Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,808
- 218,456
Akizungumza Bungeni Dodoma , Festo Sanga ambaye ni Mbunge wa Makete kupitia CCM , amedai kwamba , Kwa vile Rais wa Nchi anafanya Maridhiano na vyama vya siasa vya upinzani , basi na vyama hivyo ni bora vikafanya maridhiano yao ya ndani.
Ndugu Festo akaendelea kuchangia bungeni kwamba, Nanukuu, " Haiwezekani chama kikubali ruzuku lakini kiwakatae wabunge wake wanaokipa ruzuku hiyo " mwisho wa kunukuu.
Labda kwa kumbukumbu , na hasa kwa wale wasiomjua huyu kijana ni kwamba Festo Sanga alianzia harakati zake Chadema akiwa mpambe au mshika mafaili wa Mtela Mwampamba, nadhani mnaweza kuelewa maana ya mshika mafaili au mbeba begi wa mtu mdogo kama Mtela, sasa baada ya Akina Mtela na Juliana Shonza kununuliwa na ccm na yeye akajichomeka huko, haijulikani ilikuwaje akawa mbunge wa Makete .
Siku zote tumeandika humu na kwa kurudia tena na tena kwamba Ruzuku za vyama vya siasa hazitokani na idadi ya wabunge wa viti maalum, sasa huyu ni mbunge ambaye hata utaratibu wa nchi haujui , Mtu kama huyu anawezaje kuwakilisha Jimbo?
Ni vema hawa wabunge duni kama huyu Festo wakitaka kujipatia umaarufu kupitia Chadema basi waje na hoja za maana
Ndugu Festo akaendelea kuchangia bungeni kwamba, Nanukuu, " Haiwezekani chama kikubali ruzuku lakini kiwakatae wabunge wake wanaokipa ruzuku hiyo " mwisho wa kunukuu.
Labda kwa kumbukumbu , na hasa kwa wale wasiomjua huyu kijana ni kwamba Festo Sanga alianzia harakati zake Chadema akiwa mpambe au mshika mafaili wa Mtela Mwampamba, nadhani mnaweza kuelewa maana ya mshika mafaili au mbeba begi wa mtu mdogo kama Mtela, sasa baada ya Akina Mtela na Juliana Shonza kununuliwa na ccm na yeye akajichomeka huko, haijulikani ilikuwaje akawa mbunge wa Makete .
Siku zote tumeandika humu na kwa kurudia tena na tena kwamba Ruzuku za vyama vya siasa hazitokani na idadi ya wabunge wa viti maalum, sasa huyu ni mbunge ambaye hata utaratibu wa nchi haujui , Mtu kama huyu anawezaje kuwakilisha Jimbo?
Ni vema hawa wabunge duni kama huyu Festo wakitaka kujipatia umaarufu kupitia Chadema basi waje na hoja za maana