Los técnicos
JF-Expert Member
- Sep 14, 2014
- 3,015
- 2,645
Bada mnaamini sisi wananchi ni wajinga kiasi hicho kwamba tutalikabidhi jimbo bila kukaa chini na kutathimini kabla ya uamuzi huo?
Ujinga wenu ninyi vijana ni kudhani mnayo haki ya kumfanyia maamuzi mtu, wakati ninyi mnaweza tu kumshauri rais kutimiza ahadi zake.
Mtu kuchaguliwa ni baada ya kupambanua hoja, na kujibu hitaji la wananchi ni nini atawafanyia? Na kuwaahidi atakuwa ni kiongozi wa namna gani.
Si vyema kujipa uhakika kwa jambo ambalo maamuzi yapo kwa mtu mwingine ni ujinga
Ujinga wenu ninyi vijana ni kudhani mnayo haki ya kumfanyia maamuzi mtu, wakati ninyi mnaweza tu kumshauri rais kutimiza ahadi zake.
Mtu kuchaguliwa ni baada ya kupambanua hoja, na kujibu hitaji la wananchi ni nini atawafanyia? Na kuwaahidi atakuwa ni kiongozi wa namna gani.
Si vyema kujipa uhakika kwa jambo ambalo maamuzi yapo kwa mtu mwingine ni ujinga
Kwa maneno haya ya DC wa Hai Lengai Ole Sabaya aliyo yaongea mbele ya vijana wa Uvccm mkoa wa Kilimanjaro je Mbowe Atarudi kweli 2020?
"Ule wakati wa kuwageuza geuza watu kama chapati umepita, Alikuja Rais Kikwete mkamuita dhaifu, Sawa Yupo huyu Rais wa kazi mnamuita Dickteta, Ni mwananchi mwenye akili anaweza kukubali kila asubuhi kugeuzwa geuzwa.
HESABU HAZIDANGANYI,Kwa kazi za heshima zinazoendelea nchi hii jimbo la Hai mtalisahau, Nendeni kapigeni kura kwenye mitandao kwenye kura zenu za maruani, na kama mnanijaribu mwezi
October wapiga kura watawafurahisha.
NIMEKUJA HAPA KUWATAARIFU KUWA hao chadema watashinda face book ,insta na Jamii forum na sio Hai.
Jimbo la Hai ni mali ya wananchi na watalikabidhi kwa chama cha wakulima na wafanyakazi CCM.nimeyasema haya hadharani na nimemaliza".