Mbona Afrika hatuandamani kupinga mauaji ya kikatili na kifedhuli ya mweusi mwenzetu?

Zaid ya hapo uwoga wa wananchi wenyewe. Atleast wenzetu wanadhubutu kuandamana. Sisi huku jaribu tu kidogo . Inakuwa vita
Sio uoga. Ni hali ya usalama wetu ndio tunaozingatia. Ukiniambia mie kuandamana kwangu sio ishu nina guts ila nikifikiria kuwa kuna nguvu kubwa sana itatumika dhidi yangu ikiwa inaweza kuondoa hata uhai wangu inakuwa meaningless. Siwezi andamana kama nitapigwa risasi nife na familia yangu ibaki ikiteseka. Siwezi andamana!!!

Unafikiria hata hao US wangejengwa kisaikolojia kwamba wakiandamana kuna kufa kuna mtu angetoa pua nje hata? Ni saikolojia kwa wenzetu wana hofu na katiba na wanajali haki za binaadamu. Hawana mambo ya kijinga kama Afrika.
 
hayo maandamano ni kwa watu ambao hata akiumka mwili basi ana bima ya afya na pia ana account yenye pesa za kujikimu..mwenzangu na mimi hapa nivunjwe mguu ilihali nilichonacho kwenye maisha yangu ni kumiliki no ya NIDA tu wapi na wapi
 
Ndiyo ukweli halisi..
Utapigwa kama mbwa koko, familia itateseka kujaribu kukunusuru na kesi ya uhujumu uchumi na utakatishaji fedha na madawa ya kulevya.

It's not worth it...

Everyday is Saturday........................
Nyerere na wenzake wangesema hivyo wakati wa ukoloni tungekuwa wapi sasa?
 
Nyerere na wenzake wangesema hivyo wakati wa ukoloni tungekuwa wapi sasa?
Wakoloni hawakuwahi kuwapiga kina Nyerere na co kama mbwa koko...
Mkuu Kiranga, HISTORY niliyosomeshwa mimi haina manyanyaso ya viongozi wa TAA na TANU, kuchezea virungu wala kufyatuliwa risasi.

Na inasikitisha kuona tumejitawala wenyewe tunatumia mabavu na nguvu kuliko mkoloni.

Everyday is Saturday........................
 

Hao kina Nyerere ndio wanatutesa na kutupiga sisi. Adui wa Muafrica ni Muafrica mwenziwe
 

Kwa wazo langu hiyo ni kawaida sana ukilinganisha na yanayotokea Africa kuna watu wanafanyiwa unyama zaidi ya huyo na ni weusi sijawahi kuona hawa blac american wanaandamana jinsi Congo, Libya n.k wanafanyiwa ukatili na Serikali zao ndio wahusika.

Haya maandamano ni kutokana na njaa ya lockdown na si kusema wanataka haki.
Wengi wao ni wezi tu wanavunja maduka na kuiba suala la haki iko wapi?

Halafu wakati mwingine huyo askari alifanya kosa kama kosa lingine kuna waamerika wangapi whites wameuwawa kwa njia za kihuni? Na wengine wameuwawa na wazungu wenzao wengine na black hawakuiona hilo? hatukuona maandamano kwa hiyo tusiinhilie mambo ya watu
 
Tutaharibu maandamano na kukwamisha lengo la Wamarekani. Maana wataachana na agenda yao na kuanza KUANDAMANA KUPINGA MAUAJI WA WAANDAMANAJI AFRIKA.... Over.
 
Ulishawahi kusikia wao wameandamana kwa ajili yako? Acha wapambane na mambo yao kwanza
 
Jiulize kwa nini wewe hauandamani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…