Pakome
JF-Expert Member
- Dec 8, 2024
- 1,541
- 916
Kiongozi mwenye busara analinda Wanachama wake lakini kiongozi asiyekuwa na hekima Wanachama wake watapoteza uhai
Mbowe angekuwa ndiye Mwenyekiti wa CHADEMA, hakuna mwanachama wake angepoteza maisha October
Hii ni kwasababu Mbowe alikuwa anatumia hekima na busara kuongoza CHADEMA kwa miaka yote
Hakuwa akiongoza CHADEMA kwa namna hii ya kilimbukeni inayoongoza sasa
Hekima na busara zake ndizo zilipofusha CHADEMA waone kuwa ni Mwenyekiti asiyekuwa na sifa za uongozi
Wakadhani kwamba anawachelewesha kumbe Lissu alipowawahisha wakaishia kupoteza maisha
CHADEMA ya sasa iliamini kuwa Lissu ndiye rubani mzuri ila matokeo yake ameangusha ndege na yeye pia ameumia
Matokeo yake ikapelekea Wanachama wengi wa CHADEMA kupoteza nafasi za Ubunge na mbaya zaidi kupoteza maisha October
Lissu alirusha ndege isiyokuwa na dira ikaishia kuanguka na kupoteza maisha ya Wanachama
Sio maisha tu bali hata Chama kimepoteza Mwenyekiti wake pamoja na ndoto za kukamata dola
Kwa ufupi ni kuwa Chama kilidhani kikimtupa Mbowe kitafanikiwa ila kimepoteza kila kitu yaani CHADEMA imegawana hasara, wote wamekosa
Mbowe alilia sana kwa kutukanwa na Wanachama wa CHADEMA na hakuna aliyemfuta machozi badala yake waliishia kumdhihaki na huu ni wakati wa Wanachama wa CHADEMA kulia kama alivyolia yeye
Imekuwa ni mwendo wa kugawana hasara
Kama CHADEMA ilimchoka Mbowe basi ingemuaga kwa heshima kubwa lakini sio kwa namna ile ya Matusi hii ni kwasababu Mbowe hakuwa kiongozi mbaya na kama alikuwa mbaya basi wasingepokea CHADEMA iliyokuwa imesheheni idadi kubwa ya Wanachama walioipa CHADEMA sifa ya Chama Kikuu Cha Upinzani
Mbowe angekuwa ndiye Mwenyekiti wa CHADEMA, hakuna mwanachama wake angepoteza maisha October
Hii ni kwasababu Mbowe alikuwa anatumia hekima na busara kuongoza CHADEMA kwa miaka yote
Hakuwa akiongoza CHADEMA kwa namna hii ya kilimbukeni inayoongoza sasa
Hekima na busara zake ndizo zilipofusha CHADEMA waone kuwa ni Mwenyekiti asiyekuwa na sifa za uongozi
Wakadhani kwamba anawachelewesha kumbe Lissu alipowawahisha wakaishia kupoteza maisha
CHADEMA ya sasa iliamini kuwa Lissu ndiye rubani mzuri ila matokeo yake ameangusha ndege na yeye pia ameumia
Matokeo yake ikapelekea Wanachama wengi wa CHADEMA kupoteza nafasi za Ubunge na mbaya zaidi kupoteza maisha October
Lissu alirusha ndege isiyokuwa na dira ikaishia kuanguka na kupoteza maisha ya Wanachama
Sio maisha tu bali hata Chama kimepoteza Mwenyekiti wake pamoja na ndoto za kukamata dola
Kwa ufupi ni kuwa Chama kilidhani kikimtupa Mbowe kitafanikiwa ila kimepoteza kila kitu yaani CHADEMA imegawana hasara, wote wamekosa
Mbowe alilia sana kwa kutukanwa na Wanachama wa CHADEMA na hakuna aliyemfuta machozi badala yake waliishia kumdhihaki na huu ni wakati wa Wanachama wa CHADEMA kulia kama alivyolia yeye
Imekuwa ni mwendo wa kugawana hasara
Kama CHADEMA ilimchoka Mbowe basi ingemuaga kwa heshima kubwa lakini sio kwa namna ile ya Matusi hii ni kwasababu Mbowe hakuwa kiongozi mbaya na kama alikuwa mbaya basi wasingepokea CHADEMA iliyokuwa imesheheni idadi kubwa ya Wanachama walioipa CHADEMA sifa ya Chama Kikuu Cha Upinzani