Mbinu mpya wakwapuaji wa Benki

Mbinu mpya wakwapuaji wa Benki

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,992
Reaction score
12,036
Chukua tahadhari baada ya kuchukua pesa benki...
Dada mmoja Mkazi wa Msigani leo ameibiwa zaidi ya MILIONI MBILI akitokea Tawi la CRDB Mbezi Mwisho. Ilikuwa hv dada amechukua fedha ndani ya benki kufika kwenye Gari yake akamkuta MJAMZITO ameegemea gari akiomba msaada wa kuwahishwa Hospt Luguruni kwa Masista. Wakiwa njiani akamuuliza MJAMZITO huna vifaa? Akajibiwa kwamba mumewe atamletea Hospt, walipofika Kituo cha mafuta LUGURUNI ikatokea pkpk ambayo iliashiria kuwasimamisha ndipo Dada dereva akamuuliza MJAMZITO kama ndiye mumewe, wakati huo MJAMZITO alijitia amelaza kiti akajibu ndio, walimpakia yule baba akiwa na mfuko. Walipoingia njia ya VUMBI ndipo MJAMZITO akaomba gari isimame ili ATAPIKE, ndipo dereva akasimama, gari wakati MJAMZITO FEKI anajitia kutapika ndipo MUME FEKI akatoa KISU KIKUBWA akitaka FEDHA iliyotolewa benki na DADA Driver huku akitaja kiasi halisi ambacho kimetolewa benki. Dada wa watu hakuwa na jinsi akatoa fedha husika na mara zikatokea pkpk mbili MJAMZITO NA MUMEWE waka panda na kuondoka. Maskini yule DADA kwa mshtuko AKAHARIBIKIWA hadi kushindwa kuendesha gari. Chukua tahadhari ukiwa BENKI usiamini mtu yeyote utokapo benki. Imetokea jana 12/03/2015. Nawasilisha kama nilivyotumiwa
 
Nitaabu huku wengine wamelizwa kwenye airtelmoney tena mwakala, jamani wezi hawatakuja kuisha wanabadiri mbinu
 
Mbinu nzuri 7bu wanakuachia roho yako
Ni a very complex technique imetumika ili kuhakikisha hafi mtu. wengine hawana muda wa huu upuuzi.., unakula risasi ya kichwa wanaondoka na mzigo. Big up kwa kutotoa roho ya huyo dada. ila bado mwenye uwezo atawaadhibu kwa mlichofanya.
 
enh yaa rabi tunusuru na njama hizi kila kukicha
 
Bank Tellers wana husika, Serikali ilazimishe wavae vitambulisho vyenye majina yao ili mtu akiibiwa kwa mtindo huo aweze kumtambua mhusika na mawasiliano yake yaweze kufuatiliwa
 
unataka kusema humo benki kuna mtu alimwamini na kumwambia "nimekuja kuchukua milioni mbili, na pale nje nimekuja na noah"!!! hii story huenda ni ya uwongo au imeongezwa chumvi, mfanyakazi wa benki akiamua kucolaborate na wahalifu anafanya hivyo kwa pesa nyingi, siyo milioni mbili!!!!!! no wonder Ufoo alikosa msaada wa gari akaonewa imani na bodaboda sababu ya kutishana hivihivi. Muhim ni kuwa makini tu, wewe mtu ameshikwa na uchungu anakuja kusubiri gari imepark kama yake vile, hujiulizi kwa nini hajasimamisha zilizo barabarani tayari?!
 
Hii stori unaweza ukatengeneza movie nzuri sana . Mpelekee LULU KOMBA
 
Bank Tellers wana husika, Serikali ilazimishe wavae vitambulisho vyenye majina yao ili mtu akiibiwa kwa mtindo huo aweze kumtambua mhusika na mawasiliano yake yaweze kufuatiliwa

Teller ashirikiane na majambazi kwa ajili ya mgao wa laki mbili?!!! vitambulisho wanavyo, na madirisha yana namba inajulikana nani alikaa namba ngapi siku fulani.
 
unataka kusema humo benki kuna mtu alimwamini na kumwambia "nimekuja kuchukua milioni mbili, na pale nje nimekuja na noah"!!! hii story huenda ni ya uwongo au imeongezwa chumvi, mfanyakazi wa benki akiamua kucolaborate na wahalifu anafanya hivyo kwa pesa nyingi, siyo milioni mbili!!!!!! no wonder Ufoo alikosa msaada wa gari akaonewa imani na bodaboda sababu ya kutishana hivihivi. Muhim ni kuwa makini tu, wewe mtu ameshikwa na uchungu anakuja kusubiri gari imepark kattini hajasimamisha zilizo barabarani tayari?!

Mkuu nadhani wewe ndo ukikutana na wajanja utaibiwa hata soksi uliyovaa na ustambue.Hzo nı technique simpo kabsa.Wana mchongo na teller na wanawasiliana kwa namna nyngi au signs.Teller anaweza kumuuliza kwa sautı akishaona kinafaa kuibwa,"UNATOA SHS NGAPI?"Kuna mpambe jirani alıshamwona toka anaingia.Mtandao unaendelea,wanawasiliana na wenzao nje.
 
Mkuu nadhani wewe ndo ukikutana na wajanja utaibiwa hata soksi uliyovaa na ustambue.Hzo nı technique simpo kabsa.Wana mchongo na teller na wanawasiliana kwa namna nyngi au signs.Teller anaweza kumuuliza kwa sautı akishaona kinafaa kuibwa,"UNATOA SHS NGAPI?"Kuna mpambe jirani alıshamwona toka anaingia.Mtandao unaendelea,wanawasiliana na wenzao nje.

Bwahahahahahahah, kumbe nyie ndiyo mnaeneza uzushi fb?!! Benki ya wapi hiyo wanaulizaga "UNATOA SH NGAPI"? nimecheka kwa sauti..duh! Kila kitu umeandika kwenye slip kwa namba na maneno halafu teller anakuuliza kwa sauti?..hiyo itakuwa bank ya mpesa.
 
Hivi mpaka leo mnapanga foleni bank kuchukua hela pamoja na hizi simbanking zote?labda waniibie wakati naenda lipa ada za machalii zihitajizo hard copy payment receipt.
 
Yaani binadamu siku hizi watu haitakiwi kabisa kumwamini usiyemjua pole dada
 
Hivi mpaka leo mnapanga foleni bank kuchukua hela pamoja na hizi simbanking zote?labda waniibie wakati naenda lipa ada za machalii zihitajizo hard copy payment receipt.


we mwajiriwa huwezi kujua!
 
Bank Tellers wana husika, Serikali ilazimishe wavae vitambulisho vyenye majina yao ili mtu akiibiwa kwa mtindo huo aweze kumtambua mhusika na mawasiliano yake yaweze kufuatiliwa

hata kama asipo vaa kitambulisho ukirudi benki utampata,muhimu rudi uulizie jina lake anaitwa nani,baada ya hapo chukuwa hatua,ila kwa ushauri wangu ukiwa benki usimwamini mtu kuanzia ndani hadi nje ya benki,ukiweza ukiwa nje kabla hujaingia ndani tumia muda angalia hali ikoje pale nje-magari yaliyopaki,pikipiki,watu waliopi maeneo hayo na mienendo yao.....ukiingia ndani jaribu kuangalia watu waliomo na kazi wanazofanya kwa wakati huo,je kuna ambao wamekaa pembeni kwa muda mrefu na hawajishughulishi na chochote kwa muda mrefu? Ukitoka nje kama una usafiri tulia kwanza uangalie wale uliowatilia mashaka awali....,utakapo ondoka angalia kati ya magari /pikipiki zilizo kuwepo kuna inayokufuatilia?
 
Inawezekana hii hadithi ni ya uongo kwani scenario zinabadilika toka fb, Insta, Whatsapp most likely ya kutunga
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom