Hamjambo.
Nimeona viongozi wa Chadema. Asilimia tisini wapo juu ya miaka 50+ huko.
Kwa umri huo sio umri tena wa kufanya harakati zile za hekaheka. Harakati zinazohitaji nguvu kubwa ya Mwili, akili na kuongea. Viongozi hao kimsingi wamejitahidi katika maisha Yao yote ya ujana kupigania kile walichokiamini.
Lakini wakati ni ukuta. Nimewaona mara kadhaa. Ingawaje bado wana ile shauku na ari lakini baolojia inakataa. Nyuso zao na miilo yao sasa inahitaji kufanya kazi zile za mezani. Na vijana kuingia katika nafasi.
Vijana kama Malisa, Martin Maranja, John Pambalu na kina Hilda ndio wakati wao huu kupokea kijiti kusukuma gurudumu. Swali linakuja wanao uwezo wa kutosha kupambana na Dude kubwa liitwalo CCM, dude lenye mizizi mirefu, joka lenye vichwa vingi, katili lisillo na huruma?
Au wanasubiri wakati CCM ikifa kifo cha asili?
Haya mjadala upo mezani