Dotto C. Rangimoto
JF-Expert Member
- Nov 22, 2012
- 1,985
- 1,282
Tunakuhitaji bado kwani utumishi wako umetukuka, mbowe kaongoza chadema tangu 2004, hiki ni kipindi chake cha pili kinachoisha 2014, ni mwaka wa 9 sasa, na bado chama kinamuhitaji maana ameonesha utumishi uliotukuka hatuhitaji ccm watuchagulie kiongozi wetu ndani ya chama chetu. Tutamtaka hata aongoze miaka yote kwani anayo nia ya dhati ya kuwakomboa watanzania. Ni tangu lini chama cha siasa kikachaguliwa kiongozi na chama kingine? Ni kwa nini ccm hawamtaki mbowe wanamtaka zitto? Huhitaji shule kubwa kujua siri iliyopo hapa kwa zitto.
mwanachama kama wewe hufai na janga kwa chama na huna tafauti na watoto wa Lumumba wanaoamrishwa na mabwana zao wa ccm,,,wewe mbowe ni bwana wako????
Ccm ndio wanapiga kura kuchagua mwenyekiti wetu? Yaan tusichague kiongoz mwingne tafaut mbowe kisa tu kuwaogopa ccm? Hivi kwa katiba gani wataka mbowe awe kiongoz wa milele??? Au ndio kawatuma muandike huu utumbo kwenye mitandao? Mmeshafanya mbowe mjinga?? Kwa hivyo mnaamua sasa kuumpa sifa za kijinga? Kwasababu ni mjinga pekee ndio ataambiwa kuwa atatawala milele katika ulimwengu wa demokrasia na mabadiliko.
Mbowe ndio kawafundisha kuimba nyimbo za usaliti bila kuzingatia hoja za wasaliti? Mbowe ndio kawafundisha kujadili mtoa hoja badala ya hoja? Hivi kwanini mnapenda kumdhalilisha mwenyekiti wetu? Hivi kwanini mnatulazimisha tuamini kuwa Mbowe naye ana mkakati wake mchafu wenye lengo la kumbakisha madarakani?
Acheni ushabiki wa kimbulumundu,, tusimamie misingi ya chama na katiba, kinyume chake hamtakuwa tafauti na watoto wa Lumumba.