mtarimbo
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 1,529
- 3,919
Urusi kiukweli wameonesha umahiri wa kutumia mbinu za enzi ya kina hitla na dola la kirumi katika uvamimizi.Kabla sijaelezea mbinu hizo naomba ufahamu kuwa Urusi haikua na malengo ya kuivamia Ukraine yote,bali ililenga maeneo ya eastern part yaliyopakana na mipaka yake ,lengo ikiwa ni kuyasaidia majimbo yaliyikua yanataka kujitenga na Ukraine ,kumbuka mipango iliandaliwa tangu 2010,na propaganda nyingi ziliundwa na mrusi ili kuchochea majimbo hayo kujitenga.sitaki kwenda deep mnaelewa hizo siasa za mrusi.
Sasa nije kwenye mbinu ya kuhakikisha wanyakwapua majimbo hayo,maana walielewa fika wakienda kichwakichwa wangeumbuka mno.
Kwanza kabisa walijigawa makundi matatu ,ambapo kundi la kwanza lilitangulia upande wa mji mkuu Kiev kama vile wanataka kuingia mjini,ila walikua wanazuga tuu ili kuvuruga mipango ya jeshi la Ukraine ,na kweli lilivurugika kweli maana Ukraine ilijikita kutumia nguvu nyingi kuzuia jeshi la Russian kuingia mji mkuu Kiev, huku wakisahau kuna kundi lilikua linazunguka Eastern na kujiimarisha huko
Kundi la pili lilijikita kama linataka kutokea upande wa kaskazin kupitia Belarus ila nao ilikua zuga tuu.
Kundi la tatu ndilo la kifo lilijikita majimbo ya mashariki likiwa na shehena ya silaha nyingi na kujiimarisha huko ,huku wenzao wakiendelea kuzuga ,mbinu hii inaitwa cover the main target
Wakati mataifa ya ulaya na dunia wakimzomea puttin kwamba kashindwa kutimiza lengo lake la kuingia Kiev ,yeye aliendelea kujiimarisha zaidi
Baada ya kuhakikisha ameshajiimarisha vikosi hivyo vilirudi kwenda kuungana na wenzao huko mashariki.
Nataka niwaambie tuu majimbo yote ya mashariki kamwe Ukraine hawezi tena kuyakomboa ,hata wazungu wamepigwa na butwaaa kuchezewa akili na Putin
Ila kwa hitimisho sijapenda mbinu hii maana inagharama sana ,maisha ya RAIA wasio na hatia, uharibifu mkubwa wa miundombinu ,pia hata hasara kwa jeshi la urusi maana wengi wanaotumwaga kufanya coverage huwa ni askari wasio weled na mara nyingi hawapewi zana za kisasa, hivyo wengi hupoteza maisha ili kumpa moyo anayevamiwa akidhani anapata ushindi kumbe anaelekea shimon.
Wengi mkisikia mrusi ni mbabe wa vita huwa mnaona ni neno dogo ila Mrusi ni hatari sana ana mbinu za kushangaza na ambazo adui hawezi fikiria.
Sasa nije kwenye mbinu ya kuhakikisha wanyakwapua majimbo hayo,maana walielewa fika wakienda kichwakichwa wangeumbuka mno.
Kwanza kabisa walijigawa makundi matatu ,ambapo kundi la kwanza lilitangulia upande wa mji mkuu Kiev kama vile wanataka kuingia mjini,ila walikua wanazuga tuu ili kuvuruga mipango ya jeshi la Ukraine ,na kweli lilivurugika kweli maana Ukraine ilijikita kutumia nguvu nyingi kuzuia jeshi la Russian kuingia mji mkuu Kiev, huku wakisahau kuna kundi lilikua linazunguka Eastern na kujiimarisha huko
Kundi la pili lilijikita kama linataka kutokea upande wa kaskazin kupitia Belarus ila nao ilikua zuga tuu.
Kundi la tatu ndilo la kifo lilijikita majimbo ya mashariki likiwa na shehena ya silaha nyingi na kujiimarisha huko ,huku wenzao wakiendelea kuzuga ,mbinu hii inaitwa cover the main target
Wakati mataifa ya ulaya na dunia wakimzomea puttin kwamba kashindwa kutimiza lengo lake la kuingia Kiev ,yeye aliendelea kujiimarisha zaidi
Baada ya kuhakikisha ameshajiimarisha vikosi hivyo vilirudi kwenda kuungana na wenzao huko mashariki.
Nataka niwaambie tuu majimbo yote ya mashariki kamwe Ukraine hawezi tena kuyakomboa ,hata wazungu wamepigwa na butwaaa kuchezewa akili na Putin
Ila kwa hitimisho sijapenda mbinu hii maana inagharama sana ,maisha ya RAIA wasio na hatia, uharibifu mkubwa wa miundombinu ,pia hata hasara kwa jeshi la urusi maana wengi wanaotumwaga kufanya coverage huwa ni askari wasio weled na mara nyingi hawapewi zana za kisasa, hivyo wengi hupoteza maisha ili kumpa moyo anayevamiwa akidhani anapata ushindi kumbe anaelekea shimon.
Wengi mkisikia mrusi ni mbabe wa vita huwa mnaona ni neno dogo ila Mrusi ni hatari sana ana mbinu za kushangaza na ambazo adui hawezi fikiria.