Mbunge wetu


Mkosamali>> Kwanini Taasisi mbalimbali ziwe chini ya Rais? Kwanini TAKUKURU iwe ofisi ya Rais na isiwe chini ya Waziri Mkuu… Hizi Taasisi za Ofisi ya Rais ndio zina njaa kwelikweli.. ukiona TAKUKURU inafeli maana yake Rais hana utashi wa kisiasa wa kupambana na Rushwa.. Awamu ya nne imeshindwa kupambana na Rushwa, mnakusanya kodi hamna uwezo wa kutekeleza vitu hivi” >> Mbunge Felix Mkosamali.

Akasimama Waziri Mkuchika >> “Kwa mujibu wa kanuni inayosema Mbunge hatotumia jina la Rais kwa dhihaka katikka mjadala au kwa madhumuni ya kulishawishi Bunge.. Mkosamali ameeleza Rais hana utashi wa kisiasa wa kupambana na Rushwa.. Kiustaarabu afute tu hiyo kauli>>

Mkosamali akaendelea >> “Nitafutaje wakati ndio hali halisi.. Juzi Katibu Mkuu amesafisha watu.. Kesi zote zikichunguzwa DPP anazifuta mbona yako wazi”>>

Akasimama Mbunge Innocent Sebba >> “Niwashukuru Mawaziri wanaohusika na Ofisi ya Rais.. Pamoja na kelele zinazopigwa hawa wenzetu tunawaita ni wapiga debe sio wasafiri.. Wanaosafiri

Baadae akapata nafasi Waziri Mark Mwandosya >> “Hoja ya leo inamzungumzia Ofisi ya juu kabisa katika nchi.. unapokizungumzia chombo hiki kipe heshima inayohitajika.. Huwezi ukamzungumzia Rais kama unavyomzungumzia Mbunge wa Rungwe“>>
 
Na vipi Mh.Mwandosya alivyosema kuhusu uzalendo wa mwanasiasa mmoja aliyekwenda Marekani na kuiponda serikali ya TZ na akaendelea kusema mambo yakwetu tuyaongelee huku huku kwetu,nadhani Mh.Mark alisahau tarehe ya kura ya maoni walitangaziwa watanzania na mtangazaji akiwa nje ya nchi.
 
Chadema wanafikiri watachukuwa nchi kwa uongo.

Wajifunze kwa CUF.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…