mwengeso
JF-Expert Member
- Nov 27, 2014
- 9,286
- 6,727
Vp mo kapatikana.hyo ya mbowe na hamahama bdo slow slow kashasema mwisho desemba wawahi.
Nyinyi na mbowe, sisi na nchi!
Mwambieni yule mwenyekiti kichaa wa chama cha makinikia aache kutumia nguvu za dola kupambana na fikra kinzani
Ninyi wanaCHADEMA, mlijadili suala la hamahama ndani ya chama kwa jicho pevu. Majibu rahisi hayo na shutuma hizo kwa upande wa pili hayatakitakijenga chama.Kama wewe na wenzio huko mliko sio mandondocha chukueni fomu za kagombea ubunge kule ukelewe! Kabla ya kuja kwa Mbowe anza na mtakatifu Yohana anayeendesha nchi na chama chenu kama mali yake binafsi!
Na isitoshe mnaonesha jinsi upeo wenu wa kuchambua masuala ya kisiasa ulivyo. Mnaona uovu lakini mnakuwa vipofu. Mnasikia mambo ya hovyo mnajifanya hamna masikio.
Jamii inachoshwa na kilio cha viongozi wa chama kudai ati hakuna demokrasia, Katiba inavunjwa, au kura zinaibiwa, wakati majukwaani hawanadi Sera zaidi ya vilio hivyo.
Watanzania wanahitaji vyama vya siasa vinavyoongozwa na viongozi walioiva kisiasa. Viongozi walio na uwezo na upeo wa juu kuchambua na kuzieleza, kwa ufasaha, Sera na Itakadi za vyama vyao kwa wapiga kura. Viongozi ambao hawatoi majibu mepesi kwa maswali magumu.
Jamii inataka kusikia na kuona kwa vitendo Sera na Mikakati mbadala ya kuiendeleza nchi hii kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiteknolojia.