 38 kwa Miaka mitano.
Bilioni 5.6 kila mwaka.
Ongezeko la 10% kwa kila mwaka.
FAIDA ZA KIMKATABA.
1. Ujenzi wa Uwanja wa Bunju (Watu Elf10 hadi 12).
2. Gari jipya la Irizar .
3. Studio ya kisiasa.
4. Ujenzi wa ofisi ya klabu.
5. Kukuza Vipaji ( pesa cash kutolewa)
6. Maadalizi ya timu mwanzo wa msimu - Milioni 100
7. Ujenzi wa kituo cha tiba.
8. Simba Day - Milioni 100 kila mwaka.
9. Shughuli za uendeshaji - Milioni 470 kwa mwaka.
10. Uingizaji jezi zenye chapa ya kidunia.
MASWALI
1. Nini masharti ya muwekezaji au yeye kazi yake ni kutoa tu? Hakuna mkataba wa kibiashara wa hivi.
2. Nini nafasi ya mdhamini huyu ndani ya klabu kwa sababu tayari MO yumo ndani? Nini mipaka yao kiutendaji na MO amelipokeaje hili?
3. Hawa Jayrutty Investment East Africa Limited wanauelewa kiasi gani wa mambo ya michezo? Wanazifahamu vizuri changamoto za biashara hii?
4. Mkataba unasemaje iwapo Jayrutty Investment East Africa Limited watashindwa kutekeleza ahadi zao?
5. Jayrutty wataingiza pesa kupitia jezi na bidhaa nyingine pekee kama kofia au kuna chanzo kingine mpaka waahidi yote haya?
6. Jayrutty wametumia kigezo gani kuamini wanakwenda kupata faida kubwa ya kuwawezesha kufanya yote haya kupitia jezi na menkandaizi nyingine pekee? Angeahidi Kassim Dewji, Vunjabei au Sandaland nisingekuwa na mashaka sababu wanaijua vizuri biashara hii.
Angalizo la Mwenyekiti Mangungu kwa Jayrutty na uwasilishaji wa kishabiki wa CEO wa Jayrutty Bw. Joseph Rwegasira vilitosha kunionesha giza lililopo hapo mbele labda kama Jayrutty Investment East Africa Limited tayari Bilioni 38 wanazomkoni + pesa ya uwanja+ hizo nyongeza na wamekuja Simba SC kutoa msaada kama ambavyo tumesikia wamekwisha tupia 30% ya Bilioni 5.6 ambayo hata sijui ni ya msimu upi.
Nimejiuliza maswali tu,nikilipata kabrasha zima la mkataba na kulisoma ndio nitachambua.
Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app

