Mbunge aweka kando ubunge, afanya kazi ya kutoa `uchawi`

MAGEUZI KWELI

JF-Expert Member
Jul 16, 2011
1,947
253
NA THOBIAS MWANAKATWE
9th March 2012

Majimarefu.jpg

Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani


Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani maarufu Profesa Majimarefu, juzi aliweka ubunge wake kando na kurejea kazi yake ya uganga kwa kutoa ‘wachawi' katika kijiji cha Kwemazandu.

Mbunge huyo alifanya kazi hiyo baada ya kuhudhuria mkutano wa kijiji uliopitisha maamuzi ya kumtimua mmoja wa wanakijiji wao kwa tuhuma za kishirikina.

Akizungumza na NIPASHE kwa simu kutoka Korogwe, alisema alilazimika kufanya kazi hiyo wakati wa mkutano wa halmashauri ya kijiji ambao pamoja na mambo mengine, ulijadili suala la kijiji hicho kukosa mvua kwa kipindi kirefu.

Kufuatia kutonyesha kwa mvua hiyo, wakazi wa kijiji hicho walikuwa wakimtuhumu mkazi mwenzao, (jina limehifadhiwa) kwamba amekuwa akijigamba mitaani kuwa mvua kijijini hapo haitanyesha.

Baada ya wajumbe wa kijiji kuchangia kuhusu suala hilo, ndipo mbunge alipoondoka huku akiongozana na wajumbe hao pamoja na wananchi waliofurika kumwangalia, wakielekea katika nyumba ya mtuhumiwa huyo kwenye kitongoji cha Kimunyu.

"Jamani mnakumbuka kwenye kampeni nilivyosema, napenda niwakumbushe, nilisema kazi ya ubunge ni ya miaka mitano lakini kazi yangu ya uganga siwezi kuiacha nitaifanya hadi nitakapokufa," alisema Profesa Majimarefu.

Mbunge huyo baada ya kueleza hivyo aliongozana na mwenyekiti wa kijiji hicho, mtendaji wa kijiji na mwenye nyumba hizo kuingia nao ndani ya nyumba ya mtuhumiwa.

Baada ya kuingia katika nyumba hiyo, Profesa Maji Marefu alitoka akiwa na tunguri mbalimbali zilizodaiwa kumilikiwa na mtuhumiwa huyo.
 
Dah.....................! Hivi mpaka lini watz tutaongozwa na hawa wachawi? Ni bora tupate kiongozi ambaye ni mchungaji, padri au shehk kuliko kuwachagua wachawi wakatuwakilishe bungeni, Alafu wa2 wa pwani mnachekesha sana kwa kuamini imani potofu zay hadi leo hamfanyi mabadiliko ya kisiasa uchumi na kijamii.
 
Karne ya 21 tunafanya hivi!!! Hivi haya mambo kikatiba yameekaje?
 
NA THOBIAS MWANAKATWE
9th March 2012

Majimarefu.jpg

Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani


Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani maarufu Profesa Majimarefu, juzi aliweka ubunge wake kando na kurejea kazi yake ya uganga kwa kutoa ‘wachawi’ katika kijiji cha Kwemazandu.

Mbunge huyo alifanya kazi hiyo baada ya kuhudhuria mkutano wa kijiji uliopitisha maamuzi ya kumtimua mmoja wa wanakijiji wao kwa tuhuma za kishirikina.

Akizungumza na NIPASHE kwa simu kutoka Korogwe, alisema alilazimika kufanya kazi hiyo wakati wa mkutano wa halmashauri ya kijiji ambao pamoja na mambo mengine, ulijadili suala la kijiji hicho kukosa mvua kwa kipindi kirefu.

Kufuatia kutonyesha kwa mvua hiyo, wakazi wa kijiji hicho walikuwa wakimtuhumu mkazi mwenzao, (jina limehifadhiwa) kwamba amekuwa akijigamba mitaani kuwa mvua kijijini hapo haitanyesha.

Baada ya wajumbe wa kijiji kuchangia kuhusu suala hilo, ndipo mbunge alipoondoka huku akiongozana na wajumbe hao pamoja na wananchi waliofurika kumwangalia, wakielekea katika nyumba ya mtuhumiwa huyo kwenye kitongoji cha Kimunyu.

“Jamani mnakumbuka kwenye kampeni nilivyosema, napenda niwakumbushe, nilisema kazi ya ubunge ni ya miaka mitano lakini kazi yangu ya uganga siwezi kuiacha nitaifanya hadi nitakapokufa," alisema Profesa Majimarefu.

Mbunge huyo baada ya kueleza hivyo aliongozana na mwenyekiti wa kijiji hicho, mtendaji wa kijiji na mwenye nyumba hizo kuingia nao ndani ya nyumba ya mtuhumiwa.

Baada ya kuingia katika nyumba hiyo, Profesa Maji Marefu alitoka akiwa na tunguri mbalimbali zilizodaiwa kumilikiwa na mtuhumiwa huyo.[/QUOTE
Maji marefu ni tapeli kweli kweli kwa asie mjua atapata shida kumuelezea huyu bwana Ana ujuzi flani wa mazingaumbwe na uganga wake ni kama walivyo waganga wengi ambao wame vamia jiji la Dsm na Kama hawaja kudhuru hutajua ni wezi, maji marefu mwanzoni mwa miaka ya 90 ali wahi kufukuzwa Dsm akakimbilia Nrb huko ndiko aliko Patia pesa zilizo mpa
 
NA THOBIAS MWANAKATWE
9th March 2012

Majimarefu.jpg

Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani


Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani maarufu Profesa Majimarefu, juzi aliweka ubunge wake kando na kurejea kazi yake ya uganga kwa kutoa ‘wachawi’ katika kijiji cha Kwemazandu.

Mbunge huyo alifanya kazi hiyo baada ya kuhudhuria mkutano wa kijiji uliopitisha maamuzi ya kumtimua mmoja wa wanakijiji wao kwa tuhuma za kishirikina.

Akizungumza na NIPASHE kwa simu kutoka Korogwe, alisema alilazimika kufanya kazi hiyo wakati wa mkutano wa halmashauri ya kijiji ambao pamoja na mambo mengine, ulijadili suala la kijiji hicho kukosa mvua kwa kipindi kirefu.

Kufuatia kutonyesha kwa mvua hiyo, wakazi wa kijiji hicho walikuwa wakimtuhumu mkazi mwenzao, (jina limehifadhiwa) kwamba amekuwa akijigamba mitaani kuwa mvua kijijini hapo haitanyesha.

Baada ya wajumbe wa kijiji kuchangia kuhusu suala hilo, ndipo mbunge alipoondoka huku akiongozana na wajumbe hao pamoja na wananchi waliofurika kumwangalia, wakielekea katika nyumba ya mtuhumiwa huyo kwenye kitongoji cha Kimunyu.

“Jamani mnakumbuka kwenye kampeni nilivyosema, napenda niwakumbushe, nilisema kazi ya ubunge ni ya miaka mitano lakini kazi yangu ya uganga siwezi kuiacha nitaifanya hadi nitakapokufa," alisema Profesa Majimarefu.

Mbunge huyo baada ya kueleza hivyo aliongozana na mwenyekiti wa kijiji hicho, mtendaji wa kijiji na mwenye nyumba hizo kuingia nao ndani ya nyumba ya mtuhumiwa.

Baada ya kuingia katika nyumba hiyo, Profesa Maji Marefu alitoka akiwa na tunguri mbalimbali zilizodaiwa kumilikiwa na mtuhumiwa huyo.[/QUOTE
Maji marefu ni tapeli kweli kweli kwa asie mjua atapata shida kumuelezea huyu bwana Ana ujuzi flani wa mazingaumbwe na uganga wake ni kama walivyo waganga wengi ambao wame vamia jiji la Dsm na Kama hawaja kudhuru hutajua ni wezi, maji marefu mwanzoni mwa miaka ya 90 ali wahi kufukuzwa Dsm akakimbilia Nrb huko ndiko aliko Patia pesa zilizo mpa kiburi cha kugombea ubunge kama mnavyo jua wenzetu wa tanga tena waka mpa ,kipofu anaongoza vipofu wenzie
 
Dah.....................! Hivi mpaka lini watz tutaongozwa na hawa wachawi? Ni bora tupate kiongozi ambaye ni mchungaji, padri au shehk kuliko kuwachagua wachawi wakatuwakilishe bungeni, Alafu wa2 wa pwani mnachekesha sana kwa kuamini imani potofu zay hadi leo hamfanyi mabadiliko ya kisiasa uchumi na kijamii.

Ha ha haa...kaka mkuu wa nchi mwenyewe yumo...
 
Tatizo sio la huyo mbunge..tatizo ni wananchi wenyewe na eneo analotoka huyo mbunge.wlimu haijawasaidia ipasavyo.
 
Back
Top Bottom