Mbunge CHADEMA atetea posho mpya

KIROJO

Senior Member
Dec 7, 2011
169
21
PAMOJA na kusudio la kuongeza posho za wabunge kupingwa na vyama vya siasa, viongozi
wa dini na jamii, Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema) mkoani Rukwa, Anna Malack ameamua
kutetea kusudio hilo.

Mbunge huyo amesema kuwa wabunge walio wengi wanaishi maisha magumu kupindukia wanapohudhuria vikao vya Bunge mjini Dodoma kutokana na alichoita ukata mkali unaosababishwa na malipo duni wanayolipwa bungeni.

Alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki katika Kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya
Mji wa Mpanda baada ya madiwani hao kutoa ombi kwa Serikali ifute kabisa posho mpya za vikao vya wabunge.

Madiwani hao katika ombi lao waliitaka Serikali, badala ya kuongeza posho za wabunge,
iboreshe posho za madiwani ambazo walidai ni duni na zimepitwa na wakati.

Wakati wa kujadili suala hilo, baadhi ya madiwani walilaani uamuzi wa wabunge kutaka kujiongezea posho ya vikao wawapo bungeni kutoka Sh 70,000 hadi Sh 200,000 wakidai kuwa ni uamuzi wa kilafi, tamaa na ubinafsi unaowasukuma wabunge hao.

Hata hivyo, baada ya madiwani hao kutoa ombi hilo na maneno ya kulaani kusudio hilo, Mbunge huyo aliamua kueleza alichoona kuwa ndiyo hali halisi.

“Kama si kulima vitunguu mie na mume wangu, ningetegemea mshahara wa bungeni, ningekuwa nimeadhirika ile mbaya… baadae mtu unajuta kwanini umeingia kwenye siasa.

“Mfano unaamka asubuhi unafungua mlango na kukuta watu zaidi ya hamsini wanakusubiri wakiomba uwasaidie… baadae unalazimika kuuza vitu vya ndani ili uwasaidie.

“Ukifika nyumbani kwangu sina lolote zaidi ya kukutana na harufu kali ya vitunguu, huwezi
kuamini kama ni nyumba ya mbunge wenu.

“Wabunge kwa hali hiyo tunaadhirika, kama huna miradi ya kujiongezea kipato ndio umekwisha,” alisema.

Alisema kutokana na ukata baadhi ya wabunge wamekuwa wakikacha kurejea kwenye majimbo
yao ya uchaguzi na badala yake wanaamua kukaa Dar es Salaam.

*Hajapokea lakini anazitamani
Mbunge huyo alisema kuwa yeye binafsi hajawahi kulipwa posho mpya ya vikao vya Bunge na
kuongeza kwamba ofisi ya Bunge imekuwa ikiwazungusha kuwalipa na kusababisha afulie ile mbaya.

“Nadhani watu hawaelezi ukweli, malipo ya posho hizo mpya ni blaa blaa tu kwani mie binafsi sijawahi kulipwa hata siku moja isitoshe nimekuwa nikisoma kwenye magazeti na kusikia kwenye vyombo vingine vya habari.

“Labda kama ofisi ya Bunge imebagua na kuwalipa wabunge wengine watueleze tujue,” alisema.

Alidai kutokana na kutolipwa hiyo posho mpya wamepigiana simu na wabunge wengine na wamekubaliana kufanya mgomo wa kutoingia bungeni katika mkutano ujao wa Bunge hadi wafahamu hatima ya malipo yao.

“Bila kuwataja kwa majina wapo baadhi ya wabunge kutokana na ukata wanashindwa
kulipia nyumba za kulala wageni, wanalazimika kulala kwenye magari yao huku suti zao zikiwa zimetundikwa kwenye kiti cha nyuma, amini usiamini wanalia kama watoto wadogo,” alisema.

Akiunyambulisho mshahara wake alisema kama Mbunge analipwa Sh 70,000 za posho na
mshahara wake ni Sh 2,500,000 lakini baada ya makato anasalia na Sh 800,000 tu.

“Makato hayo ni ya gari nililokopa na makato mengineyo hivyo nimefulia ile mbaya…nikisafiri na gari langu kutoka Mpanda hadi Dodoma natumia Sh 700,000 kwa mafuta tu,” alisema.

Madiwani wakaza uzi Hata hivyo madiwani hao bila kuuma uma maneno, walimtaka mbunge huyo akienda bungeni atoe shilingi kwenye mshahara wa waziri husika akishinikiza posho za madiwani ziboreshwe.
source : Habarileo.
my take SIJAMUELEWA MWANDISHI WA HABARI HII
 
Nimewachoka hawa wabunge na kelele zao za posho! Kama wanaona wanaishi maisha magumu si wajitoe katika siasa? Nani anaishi maisha mazuri hapa! Kila mtu anapambana kadri awezavyo katika hali hii ngumu ya maisha. Wengine tuko ofisini mpaka saa 2 usiku mbona hatumpigii mtu kelele? Aghaaaaa!
 
Huyu Mbunge anaenda nje ya msimamo wa CDM wa kufuta posho. Penye red wananikumbusha tabia ya wabunge wa CDM kususia vikao vya bunge
 
PAMOJA na kusudio la kuongeza posho za wabunge kupingwa na vyama vya siasa, viongozi
wa dini na jamii, Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema) mkoani Rukwa, Anna Malack ameamua
kutetea kusudio hilo.

Mbunge huyo amesema kuwa wabunge walio wengi wanaishi maisha magumu kupindukia wanapohudhuria vikao vya Bunge mjini Dodoma kutokana na alichoita ukata mkali unaosababishwa na malipo duni wanayolipwa bungeni.

Alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki katika Kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya
Mji wa Mpanda baada ya madiwani hao kutoa ombi kwa Serikali ifute kabisa posho mpya za vikao vya wabunge.

Madiwani hao katika ombi lao waliitaka Serikali, badala ya kuongeza posho za wabunge,
iboreshe posho za madiwani ambazo walidai ni duni na zimepitwa na wakati.

Wakati wa kujadili suala hilo, baadhi ya madiwani walilaani uamuzi wa wabunge kutaka kujiongezea posho ya vikao wawapo bungeni kutoka Sh 70,000 hadi Sh 200,000 wakidai kuwa ni uamuzi wa kilafi, tamaa na ubinafsi unaowasukuma wabunge hao.

Hata hivyo, baada ya madiwani hao kutoa ombi hilo na maneno ya kulaani kusudio hilo, Mbunge huyo aliamua kueleza alichoona kuwa ndiyo hali halisi.

"Kama si kulima vitunguu mie na mume wangu, ningetegemea mshahara wa bungeni, ningekuwa nimeadhirika ile mbaya... baadae mtu unajuta kwanini umeingia kwenye siasa.

"Mfano unaamka asubuhi unafungua mlango na kukuta watu zaidi ya hamsini wanakusubiri wakiomba uwasaidie... baadae unalazimika kuuza vitu vya ndani ili uwasaidie.

"Ukifika nyumbani kwangu sina lolote zaidi ya kukutana na harufu kali ya vitunguu, huwezi
kuamini kama ni nyumba ya mbunge wenu.

"Wabunge kwa hali hiyo tunaadhirika, kama huna miradi ya kujiongezea kipato ndio umekwisha," alisema.

Alisema kutokana na ukata baadhi ya wabunge wamekuwa wakikacha kurejea kwenye majimbo
yao ya uchaguzi na badala yake wanaamua kukaa Dar es Salaam.

*Hajapokea lakini anazitamani
Mbunge huyo alisema kuwa yeye binafsi hajawahi kulipwa posho mpya ya vikao vya Bunge na
kuongeza kwamba ofisi ya Bunge imekuwa ikiwazungusha kuwalipa na kusababisha afulie ile mbaya.

"Nadhani watu hawaelezi ukweli, malipo ya posho hizo mpya ni blaa blaa tu kwani mie binafsi sijawahi kulipwa hata siku moja isitoshe nimekuwa nikisoma kwenye magazeti na kusikia kwenye vyombo vingine vya habari.

"Labda kama ofisi ya Bunge imebagua na kuwalipa wabunge wengine watueleze tujue," alisema.

Alidai kutokana na kutolipwa hiyo posho mpya wamepigiana simu na wabunge wengine na wamekubaliana kufanya mgomo wa kutoingia bungeni katika mkutano ujao wa Bunge hadi wafahamu hatima ya malipo yao.

"Bila kuwataja kwa majina wapo baadhi ya wabunge kutokana na ukata wanashindwa
kulipia nyumba za kulala wageni, wanalazimika kulala kwenye magari yao huku suti zao zikiwa zimetundikwa kwenye kiti cha nyuma, amini usiamini wanalia kama watoto wadogo," alisema.

Akiunyambulisho mshahara wake alisema kama Mbunge analipwa Sh 70,000 za posho na
mshahara wake ni Sh 2,500,000 lakini baada ya makato anasalia na Sh 800,000 tu.

"Makato hayo ni ya gari nililokopa na makato mengineyo hivyo nimefulia ile mbaya...nikisafiri na gari langu kutoka Mpanda hadi Dodoma natumia Sh 700,000 kwa mafuta tu," alisema.

Madiwani wakaza uzi Hata hivyo madiwani hao bila kuuma uma maneno, walimtaka mbunge huyo akienda bungeni atoe shilingi kwenye mshahara wa waziri husika akishinikiza posho za madiwani ziboreshwe.
source : Habarileo.
my take SIJAMUELEWA MWANDISHI WA HABARI HII

haijalishi kama amesema au hajasema yeye huyo mbunge. Matazamo wangu kwa wabunge ni kuwa ni kazi ambayo inalipa sana kuliko hata kazi nyingine au kwenye sekta nyingine 2meona au 2naona jinsi watendaji mbalimbali wakurugenzi,wakuu wa mikoa,wahadhiri na watendaji wengi sana ama walijaribu na wengine wamethubutu kuacha kazi kusudi wagombee ubunge,WABUNGEwengine kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu walithubutu kulalamika kuwa kuna watu wanajipitisha kwenye 'majimbo yao'.SWALI je ubunge haulipi? NA KAMA HAULIPI
{1} KWA NINI WENGI WAO WANAACHA TAALUMA ZAO NA WANAKIMBILIA HUKO ?
{2}MBONA HAWAJIUZULU AU KUACHA KAZI HIYO KAMA MASLAHI MADOGO?
{3}KWA NINI KIPINDI CHA UCHAGUZI WANATUMIA PESA NYINGI SANA KWA TAKRIMA NA RUSHWA? .
 
Kama kazi ya ubunge ni ngumu kwa nini hawa watu wasijiuzuru mbona bla bla nyingi sana
 
Shibuda kazini siyo issue, kuta ni kitu yake shibuda bungeni. Ok yupo cdm kweli lakini jina lenyewe ndio leo nalisikia. Hivi huyu alishawahi hata kuuliza swali kweli? Mwenye picha yake aiweke tafadhali. Tuwajue hawa walafi.
 
Kumbe ni wa Viti Maalumu.. Basi haina haja ya kumdiscuss..siyo kosa lake.
 
shida inakuja kwenye mamba wengi hata kenge wamo .Hata Ccm,cuf,TLp,Nccr kuna baadhi ya wabunge hawapendezwi na ongezeko hili la nyongeza za posho pia nadhani ni misimamo ya binfsi zaidi kuliko vyama .ila ningependa mbunge huyu ajue ubunge ni kuwatumikia wananchi sio kuwapa misaada wananchi .kumpa mtu msaada mtu ni kwa kila mtu sio mbunge tu .Akumbuke anatakiwa kuwafundisha watu jinsi ya kuvua samaki sio kuwapa samaki .kimtazamo wangu shida ndio ile ile ya viongozi wetu kukosa ubunifu wa kuwasaidia wananchi wetu jifunzeni kutoka china viongozi wao wengi ni leaders sio mabosi kama hapa kwetu ulikuwa na haja gani ya kuchukua Gari la milioni 90 wakati ungechukua hiyo hela na unge wekeza kwenye vitunguu shamba la jumuia la hao unaodai wanakusubiri mlangoni uwape msaada .wangepata ajira na pia wangekuwa na chama chao wange anzia hapo kuelekea kwenye mafanikio .kuongezwa posho sio tiba ya kumalizia matatizo ya wananchi wenu majimboni kuweni wabunifu .Natoa hoja
 
sina uhakika na hii post na ukizingatia source yenyewe kazi yake kubwa huwa ni kuipaka matope cdm na watu wake.It may be one among jukumu la hii source,so isitupotezee mda
 
Duh hii kali laiti angekuwa mbunge wa chama kingine tofauti na magwanda thread ingekuwa inakimbilia page ya 10 ahaaa aaa.
 
Duh hii kali laiti angekuwa mbunge wa chama kingine tofauti na magwanda thread ingekuwa inakimbilia page ya 10 ahaaa aaa.

chama gani pombe aina ya NGONGO kingine kitaje basi tuweze kuchangia zaidi
 
Back
Top Bottom