Kama ilivyo ada na kawaida ya Mh Mbowe kutoa matamko ya kiulaghai na uongo kwa kudai kwamba huwa ana ushahidi wa mambo mbalimbali yanayotokea ktk mustakbali wa siasa za nchi yetu, kama alivyowahi kudai siku zilizopita, ambapo alidai ana video ya ushahidi wa Bomu la Olasiti Arusha, na pia Maswala ya Mwangosi na yale matukio ya waandishi kumwagiwa tindikali, ushahidi ambao hajawahi kuutoa kwenye vyombo vya sheria, leo kaja na mpya baada ya kudai ana ushahidi kutoka vikao vya ndani vya ccm kwamba eti hawataki kutekeleza mchakato wa katiba mpya bali wanawalaghai tu ili waingie ndani ya bunge la katiba na kisha waamue kufanya watakavyo. My take, kwa kuwa huyu mh Mbowe amekuwa ni mtu wa kudai kuwa ana ushahidi wa mambo mengi tena yeye tu, itabidi vyombo vya dola vimbane ili aisadie polisi katika mengi ambayo yanahusisha jinai ili haki ipatikane kwa wahanga.
Vipi ushahidi wa Mwigulu ameshautoa mbinguni au kautoa duniani?Anachofanya sasa ni kero tupu! Kila siku, ana ushahidi na hautoi popote aagh!
vipi mwigulu na ushaidi wake wa ugaidi???
No research,no right to speak.Unajua kuna watu wengine hata uletaji mada yake utajua ni kanjanja,unaweza ukapoteza muda wako kubishana naye na energy.Kubishana na watu wa buku 7 ni kazi sana,wengi unakuta wamelishwa maneno.
Kama kuna mtu anaamini kuwa chini ya bunge maalumu lililojaa maccm linaweza kutupatia katiba mpya basi mtu huyo ni wa kuhurumiwa daima! Ccm hawana dhamira ya dhati ya kutupatia katiba mpya kamwe!
MKUU point ya msingi sana umeanza nayo, kama mtu hajafanya utafiti wa jambo basi hana haki ya kuliongelea, nakubali kabisa, lakini ujumbe huu ungeuelekeza kwa mhe Mbowe, ambaye ndiye tatizo kwenye mada yetu ya leo, kwa kuropoka ovyo kuwa ana ushahidi wa jambo fulani wakati hana. Elekeza kwake mchango wako mkuu.
sasa hapo ulaghai uko wapi? Mbona yotyote aliyoyasema ni ukweli mtupu.Kama ilivyo ada na kawaida ya Mh Mbowe kutoa matamko ya kiulaghai na uongo kwa kudai kwamba huwa ana ushahidi wa mambo mbalimbali yanayotokea ktk mustakbali wa siasa za nchi yetu, kama alivyowahi kudai siku zilizopita, ambapo alidai ana video ya ushahidi wa Bomu la Olasiti Arusha, na pia Maswala ya Mwangosi na yale matukio ya waandishi kumwagiwa tindikali, ushahidi ambao hajawahi kuutoa kwenye vyombo vya sheria, leo kaja na mpya baada ya kudai ana ushahidi kutoka vikao vya ndani vya ccm kwamba eti hawataki kutekeleza mchakato wa katiba mpya bali wanawalaghai tu ili waingie ndani ya bunge la katiba na kisha waamue kufanya watakavyo. My take, kwa kuwa huyu mh Mbowe amekuwa ni mtu wa kudai kuwa ana ushahidi wa mambo mengi tena yeye tu, itabidi vyombo vya dola vimbane ili aisadie polisi katika mengi ambayo yanahusisha jinai ili haki ipatikane kwa wahanga.
kama kuna mtu anaamini kuwa chini ya bunge maalumu lililojaa maccm linaweza kutupatia katiba mpya basi mtu huyo ni wa kuhurumiwa daima! Ccm hawana dhamira ya dhati ya kutupatia katiba mpya kamwe!
Kama kuna mtu anaamini kuwa chini ya bunge maalumu lililojaa maccm linaweza kutupatia katiba mpya basi mtu huyo ni wa kuhurumiwa daima! Ccm hawana dhamira ya dhati ya kutupatia katiba mpya kamwe!