Mbunge aliyedai waongezewe mshahara atakiwa aachie jimbo, CCM nao watoa kauli

Chongolo anatakiwa kuwa na hekima Sana ktk kuwajibu wabunge wa chama chake. Huyu ni mbunge, ana hadhi yake. Hata kama hoja yake inaleta maudhi lkn Chongolo kwa nafasi yake hakupaswa kutoa majibu ya kidikteta kiasi hiki.

Tisizilee kauli za kibabe kiasi hiki.
Ukileta hoja za kijinga unategemea majibu gani yanayolenga hoja zako ya kijinga?Upo msemo wa Kingereza usemao,"foolish answers for foolish questions."
 
Moja ya taasisi inayokula fedha za wananchi bila kazi yenye manufaa kwa Taifa ni bunge

1624519034186.png


1624519054791.png
 
Kuleana ndiko kunakoliangamiza taifa, kwanini yeye hakutumia hekima kuomba nyongeza ya mshahara huku akijua mwalimu anapata laki 3 kwa mwezi wakati yeye anaipata kwa siku.
Mwalimu kulipwa laki 3 siyo kosa la huyu mbunge, ni la mfumo. Na kosa hili la kimfumo halimzuii yeye kudai nyongeza ya mshahara wake.
 
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimemtaka Mbunge wa Mbogwe, Nicodemus Maganga kama anataka kuhudumia wananchi afuate utaratibu wa nchi na akitaka kulipwa kwa dola ahamie katika nchi zinazofanya hivyo.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo aliopohijiwa na gazeti la Nipashe

Kwa upande wake kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alipoulizwa na Nipashe kuhusu suala hilo alisema

Kama maslahi hayatoshi aache kazi ya Ubunge.

"Wabunge wasipoogopa wananchi hawatakuwa wabunge, Wakati Rais anawaambia wafanyakazi hawawezi kupandishia mishahara kwa sababu ya hali ya uchumi, Mbunge anataka malipo zaidi ni hujuma kwa Rais".

#NipasheView attachment 1828316
ZAO la UCHAFUZI wa UCHAGUZI MKUU 2020
 
Umesahau kuwa wabunge wenzie walimpigia makofi ya mikono na miguu na kushangiliwa. Unataka tupoteze tena mda wa kusikiliza kisichoendana na uhalisia
Sasa kwann chongolo anamtolea maneno ya kibabe kiasi hiki. Hajui nyuma ya kauli hii Kuna robo tatu ya wabunge wa chama chake?
 
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimemtaka Mbunge wa Mbogwe, Nicodemus Maganga kama anataka kuhudumia wananchi afuate utaratibu wa nchi na akitaka kulipwa kwa dola ahamie katika nchi zinazofanya hivyo.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo aliopohijiwa na gazeti la Nipashe

Kwa upande wake kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alipoulizwa na Nipashe kuhusu suala hilo alisema

Kama maslahi hayatoshi aache kazi ya Ubunge.

"Wabunge wasipoogopa wananchi hawatakuwa wabunge, Wakati Rais anawaambia wafanyakazi hawawezi kupandishia mishahara kwa sababu ya hali ya uchumi, Mbunge anataka malipo zaidi ni hujuma kwa Rais".

#NipasheView attachment 1828316
Hawa ni wabunge waliopitishwa na mwendazake baada ya wizi wa kura.
 
Huyu mbunge hakupaswa kuhukumiwa kwa hisia na machungu ya umaskini wetu. Alipaswa kupewa nafasi ya kufanya hata mdahalo wa wazi hivi ajenge hoja yake, kisha apigwe maswali na kuyatolea majibu.

Ukiangalia wachangiaji wengi ktk nyuzi zinazohusu kauli ya huyu mbunge, hakuna anayepinga kwa hoja kuntu. Wengi wanajadili utofauti uliopo Kati ya mshahara wa mbunge na wafanyakazi wengine.

Lkn hawajikiti kwenye mantiki ya hoja ya mbunge kwamba mshahara haumtoshi mbunge ukilinganisha na majukumu aliyo nayo.
Hajahukumiwa bado; kesi yake iko kwa wananchi hadi 2025 ndipo hukumu utajionea mwenyewe, kama ndiyo shida yako.
 
wengi sana hapo futa Special seats wote ,futa nominated by PRESIDENT wote ,punguza majimbo 170
Haya nitafanya hivyo bosi wangu, kama ni rahisi tu kiasi hiko -- Kufuta!!! Kufuta!!! Kufuta!!! Nawaambia njoeni tarehe 1 Julai tuandamane Bi Mkubwa katuharibia nchi, mnabaki tu Jeiefu kutaipu sijui nini.

Unadhani waliopigana na Mzungu hadi akakimbilia kwao, wangefanya hivi tungekuwa na uhuru leo!???

Tokeni mje tuandamaneeeee mguu kwa mguu kutoka Newala Mtwara hadi Missenyi Kagera, kupitia Magogoni na Chamwino then Msoga.

Mwenge tutauzimia kuleee Butiama baada ya kuhitimisha kazi. Au nasema uongo ndugu zangu!???
 
Alitakiwa kushusha nondo za kutetea maslahi ya mfanyakazi wa nchi hii bila kusahau mkulima, halafu ndo apandishe hoja yake ya maslahi ya wabunge.....utaona kabisa ubinafsi umemjaa.....
 
Back
Top Bottom