Mbowe: Nitamzungumzia Dk. Slaa muda ukifika

Mbowe: Nitamzungumzia Dk. Slaa muda ukifika

Kaimu Katibu wa Kichama Mkoa wa Kinondoni ROSE MUSHI mmmh! Hivi hakuna watu wengine hapo?
 
Mbowe mbona hakumuachia Lowasa uenyekiti wa chama kaamua kudalalia nafasi ya kugombea urahisi tu.

Matokeo yake chama kimegeuka dampo la mizoga ya kisiasa. Chama cha demokrasia ya magugu na ngano vikimea pamoja.

Kikao cha kamati kuu ya chama kinachoamua mambo mazito kama mgombea wa urais bila ya katibu mkuu hii iko vipi. Sikuwahi kufikiria kuwa huyu mbowe anaweza kuwa kiongozi wa hovyo kwa kiwango hiki.

Mh huyu awafahamishe waTZ kuwa alipewa nini kilicho pofusha hekima yake na kusimamia maamuzi haya ya hovyo.
 
"Nitazungumza na Dr Slaa muda ukifika" Mbowe. Na wala sio "Nitamzungumzia Dr slaa muda ukifika". Tafadhali kuweni makini, au mnafanya kusudi ili kupotosha?
 
Kuna propaganda chafu mno zinasambazwa juu ya Dr Slaa na kinachostua ni baadhi ya vijana wa Chadema wanashiriki kuvichochea.....fanyeni mizaha wakati mwingine si huu.....vijana tutumie akili zetu vyema.....tuna safari ndefu na taifa letu.....tusiwavunje moyo watu waliosimama nasi wakati wote mgumu.....
nakumbuka ulipomuambia mungi '' with all struggling umeharibu kise..... malizia maana naogopa!''
ukweli ni kwamba slaa keshaachia ngazi na barua ipo mezani kwa mbowe tatizo sasa ni jinsi gani watawaambia watu na mapokeo yake yatakuwaje. nashangaa mnashindwa kuelewa vitu vidogo kama hivyo
hata huyo mnyika naye alikuwa amfuate slaa, ndo maana hata alivyohojiwa hana majibu zaidi ya kusema siwezi kuongelea hilo-
fikirieni japo kidogo.
 
Kwa nini barua ya Dr Slaa ya kujiuzulu wameikalia kwa siku zote hizi? Ila Lowasa kuwa mwanachama na kuchukua fomu za kugombea urais ni matukio yaliyo tofautiana kwa masaa machache tu.
 
Back
Top Bottom