Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,808
- 11,973
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) inayashikilia magari 10 ya wagonjwa ambayo yalikuwa yagawanywe kwa kata 10 za Jimbo la Same Magharibi na Mbunge wa Jimbo hilo Dkt. Mathayo David kama utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa mwaka 2015.
Magari hayo yalikuwa yagawanywe kwa kata hizo jana tarehe 08.07.2020 kupitia ofisi za CCM Wilaya ya Same lakini TAKUKURU ikaingilia kati na ikamuita Dkt. Mathayo na kumhoji kuhusu tukio hilo, kuelekea mchakato wa kupata wagombea ndani ya CCM kwa ajili ya uchaguzi mkuu