CCM situ kwamba hawataki hoja ya serikali tatu ndani ya katiba mpya bali hawataki kabisa katiba mpya. Anayetaka katiba mpya ni Kikwete yeye binafsi wala si taasisi ya Rais. Kumbuka Mwnasheria mkuu wa Serikali ambaye ni shabiki No1. wa sisiem aliwahi kusema haoni haja kuwa na katiba mpya maana hii iliyopo inakidhi matakwa ya watanzania. Celina Kombani akiwa waziri wa katiba na sheria aliwahi tanka kuwa hakuna mpango wowote wa kuwa nakatiba mpya kwakuwa iliyopo inatosha na kama kunahaja ya kushughulika na jambo lolote basi itafanyiwa marekebisho.
CCM haikuwahi kuwa na agenda ya katiba mpya, hii kikwete aliibua tu katika kutafuta umaarufu na kuacha kichu cha kumfanya akumbukwe. Kwa hilo walau amejaribu ingawa anapambana na vikwazo vingi kutoka katika chama chake.
Akina Lukuvi, Wasira, Chikawe, Werema hao ndio kabisaaaaaaa hawataki kusikia maana hata kusikia JK anawaalika wapinzani Ikulu inakuwa nongwa kwao, wanadhani wapinzani watamaliza juice yote ikulu. Kwahiyo njia iliyobuniwa na wasiotaka katiba ni kuweka utaratibu utakaoruhusu wajumbe wengi wa sisiemu ili watibue mchakato wote.
Wapinzani sasa inabidi kujiandaa kwa plan B ya matokeo ya mchakato wa katiba bila kusubiri matokeo ya kura za maoni. Kuwa endapo ccm watafaulu kuondoa hoja ya serikali tatu, lakini tume ya uchaguzi ikawa huru na baadhi ya vipengele vya kuleta manufaa kwa wanachi vikapita, si bora tupokee hivyo kwanza halafu hatua itakayo fuata ni kuhamasisha wazanzibari wadai ASP yao ili tuone kama TANU haitachomoza, na hapo ndipo msajili wa vyama atakapopata kazi ya kuisajili upya TANU.