jobe ayoub
JF-Expert Member
- Jan 30, 2012
- 203
- 99
Msafara wa mgombe udiwani kwenda kuchukua fomu uwanja wa nanenane zilipo ofisi za Msimamzi wa uchaguzi
MGOMBE Udiwani kata ya Tungi Manispaa ya Morogoro kwa tiketi ya Chadema Juma Tembo juzi amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo kwa mbwembwe baada ya kusindikizwa na msafara wa magari na pikipiki.
Kata ya Tungi imeingia kwenye uchanguzi mdogo baada ya aliyekuwa diwani wa kata hiyo Mh Daud Mbao'CCM' kuiaga dunia na tume ya uchanguzi kuandaa uchaguzi mdogo kuziba nafasi ya marehemu huyo aliyeugua kwa muda mrefu muda.
Kata ya Tungi imeingia kwenye uchanguzi mdogo baada ya aliyekuwa diwani wa kata hiyo Mh Daud Mbao'CCM' kuiaga dunia na tume ya uchanguzi kuandaa uchaguzi mdogo kuziba nafasi ya marehemu huyo aliyeugua kwa muda mrefu muda.
Mgombe huyo akiwasili ofisi za msimamizi wa uchanguzi
Akisoma fomu hizo
wapambe wake wakishuhudia
Akiwasili ofisi zaChadema kata ya Tungi
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi hiyom ya kata baada ya kuchukua fomu
Wakishangilia nje ya Ofisi hiyo ya kata
Akisaini baada ya kuchukua fomu hiyo
Wakiondoka baada ya kuchukua fomu ambapo walipita nyumbani kwa mgombe udiwani kwa tiketi ya CCM jirani na ofisi za kata za Chama hicho
Chama cha Demokrasia na Maendelea'CHADEMA' kimemteua Juma Tembo aliyegombe ubunge jimbo la Morogoro Kusini 2010 na kushindwa na mpinzani wake mkubwa lnnocent Kalogerezi'CCM' ameteuliwa tena na chama chake kugombe udiwani katika kata hiyo.
Juzi Diwani huyo alikwenda kuchkua fomu na msafara mkubwa wa magari na pikipiki akitokea ofisi za wilaya za Chama hicho zilipo mtaa wa Konga na kuelekea kata ya Tungi umbali wa takribani kilometa 12 kwenda kuchukua fomu hiyo.
Baada ya kukabidhiwa fomu hiyo na msimamizi msaidizi wa uchnguzi huo Bw Abuu Rashid Liwangila alimkabidhji pia kitabu cha kanuni za uchanguzi huo.
Akizungumza na Mtandao huu Msimanizi huyo alisema zoezi la uchukuaji fomu lilianza Januari 2 na mwisho wa kurejeshwa fomu hizo ni January 15.
"Baada ya zoezi hilo kukamilia kampenzi za uchaguzi huo zitaanza Januari 16 na kufikia tamani Februari 8"alisema Bw Liwangila ambaye pia ni Afisa Mtendaji wa kata hiyo ya Tungi.
Msimamizi huyo amedai kwamba mpaka sasa ni wagombea wawili ndio waliofuika ofisini wake na kuchukua fomu hizo ambapo alipotakiwa kuwataja wagombe hao na vyama vyao Afisa Mtendaji huyo aligombe.
Pekua pekua ya Mtndao huu imebani wagombe hao ni wavyama vya CCM na Chadema ambapo CCM imemsimami mwanamke aliyefahmika kwa jina la Mama Twaha
Manispaa ya Morogoro inajumla ya kata 29 na kata zote zinaongozwa na madiwani wa chama cha Mapinduzi'CCM'