" Niwaombe watanzania wenzagu hii nuru tuliyonayo si kitu cha bedha wala siyo kitu cha kutikisa na kwenda kujaribu, na wasahili wanasema sumu haijaribiwi kwa kuonja tumejionea sisi wenyewe yaliyotokea. Wapo waloathirika hata ambao walikuwa hawahusiki na hayo mambo lakini tumeenda kuangamiza wasiokuwa na hatia kwa tamaa zetu sisi ama mambo yetu ambayo tunayatamani kwenye maisha yetu haya ya kwaida" - Amesema Mbunge Kunti Yusuph Majala leo Januari 27, 2026 katika Bunge la 13, Mkutano wa 2, Kikao cha 1.