Mzee mende
Member
- May 29, 2020
- 33
- 29
Mchakato wa ufutaji hatimiliki za ardhi ambazo hazitumiki unadaiwa kuingiliwa na baadhi ya matajiri wanaotumia wanyonge ili wavitumie viwanja kwa maslahi yao. JAMHURI lina taarifa kwamba katika orodha ya hatimiliki za ardhi zilizowekwa mezani kwa Rais John Magufuli kwa ajili ya kufutwa, zipo za watu ambao hadi sasa hata hawana habari kwamba umiliki wao wa ardhi unakaribia kufutwa. Na kwamba jambo pekee linalowaokoa ambao hawajafutiwa hadi sasa ni umakini wa Rais Magufuli, ambaye shughuli hii huifanya kwa uangalifu na umakini mkubwa.
“Hao ambao hatimiliki zao zinatakiwa kufutwa wanapaswa kumshukuru sana Dk. Magufuli, kwa sababu jambo hili halifanyii haraka. Anajipa muda na kuwasiliana na vyanzo vyake mbalimbali vya taarifa. “Angekuwa ni mtu wa kupokea tu taarifa na kusaini, watu wengi wangekuwa wamekwishaumia na wengine wengi wangeendelea kuumia kila mwaka. “Kwa sasa yeye ndiye tegemeo la wanyonge ambao wangeumizwa na tabia hii mpya ya matajiri kuingilia mchakato huo wa ardhi ili wayatumie maeneo ya watu wengine kwa faida binafsi,” anasema ofisa mmoja wa Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi katika mahojiano na JAMHURI.
Ofisa huyo ametoa mifano ya mashamba kadhaa ndani ya Mkoa wa Katavi yanayodaiwa kuwa katika hatari ya kufutiwa umiliki, hati zake zikidaiwa ama kuandaliwa kuwekwa mezani kwa Rais, au tayari zinasubiri saini ya kiongozi huyo mkuu wa nchi. Mbali na Katavi, JAMHURI lina mfano wa kiwanja chenye hatimiliki namba 35871, kilicho katika kitalu namba 270, eneo la Viwanda, Mbezi Beach jijini Dar es Salaam, ambacho tayari hati yake imewekwa mezani kwa Rais kwa ajili ya kufutwa matumizi, kwa maelezo kwamba hakijaendelezwa na aliyekuwa akikimiliki.
Hata hvyo, JAMHURI lilipotembelea eneo hilo limekuta shughuli kadhaa zikiendelea, yakiwapo makontena; ishara kuwa mmiliki halali wa sasa analitumia (au kuliendeleza) eneo ambalo umiliki wake umo katika hatihati ya kufutwa. Eneo hilo lenye huduma za maji na umeme, pia limezungushiwa uzio na mmoja kati ya wafanyakazi 10 waliopo hapo anasema makontena hayo yanatumika kuhifadhi vifaa mbalimbali, ingawa hakubainisha ni kwa matumizi gani.
Wasamaria wema ambao ni majirani wa eneo hilo wameliambia JAMHURI kuwa kuna mchezo mchafu unafanywa na mmoja wa matajiri walio na ardhi maeneo hayo (jina tunalihifadhi) anayetaka kulitwaa kwa manufaa yake. “Hapa sisi tunamjua mmiliki wa hili eneo. Huwa anakuja, na ni jirani yetu. Watumishi wa Wizara ya Ardhi wenye nia njema wametutonya kwamba Rais amepelekewa faili ili abatilishe umiliki halali wa kiwanja hiki. “Huyu jirani mwingine ambaye ni tajiri anapambana liwe ‘open space’ (eneo LYAMBA-LYA-MFI- ushawishi wao serikalini kufuta hati za NA JOE BEDA RUPIA la wazi); kwamba anapanga kufungua ‘supermarket’ lakini anadhani kutakuwa na shida ya maegesho ya magari ya wateja. Ndiyo maana hiyo open space anaitaka kwa ajili ya maegesho.
“Hatari tunayoiona mbele yetu ni kwamba akifanikiwa kuchukua eneo hilo, hata sisi hatutakuwa salama. Anaweza kutufanya anachotaka, kwa kuwa tabia mbaya huwa haina dawa,” anasema jirani mmoja na kuongeza kuwa hofu hiyo ndiyo imesababisha wao kulitaarifu JAMHURI, kwa kuwa ni kama tajiri huyo anamweka Rais mtegoni.
JAMHURI limeelezwa kuwa eneo hilo ni la mita za mraba 885 na taarifa kutoka Wizara ya Ardhi zinaonyesha kuwa lilinunuliwa mwaka 1989; likipewa umiliki wa miaka 99 kuanzia Julai 1, 1989. Hizi ni taarifa kutoka eneo moja tu la Tanzania, mbali na Katavi ambako gazeti hili halikuweza kuyatembelea maeneo husika, na tayari linazua maswali mengi kuhusu namna ‘zoezi’ zima la ufutaji wa hatimili za ardhi kwa watu; hasa wanyonge, linavyoendeshwa.
Iwapo eneo lililo barabarani kabisa ndani ya Jiji la Dar es Salaam linaweza kubadilishwa matumizi na kufutwa, itakuwaje kwa maeneo yaliyo mikoani ambako pia wapo matajiri wenye tamaa ya ardhi za wanyonge? Ni bahati mbaya kwamba majirani hao wamekuwa na hofu ya kuandikwa majina yao gazetini wakidai kuwa huenda tajiri mhusika ana marafiki ambao ni ‘wakubwa’ serikalini, hivyo anaweza kuhamishia hasira zake kwao Simu: 0653 336 490.
“Watendaji wanaomsaidia Rais katika masuala ya ardhi wanapaswa kuwa makini. Watu wanaonewa sana. Wanaporwa ardhi kwa hila.
“Rais Magufuli ni mtetezi mzuri wa wanyonge, lakini hawezi kujua kila kitu! Ni kweli kwamba kuna maeneo mengi nchini ambayo watu wameyanunua lakini hayatumiki na ni vizuri kuyagawa kwa watu wengine wenye uwezo wa kuyaendeleza. “Lakini kwa hapa kwetu mtu anamiliki eneo halali, analiendeleza na analipa kodi zote kwa serikali kila mwaka kama inavyotakiwa; leo serikali kufuta hatimili na kukifanya kuwa eneo la kuegesha magari, si kwamba itapoteza kodi inayopata kila mwaka, lakini itakuwa pia imemfukarisha mmiliki. “Huu ni uonevu. Sisi tunaumia kwa sababu tabia hii ni mbaya na haifai itasababisha chuki za bure kwa Rais.
Bahati mbaya ni kwamba haya mambo yako mezani kwake (Ikulu), lakini kwa kuwa bado Rais anafanya mapitio na hajaanza kufuta, upo uwezekano wa kumsaidia jirani huyu. “Jambo baya ni kwamba mwenye kiwanja hajapewa taarifa rasmi kwa maandishi; walau kuambiwa tu kuwa; ‘jiandae, kuna hili huenda likatokea’. Ni kama vile anaviziwa. Sasa na sisi majirani tuna wasiwasi nini kitafuata,” anasema jirani huyo.
JAMHURI linafahamu kuwa sheria au taratibu zilizopo haziruhusu ujenzi wa maduka eneo la viwanda na sasa linamtafuta ‘tajiri’ huyo kufahamu ukweli wa mambo.
Shughuli zikiendelea kat
“Hao ambao hatimiliki zao zinatakiwa kufutwa wanapaswa kumshukuru sana Dk. Magufuli, kwa sababu jambo hili halifanyii haraka. Anajipa muda na kuwasiliana na vyanzo vyake mbalimbali vya taarifa. “Angekuwa ni mtu wa kupokea tu taarifa na kusaini, watu wengi wangekuwa wamekwishaumia na wengine wengi wangeendelea kuumia kila mwaka. “Kwa sasa yeye ndiye tegemeo la wanyonge ambao wangeumizwa na tabia hii mpya ya matajiri kuingilia mchakato huo wa ardhi ili wayatumie maeneo ya watu wengine kwa faida binafsi,” anasema ofisa mmoja wa Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi katika mahojiano na JAMHURI.
Ofisa huyo ametoa mifano ya mashamba kadhaa ndani ya Mkoa wa Katavi yanayodaiwa kuwa katika hatari ya kufutiwa umiliki, hati zake zikidaiwa ama kuandaliwa kuwekwa mezani kwa Rais, au tayari zinasubiri saini ya kiongozi huyo mkuu wa nchi. Mbali na Katavi, JAMHURI lina mfano wa kiwanja chenye hatimiliki namba 35871, kilicho katika kitalu namba 270, eneo la Viwanda, Mbezi Beach jijini Dar es Salaam, ambacho tayari hati yake imewekwa mezani kwa Rais kwa ajili ya kufutwa matumizi, kwa maelezo kwamba hakijaendelezwa na aliyekuwa akikimiliki.
Hata hvyo, JAMHURI lilipotembelea eneo hilo limekuta shughuli kadhaa zikiendelea, yakiwapo makontena; ishara kuwa mmiliki halali wa sasa analitumia (au kuliendeleza) eneo ambalo umiliki wake umo katika hatihati ya kufutwa. Eneo hilo lenye huduma za maji na umeme, pia limezungushiwa uzio na mmoja kati ya wafanyakazi 10 waliopo hapo anasema makontena hayo yanatumika kuhifadhi vifaa mbalimbali, ingawa hakubainisha ni kwa matumizi gani.
Wasamaria wema ambao ni majirani wa eneo hilo wameliambia JAMHURI kuwa kuna mchezo mchafu unafanywa na mmoja wa matajiri walio na ardhi maeneo hayo (jina tunalihifadhi) anayetaka kulitwaa kwa manufaa yake. “Hapa sisi tunamjua mmiliki wa hili eneo. Huwa anakuja, na ni jirani yetu. Watumishi wa Wizara ya Ardhi wenye nia njema wametutonya kwamba Rais amepelekewa faili ili abatilishe umiliki halali wa kiwanja hiki. “Huyu jirani mwingine ambaye ni tajiri anapambana liwe ‘open space’ (eneo LYAMBA-LYA-MFI- ushawishi wao serikalini kufuta hati za NA JOE BEDA RUPIA la wazi); kwamba anapanga kufungua ‘supermarket’ lakini anadhani kutakuwa na shida ya maegesho ya magari ya wateja. Ndiyo maana hiyo open space anaitaka kwa ajili ya maegesho.
“Hatari tunayoiona mbele yetu ni kwamba akifanikiwa kuchukua eneo hilo, hata sisi hatutakuwa salama. Anaweza kutufanya anachotaka, kwa kuwa tabia mbaya huwa haina dawa,” anasema jirani mmoja na kuongeza kuwa hofu hiyo ndiyo imesababisha wao kulitaarifu JAMHURI, kwa kuwa ni kama tajiri huyo anamweka Rais mtegoni.
JAMHURI limeelezwa kuwa eneo hilo ni la mita za mraba 885 na taarifa kutoka Wizara ya Ardhi zinaonyesha kuwa lilinunuliwa mwaka 1989; likipewa umiliki wa miaka 99 kuanzia Julai 1, 1989. Hizi ni taarifa kutoka eneo moja tu la Tanzania, mbali na Katavi ambako gazeti hili halikuweza kuyatembelea maeneo husika, na tayari linazua maswali mengi kuhusu namna ‘zoezi’ zima la ufutaji wa hatimili za ardhi kwa watu; hasa wanyonge, linavyoendeshwa.
Iwapo eneo lililo barabarani kabisa ndani ya Jiji la Dar es Salaam linaweza kubadilishwa matumizi na kufutwa, itakuwaje kwa maeneo yaliyo mikoani ambako pia wapo matajiri wenye tamaa ya ardhi za wanyonge? Ni bahati mbaya kwamba majirani hao wamekuwa na hofu ya kuandikwa majina yao gazetini wakidai kuwa huenda tajiri mhusika ana marafiki ambao ni ‘wakubwa’ serikalini, hivyo anaweza kuhamishia hasira zake kwao Simu: 0653 336 490.
“Watendaji wanaomsaidia Rais katika masuala ya ardhi wanapaswa kuwa makini. Watu wanaonewa sana. Wanaporwa ardhi kwa hila.
“Rais Magufuli ni mtetezi mzuri wa wanyonge, lakini hawezi kujua kila kitu! Ni kweli kwamba kuna maeneo mengi nchini ambayo watu wameyanunua lakini hayatumiki na ni vizuri kuyagawa kwa watu wengine wenye uwezo wa kuyaendeleza. “Lakini kwa hapa kwetu mtu anamiliki eneo halali, analiendeleza na analipa kodi zote kwa serikali kila mwaka kama inavyotakiwa; leo serikali kufuta hatimili na kukifanya kuwa eneo la kuegesha magari, si kwamba itapoteza kodi inayopata kila mwaka, lakini itakuwa pia imemfukarisha mmiliki. “Huu ni uonevu. Sisi tunaumia kwa sababu tabia hii ni mbaya na haifai itasababisha chuki za bure kwa Rais.
Bahati mbaya ni kwamba haya mambo yako mezani kwake (Ikulu), lakini kwa kuwa bado Rais anafanya mapitio na hajaanza kufuta, upo uwezekano wa kumsaidia jirani huyu. “Jambo baya ni kwamba mwenye kiwanja hajapewa taarifa rasmi kwa maandishi; walau kuambiwa tu kuwa; ‘jiandae, kuna hili huenda likatokea’. Ni kama vile anaviziwa. Sasa na sisi majirani tuna wasiwasi nini kitafuata,” anasema jirani huyo.
JAMHURI linafahamu kuwa sheria au taratibu zilizopo haziruhusu ujenzi wa maduka eneo la viwanda na sasa linamtafuta ‘tajiri’ huyo kufahamu ukweli wa mambo.
Shughuli zikiendelea kat