Mbunu za mapinduzi Misri kutumika Tanzania soon!

HomeSweetHome

Member
Dec 18, 2010
45
9
Wana JF nipo nchini Ujerumani, na nimebahatika kukutana na Kijana mwanaharakati kutoka Taasisi moja ya Musuala ya Liberal Democracy nchini Misri. Amewasilisha mada juu ya namna Vijana wa Misri walivyounda Coalition yao na kutumia mtandao wa FB kufanya mapinduzi pale Tahrir Square.

Ameniahidi kunipa uzoefu wa kimapinduzi na jinsi ya kuing'oa madarakani serikali ya Kifalme mfano wa ile ya Chama Cha Mafisadi iliyodumu kwa zaidi ya miaka 40, tangu uhuru. Amenionesha jinsi kijana Khaled Said alivyosaidia kuchochea Mapinduzi mara baada ya kuuawa mauaji ya kikatili na polisi.

Unaweza ukajionea hapa mwenyewe:-

Google-Ergebnis für http://cdn2.likethedew.netdna-cdn.com/wp-content/uploads/2011/02/Khalid_Said_before_after.jpg

Hii iwe fundisho kwa jeshi la polisi. Nakumbuka waliwahi kupiga wananchi katika Maandamano mengi ikiwepo yale ya Wananchi kule Arusha, mbeya na kwingineko nchini. Uvumilivu ulipowashinda wananchi wa Misri wakiongozwa na vijana waliamua kuandama wakianzia na maandamano ya watu elfu 70 (70,000) katika mji wa Mahalla na baadaye watu zaidi ya milioni 2 pale Tahrir Square.

Ndugu wana JF nitaendelea ku-share nanyi mbinu za kufanya mapinduzi mara baada kumaliza mazungumzo yangu na kijana huyu ambaye alitupwa sero mara 3 katika harakati za kudai uhuru wa Kidemokrasia kwa maendeleo yao na vizazi vijavyo.
 
Njoo nazo hizo mbinu uje tuandamane sote

Tunazihitaji hizo mbinu, tunashukuru sana kwanza kwa kutoa hii mada chukua mbinu na uje ilituweze kuung'oa utawala wakifisadi na kuwafikisha mafisadi kwenye sheria. Hizo mbinu ndio haswa tunazoziihitaji. Chukua skillls na uje kuzigawa huku bongo ilituwafanikiwe katika harakati za kuwang'oa wafalme wa ccm
 
Back
Top Bottom