Kilasara
JF-Expert Member
- Dec 21, 2008
- 577
- 116
Mwenge wa Uhuru mwaka mmoja ulilala katika uwanja wa mpira katika kijiji chetu. Kesho yake, katika uzio wa kiwanja ziliokotwa sio chini ya mia moja ya mipira ya kondom iliyotumika katika ngono za fujo usiku ule.
Inasemekana kwamba katika mkondo wa njia unapopitia Mwenge wa Uhuru kila mwaka, kunakuwa na milipuko ya gonjwa hili, na vijana wengi huangamia miaka michache baadae.
Kama madhumuni ya Mbio hizi za Mwenge wa Uhuru ni kuhamasisha wananchi kuchangia miradi ya maendeleo, ni maoni yangu kwamba tubuni mbinu m'badala isiyoambatana na ngono za fujo kwa vijana wetu. Kama madhumuni ni kutukumbusha historia ya Tanzania, basi tuandike kumbu kumbu zetu na tudhamirie kwa dhati kuzikumbuka kwa njia nyingine.
Tukiendelea na staili hii ya kukusanya vijana wetu katika makundi yanayohimiza ngono zembe tutajiangimiza kama taifa.
Inasemekana kwamba katika mkondo wa njia unapopitia Mwenge wa Uhuru kila mwaka, kunakuwa na milipuko ya gonjwa hili, na vijana wengi huangamia miaka michache baadae.
Kama madhumuni ya Mbio hizi za Mwenge wa Uhuru ni kuhamasisha wananchi kuchangia miradi ya maendeleo, ni maoni yangu kwamba tubuni mbinu m'badala isiyoambatana na ngono za fujo kwa vijana wetu. Kama madhumuni ni kutukumbusha historia ya Tanzania, basi tuandike kumbu kumbu zetu na tudhamirie kwa dhati kuzikumbuka kwa njia nyingine.
Tukiendelea na staili hii ya kukusanya vijana wetu katika makundi yanayohimiza ngono zembe tutajiangimiza kama taifa.