Mbunge Ndaisaba Aibua Sakata la NIDA Mbele ya Naibu Waziri Mkuu

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,900
944

MBUNGE NDAISABA AIBUA SAKATA LA VITAMBULISHO VYA TAIFA (NIDA) MBELE YA NAIBU WAZIRI MKUU DKT. BITEKO

Mbunge wa Jimbo la Ngara Ndaisaba Ruholo amelalamikia kuwepo kwa unyanyasaji kwa wananchi juu ya upatikanaji wa vitambulisho vya Taifa hali inayopelekea wananchi wengi kukosa haki yao ya msingi

Akiongea mbele ya Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Dotto Biteko wakati wa hafla ya uwashaji umeme katika kijiji cha Ntanga Ruholo amesema kuwa wananchi wake wananyimwa haki ya kupata vitambulisho kwa sababu tu ya majina yao.

Amemuomba Dkt. Biteko kuwasaidia wananchi wa wilaya ya Ngara na maeneo mengine ya mipakani kwakuwa wamekuwa wakihangaika kupata huduma muhimu kwa kukosa kitambulisho cha Taifa.

Dkt. Biteko amewahakikishia wananchi wa wilaya ya Ngara na maeneo mengine ya mipakani kuwa wale wenye uhalali wa kupata vitambulisho hivyo watavipata na wala wasihukumiwe kwa majina yao.

Aidha amezionya taasisi zinazohusika na vitambulisho kuacha ukiritimba na urasimu badala yake watumie sharia na taratibu zinazo takiwa na wananchi wenye sifa basi wapatiwe vitambulisho vyao.

Sambamba na hilo amewataka wananchi kuwa wazalendo na kutoa ushirikiano pale wanapoona mtu ambaye hana sifa wala sio mtanzania anataka kupata kitambulisho basi wakamripoti kwenye mamlaka husika ili wale wenye haki yao waipate.
 

Attachments

  • img-20210409-wa0019-1024x678.jpg
    img-20210409-wa0019-1024x678.jpg
    77.1 KB · Views: 2

Similar Discussions

Back
Top Bottom