Mbowe, fumbo mfumbie mjinga, mwelevu ataling'amua

Mbowe, fumbo mfumbie mjinga, mwelevu ataling'amua

Dr Adam Francis

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2011
Posts
464
Reaction score
687
Nimevutiwa sana na mahojiano ya EATV na mbunge mstaafu wa Kilwa kusini, ndugu Suleiman Abdallah, almaarufu Bwege ya tarehe June 9, 2025.

Mahojiano hayo yaliyohusu mambo mengi ikiwemo, hali yake kiafya, vyama vya siasa na madai ya reforms kuelekea uchaguzi mkuu October 2025, nafasi ya ndugu Freeman Mbowe na ujio wa CHAUMA. Hili la mwisho ndilo ningependa kulizungumzia leo.

Katika mahojiano yake, ameeleza kuwa katika kulea vifaranga; utamaduni wa mama kuku ni kutangulia na vifaranga kumfuata lakini utamaduni wa bata ni vifaranga kutangulia na mama bata hufuata. Kwa maoni yake mpaka kufikia August, kwenye hili la CHAUMA, tutajua Mbowe kacheza kama bata au Kuku?

Ndugu Suleiman Abdallah anahitimisha kwa kusema, fumbo mfumbie mjinga, mwelevu ataling'amua. Amehoji; fumba na kufumbua, CHAUMA ya akina Kigaila imepata wapi uwezo wa kukodi Helikopter, kununua magari na kuanza kampeni nchi nzima?
 
file_00000000a19c61f7a8a31c72919aef6b.png
 
Watawala wakifanikiwa kumpeleka Mbowe CHAUMA itakuwa ni kete ya muhimu sana kwa wananchi. Hili litakuwa somo kubwa sana la siasa na wanasiasa kwa watanzani kuanza kujipigania wenyewe badala ya kudhani kuna mwanasiasa anayepigania maisha yao

Kimsingi kwa watu makini, litakuwa ni kosa kubwa la kimbinu na "ingekuwa" watanzania ni watu makini hili kosa watawala wangelijutia
 
Watawala wakifanikiwa kumpeleka Mbowe CHAUMA itakuwa ni kete ya muhimu sana kwa wananchi. Hili litakuwa somo kubwa sana la siasa na wanasiasa kwa watanzani kuanza kujipigania wenyewe badala ya kudhani kuna mwanasiasa anayepigania maisha yao

Kimsingi kwa watu makini, litakuwa ni kosa kubwa la kimbinu na "ingekuwa" watanzania ni watu makini hili kosa watawala wangelijutia
Umewaza vyema sana, yani ni bonge la mtego. Kama yupo smart asiingie kabisa!
 
Nimevutiwa sana na mahojiano ya EATV na mbunge mstaafu wa Kilwa kusini, ndugu Suleiman Abdallah, almaarufu Bwege ya tarehe June 9, 2025.

Mahojiano hayo yaliyohusu mambo mengi ikiwemo, hali yake kiafya, vyama vya siasa na madai ya reforms kuelekea uchaguzi mkuu October 2025, nafasi ya ndugu Freeman Mbowe na ujio wa CHAUMA. Hili la mwisho ndilo ningependa kulizungumzia leo.

Katika mahojiano yake, ameeleza kuwa katika kulea vifaranga; utamaduni wa mama kuku ni kutangulia na vifaranga kumfuata lakini utamaduni wa bata ni vifaranga kutangulia na mama bata hufuata. Kwa maoni yake mpaka kufikia August, kwenye hili la CHAUMA, tutajua Mbowe kacheza kama bata au Kuku?

Ndugu Suleiman Abdallah anahitimisha kwa kusema, fumbo mfumbie mjinga, mwelevu ataling'amua. Amehoji; fumba na kufumbua, CHAUMA ya akina Kigaila imepata wapi uwezo wa kukodi Helikopter, kununua magari na kuanza kampeni nchi nzima?
Mbowe aseme nini viongozi wa chama wapo.Mbowe akisema mtamwambia aache kuwashwawashwa.Pambaneni na hali yenu
 
Watawala wakifanikiwa kumpeleka Mbowe CHAUMA itakuwa ni kete ya muhimu sana kwa wananchi. Hili litakuwa somo kubwa sana la siasa na wanasiasa kwa watanzani kuanza kujipigania wenyewe badala ya kudhani kuna mwanasiasa anayepigania maisha yao

Kimsingi kwa watu makini, litakuwa ni kosa kubwa la kimbinu na "ingekuwa" watanzania ni watu makini hili kosa watawala wangelijutia
Chama pinzani hakipendi chama pinzani.
 
Nimevutiwa sana na mahojiano ya EATV na mbunge mstaafu wa Kilwa kusini, ndugu Suleiman Abdallah, almaarufu Bwege ya tarehe June 9, 2025.

Mahojiano hayo yaliyohusu mambo mengi ikiwemo, hali yake kiafya, vyama vya siasa na madai ya reforms kuelekea uchaguzi mkuu October 2025, nafasi ya ndugu Freeman Mbowe na ujio wa CHAUMA. Hili la mwisho ndilo ningependa kulizungumzia leo.

Katika mahojiano yake, ameeleza kuwa katika kulea vifaranga; utamaduni wa mama kuku ni kutangulia na vifaranga kumfuata lakini utamaduni wa bata ni vifaranga kutangulia na mama bata hufuata. Kwa maoni yake mpaka kufikia August, kwenye hili la CHAUMA, tutajua Mbowe kacheza kama bata au Kuku?

Ndugu Suleiman Abdallah anahitimisha kwa kusema, fumbo mfumbie mjinga, mwelevu ataling'amua. Amehoji; fumba na kufumbua, CHAUMA ya akina Kigaila imepata wapi uwezo wa kukodi Helikopter, kununua magari na kuanza kampeni nchi nzima?
Wewe ulivyomuona Bwege yuko sawa mpaka iwe rejea yako?
 
Ndugu Suleiman Abdallah anahitimisha kwa kusema, fumbo mfumbie mjinga, mwelevu ataling'amua. Amehoji; fumba na kufumbua, CHAUMA ya akina Kigaila imepata wapi uwezo wa kukodi Helikopter, kununua magari na kuanza kampeni nchi nzima?
Mbowe kwa asili ni mpiga dili. Hivyo amepiga dili la hela ya Samia kupitia kwa Abdul ndiyo kazipeleka kukodishia chopa ya Chauma..

Mbowe ana makengeza ya kwenye demokrasia tu, lkn hela anaiona vema sana.
 
Watawala wakifanikiwa kumpeleka Mbowe CHAUMA itakuwa ni kete ya muhimu sana kwa wananchi. Hili litakuwa somo kubwa sana la siasa na wanasiasa kwa watanzani kuanza kujipigania wenyewe badala ya kudhani kuna mwanasiasa anayepigania maisha yao

Kimsingi kwa watu makini, litakuwa ni kosa kubwa la kimbinu na "ingekuwa" watanzania ni watu makini hili kosa watawala wangelijutia
Tapeli tu wa siasa huyu. Mpaka namkumbuka Bw. Byakanwa kwa mambo aliyomfanyia huyu mwamba alivyokuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai. Kumbe huyu jamaa alikuwa sahihi.
 
Back
Top Bottom