Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amewasili muda huu katika msiba nyumbani kwa marehemu Edwin Mtei, aliyefariki dunia Januari 19.
Mtei alikuwa ni mwasisi wa CHADEMA pamoja na mwenyekiti wa kwanza wa chama hicho. Kufuatia kifo chake, CHADEMA imetangaza maombolezo ya siku saba kama sehemu ya kuenzi mchango wake mkubwa katika historia ya chama hicho na siasa za Tanzania.
Kwa mujibu wa Katibu wa CHADEMA Kanda ya Kaskazini, Ndondi Totinam, viongozi mbalimbali wa chama pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wanaendelea kuwasili msibani leo, huku wengine wakitarajiwa kufika kesho.
Mtei alikuwa ni mwasisi wa CHADEMA pamoja na mwenyekiti wa kwanza wa chama hicho. Kufuatia kifo chake, CHADEMA imetangaza maombolezo ya siku saba kama sehemu ya kuenzi mchango wake mkubwa katika historia ya chama hicho na siasa za Tanzania.
Kwa mujibu wa Katibu wa CHADEMA Kanda ya Kaskazini, Ndondi Totinam, viongozi mbalimbali wa chama pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wanaendelea kuwasili msibani leo, huku wengine wakitarajiwa kufika kesho.