Mbinu za ushindi katika chaguzi - Zitto Kabwe

Mbinu za ushindi katika chaguzi - Zitto Kabwe

Hii umetoa wapi R.B?

Bado sijawa na imani na Zitto kabwe maana 2014 ataibuka tena na sarakasi zake dau alilipewa ni kubwa sana haliwezi kupotea hivi hivi bila kufanya kazi

Chezea mtu aliyepitiwa umeme wa Gamba

Mmhh...kapewa shillingi ngapi? Zimwage hapa na ushahidi.(SIKUPINGI WALA SIKUUNGI MKONO KATIKA HILI).
 
makala ni nzuri!
Lakini si muamini mtoa makala hata kidogo!

Hivi haya makundi anayo sema yaliyo sababisha tupoteze umayor wameundwa na nani mpaka ana lalamika kwa wananchi?

Ni mchango wa mtoa makala katika kuvunja hayo makundi? Inawezekana tukawa watu wakulalamika tuu,oooh kuna makundi lakini hatuna mchango wowote kuyaondoa zaidi ya kukaa pembeni na kuangalia hadi mambo yanapo haribika ndio tunasema!

Mtoa makala kaandika vizuri lakini kwa muda huu ni wazi anatafuta huruma ya wananchi ili aonekane halikuwa hakikerwa sana wakati alikuwa na nafasi ya kuweka mambo sawa!

Pengine kuliko kukaa chini na kuandika makala unge kaa chini na kuanza kulalamika wakati una nafasi na kwenye vikao unakuwepo! Kwanini usiongeee uko? Tatizo limeshatokea wewe unatoa makala utafikiri uko nje ya chama! Umefanya juudi gani kutatua tatizo!

Mwandishi wamakala ana onekana kulalamika hili wananchi wasitoe lawama kwake lakini watoe kwa wengine!

with pm7 & masalia...any thing is possible.
 
Andiko zuri but naona kama huu ni mkakati wa ushindi wa chama sasa unatokaje kwenye public?
je tunataka kuwakumbusha washindani wetu namna ya kufanya mambo ili washinde?

ZKK kama ndie aliyeandika sina imani nae na cjui kwanini anafanya hivi

Huyu ni mnafiki hebu angalia alivyoelezea kuhusu arumeru mashariki na anasema kulikuwa na umoja hivi si ndo ZKK aliyeenda kutangaza kugombea urais wakati wenzake wapo bize kupigania jimbo?

Nisaidie kuuliza na kushangaa..huyo jamaa mimi pia sina imani naye kabisa.
 
Watu wanafiki huwa wanaadhibiwa haraka sana. Hakuna kitu kibaya kama unafiki maana watu wanatoa maisha yao kukuamini alafu wewe unawasaliti. Tena hao watu ni maskini hawana kimbilio ss wameona wewe ndo kimbilio mtu unayeweza kuwaletea ahueni alafu unawasaliti unafikiri utaacha kuadhibiwa. Oh! time will tell
 
hizi makala zinatoka kwenye gazeti la Tanzania Daima so mleta mada kaamua kushare hapa jukwaani.

Waambie hao!wazee wa kadi 2 wanashindwa kabisa kujiamini,mutakufa kihoro bure ndugu zanguni,just relax.
 
Yani zk kweli harakati zako zote mwisho umeamua kutusaliti kwa kuwatumia vijana wa kimasalia leo hii baada ya arumeru kutaka kutuondoa kwenye lengo kujitangaza unawania uraisi usema ubinafsi sio issue mbona uliupa nafasi,
Kama unaitakia mema chadema uliyoyaeleza umeyasimamia kwenye chama chako kwa namna unaelimisha vingine leo
Mwisho nakushangaa madhaifu yaliyojitokeza chadema unayashitakia kwa wananchi kana kwamba wewe hukuwa kiongozi au mwanachama hivyo unawaelimisha.
We si mtu wa kufanya siasa za wakina shonza mchana chadema usiku ccm nimeshangaa kumbe wewe ndo uliwafundisha BEN AMEWAKOMESHA ngoja dawa yako kamati kuu wanaiandaa walikuonya enzi zile mpaka ukaundiwa kamati ya wakina Prof. Baregu kukushauri ukajifanya much know Nakuambia utalia kama Kafulila siku mbatia anamwadibisha haitasaidia
 
makala ni nzuri sana tuache tofauti zetu kama anavyosema ili tujenge chama imara

Asante!!
 
Asante mh Zitto waache wasiokupenda watoe macho ww unakubalika sana na wananchi walioko mijini na hata vijijini achana na hawa wachache wa mtandaoni.
 
Huu ni mwendelezo wa ZITTO kuomba huruma yetu sisi wapenzi na wanachama wa CHADEMA nadhani anatakiwa akatubu kwanza kwa wajumbe wa KAMATI KUU ili wao watupe muongoze kama tumsamehe au tumdharau kama SHIBUDA.
 
Ndio zitto ; tunasubiri party 2... Muendelezo
 
Zitoo ni Naibu Katibu ila haminiki kutokana na tamaa zake na ukigeugeu wake.
Zito huna sababu ya kutoa makala hii gazetini kwani wewe ni makamu mwenyekiti, unaweza kuliongea hili kwenye vikao vya chama, sasa hivi unatakiwa kutubu urudi kikosini. Acha undumilakuwili
 
Kazi nzuri Mh Zitto may be itapunguza hasira za wana CDM kutokana na kundi lako la masalia na kuhujumu CDM. Maana watu wako Arumeru we Unatangaza kugombea Urais sa sijui ulisaidia vipi ushindi wa Joshua Nasari
 
Nasi hatutaki uwe muumini wake bali fuata misingi achana una uumini wa mtu. Na kama unataka uumini nenda Kanisani au msikitini
 
Back
Top Bottom