HomeSweetHome
Member
- Dec 18, 2010
- 45
- 9
Wana JF nipo nchini Ujerumani, na nimebahatika kukutana na Kijana mwanaharakati kutoka Taasisi moja ya Musuala ya Liberal Democracy nchini Misri. Amewasilisha mada juu ya namna Vijana wa Misri walivyounda Coalition yao na kutumia mtandao wa FB kufanya mapinduzi pale Tahrir Square.
Ameniahidi kunipa uzoefu wa kimapinduzi na jinsi ya kuing'oa madarakani serikali ya Kifalme mfano wa ile ya Chama Cha Mafisadi iliyodumu kwa zaidi ya miaka 40, tangu uhuru. Amenionesha jinsi kijana Khaled Said alivyosaidia kuchochea Mapinduzi mara baada ya kuuawa mauaji ya kikatili na polisi.
Unaweza ukajionea hapa mwenyewe:-
Google-Ergebnis für http://cdn2.likethedew.netdna-cdn.com/wp-content/uploads/2011/02/Khalid_Said_before_after.jpg
Hii iwe fundisho kwa jeshi la polisi. Nakumbuka waliwahi kupiga wananchi katika Maandamano mengi ikiwepo yale ya Wananchi kule Arusha, mbeya na kwingineko nchini. Uvumilivu ulipowashinda wananchi wa Misri wakiongozwa na vijana waliamua kuandama wakianzia na maandamano ya watu elfu 70 (70,000) katika mji wa Mahalla na baadaye watu zaidi ya milioni 2 pale Tahrir Square.
Ndugu wana JF nitaendelea ku-share nanyi mbinu za kufanya mapinduzi mara baada kumaliza mazungumzo yangu na kijana huyu ambaye alitupwa sero mara 3 katika harakati za kudai uhuru wa Kidemokrasia kwa maendeleo yao na vizazi vijavyo.
Ameniahidi kunipa uzoefu wa kimapinduzi na jinsi ya kuing'oa madarakani serikali ya Kifalme mfano wa ile ya Chama Cha Mafisadi iliyodumu kwa zaidi ya miaka 40, tangu uhuru. Amenionesha jinsi kijana Khaled Said alivyosaidia kuchochea Mapinduzi mara baada ya kuuawa mauaji ya kikatili na polisi.
Unaweza ukajionea hapa mwenyewe:-
Google-Ergebnis für http://cdn2.likethedew.netdna-cdn.com/wp-content/uploads/2011/02/Khalid_Said_before_after.jpg
Hii iwe fundisho kwa jeshi la polisi. Nakumbuka waliwahi kupiga wananchi katika Maandamano mengi ikiwepo yale ya Wananchi kule Arusha, mbeya na kwingineko nchini. Uvumilivu ulipowashinda wananchi wa Misri wakiongozwa na vijana waliamua kuandama wakianzia na maandamano ya watu elfu 70 (70,000) katika mji wa Mahalla na baadaye watu zaidi ya milioni 2 pale Tahrir Square.
Ndugu wana JF nitaendelea ku-share nanyi mbinu za kufanya mapinduzi mara baada kumaliza mazungumzo yangu na kijana huyu ambaye alitupwa sero mara 3 katika harakati za kudai uhuru wa Kidemokrasia kwa maendeleo yao na vizazi vijavyo.