Mbeya: Boniface Mwabukusi na Mdude Nyagali waachiwa kwa dhamana

Kama tulivyosema tangu awali , Shetani hajawahi kumshinda Mungu , hatimaye watuhumiwa wote wako huru

Masharti ya Dhamana kwa Mdude na Mwabukusi haya hapa .

View attachment 2720869

====

UPDATES; 1800HRS

=====

Mdude Nyagali na Boniface Mwabukusi waachiwa kwa dhamana.

Watuhumiwa wa kesi ya uhaini wakili Boniface Mwakubukusi na Mdude Nyagali waliokuwa wakishiliwa na jeshi la polisi Mkoa wa Mbeya wameachiwa huru wakibadilishiwa mashtakana na kuwa kesi ya uchochezi.

Wakili Mwambukusi na Mdude wamechiwa majira ya saa 11:30 jioni huku wakiwashukuru watanzania pamoja na mashirika mbalimbali huku wakieleza kuwa watatoa msimamo wao baada ya kukutana na Balozi Dk Wilbroad Slaa.

Wakili Philip Mwakilima anayewatetea Wakili Boniface Mwambukusi na Mdude Nyagali amesema kutoka na dhamana hiyo kosa la uhaini halipo tena hivyo wateja wake wamedhamiwa kwa kosa la uchochezi

Mwabukusi hivi karibuni aliwawakilisha wadai wanne katika kesi iliyofunguliwa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya kupinga mkataba wa ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai (IGA), akiwa kiongozi wa jopo la mawakili.

Kesi hiyo ya kikatiba namba 5 ya mwaka 2023 ilifunguliwa na Alphonce Lusako, Emmanuel Chengula, Raphael Ngonde na Frank Nyalus dhidi ya Serikali.

Agosti 10, mwaka huu Mahakama ilitoa hukumu ya kuitupa kesi hiyo ikisema haina mashiko.

Baada ya kesi kutupiliwa mbali, Jeshi la Polisi lilionya wanaoandaa maandamano ya nchi nzima ili kuiangusha Serikali kabla ya mwaka 2025, likisema waandaaji wanayahusisha na kushawishi jumuiya ya Watanzania kuwaunga mkono katika hoja kuhusu Bandari.

Bila ya kutaja majina au kikundi cha watu, Mkuu wa jeshi hilo (IGP), Camillius Wambura akizungumza na waandishi wa habari alisema kuna taarifa zinasambaa katika mitandao ya kijamii inayohusu maandamano hayo.

Hata hivyo, baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya kutoa hukumu katika kesi ya IGA, wakili Mwabukusi alitangaza uwepo wa maandamano.

Polisi: Tumemkamata Mwabukusi, Mdude kwa mahojiano

Jeshi la Polisi nchini lilithibitisha kuwakamata Wakili Boniface Mwabukusi na Mpaluka Said Nyagali maarufu kama Mdude kwa tuhuma za kutoa maneno ya uchochezi.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, SACP -David Misime ilisema wawili hao wamekatwa kwa mahojiano ambayo yanaendelea.

“Jeshi la Polisi kama lilivyo eleza jana tarehe 11 Agosti 2023 linawafuatilia ili liwakamate watuhumiwa walioandaa na kutoa maneno ya uchochezi, kazi hiyo inaendelea kufanyika kwa mujibu wa sheria.



Mwabukusi alikuwa mmoja wa wanasheria waliofungua kesi ya kupinga mkataba uliofumgwa kati ya serikali na Dubai.


Kukamatwa kwa Mwabukusi kulikuja muda mfupi baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi kuutangazia ulimwengu, kwamba “kuna njama za kumuangusha Rais wa Jamhuri, Dk. Samia Suluhu Hassan.
Hii kesi inanifundisha kitu kimoja kikubwa sana kwangu! " Sio kila jambo linatakiwa kuwa wazi kwa wote" Kinachotusumbua nimeona ni uwazi na nia njema ya Serikali yetu ya Awamu ya Sita, huko nyuma mikataba yote ilikua kimya kimya na mambo yalikuwa shwari kabisa!
 
Bado najiuliza ikiwa baraza la maaskofu Tanzania limeona umuhmu wa kusimama upande wa wananchi waliowengi na kuupinga mkataba mbovu hadhalani, je bunge letu wao kule wanamuakirisha nani!!?

Na wapo kwa masilahi yanani? Je nikweli wabunge wetu katika hili dubwana la bandari waliamua watutenge tuishi kama yatima!!?

Binafs nawapongeza Baraza la maaskofu hakika mmewatendea haki Watanganyika
 
Jeshi la Polisi linapaswa kupata ushahidi halafu kumkamata mtu. Tumerithi sheria za Jeshi kutoka Uingereza
Mfalme wa Uingereza nyakati za kale alitumia madaraka vibaya ndipo ikatengenezwa kitu inaitwa Magna Carta

Magna Carta ni sheria inayosema hivi
1. Hakuna mtu aliye juu ya sheria za nchi
2. Mtu afahamishwe kwanini anakamatwa na kwa ushahidi upi
3. Kila mtu ana haki ya kupata ushauri wa sheria
4. kaeleza haki za watu , na infact hapa ndipo ulipoanza mwanzo wa haki za Wanawake

Jeshi letu linafanya mambo kwa kutumia 'RAMLI' , kwamba Mwabukusi , Dr Slaa na Mdude wanatabiriwa kufanya UHANI. Halafu Jeshi linawakamata kwa kutumai 'Ramli', kisha linachukua simu zao na kwenda kuwapekua kutafuta ushahidi.
Inaposhindikana kupata ushahidi ikiwemo kudukua Whatsapp ndipo jeshi linabadili utabiri na kuwa uchochezi.

Hata kesi ya uchochezi watashindwa maana Dr Slaa akiongea walikuwepo , Mwabaukusi ni Mwanasheria anajua anaongea nini , Mdude ka 'graduate' huko magereza humbabaishi kwa sheria.

Ukitazama mtirirko mzima lazima upate shaka na uongozi wa Jeshi letu ikiwa wanajua madhara ya wanachokifanya

Baada ya kuichafua nchi kwa Tuhuma za UHAINI kama ilivyokuwa UGAIDI wa Mbowe, sasa wanatafuta pa kutokea

Kwa hili, tumshauri kwa dhati kabisa IGP Wambura, hujamtendea Haki Rais na Serikali yake. Kama ulipewa maagizo kutoka juu, bado hukutumia weledi wa Taaluma yako kufikia hitimisho.

Mheshimiwa IGP, huwezi kukubali kusikia Daktari amepewa maagizo kutoka juu ya kung'oa kende za mgonjwa na akafanya hivyo. Taaluma maana yake matumizi ya mafunzo na tathmini!

IGP Wambura, Jitathmini na itendee nchi haki. JITATHMINI Tafadhali ili umpe Mh Rais second Chance, bado tuna imani naye akipata usaidizi mzuri.

JokaKuu
 
Jeshi la Polisi linapaswa kupata ushahidi halafu kumkamata mtu. Tumerithi sheria za Jeshi kutoka Uingereza
Mfalme wa Uingereza nyakati za kale alitumia madaraka vibaya ndipo ikatengenezwa kitu inaitwa Magna Carta

Magna Carta ni sheria inayosema hivi
1. Hakuna mtu aliye juu ya sheria za nchi
2. Mtu afahamishwe kwanini anakamatwa na kwa ushahidi upi
3. Kila mtu ana haki ya kupata ushauri wa sheria
4. kaeleza haki za watu , na infact hapa ndipo ulipoanza mwanzo wa haki za Wanawake

Jeshi letu linafanya mambo kwa kutumia 'RAMLI' , kwamba Mwabukusi , Dr Slaa na Mdude wanatabiriwa kufanya UHANI. Halafu Jeshi linawakamata kwa kutumai 'Ramli', kisha linachukua simu zao na kwenda kuwapekua kutafuta ushahidi.
Inaposhindikana kupata ushahidi ikiwemo kudukua Whatsapp ndipo jeshi linabadili utabiri na kuwa uchochezi.

Hata kesi ya uchochezi watashindwa maana Dr Slaa akiongea walikuwepo , Mwabaukusi ni Mwanasheria anajua anaongea nini , Mdude ka 'graduate' huko magereza humbabaishi kwa sheria.

Ukitazama mtirirko mzima lazima upate shaka na uongozi wa Jeshi letu ikiwa wanajua madhara ya wanachokifanya

Baada ya kuichafua nchi kwa Tuhuma za UHAINI kama ilivyokuwa UGAIDI wa Mbowe, sasa wanatafuta pa kutokea

Kwa hili, tumshauri kwa dhati kabisa IGP Wambura, hujamtendea Haki Rais na Serikali yake. Kama ulipewa maagizo kutoka juu, bado hukutumia weledi wa Taaluma yako kufikia hitimisho.

Mheshimiwa IGP, huwezi kukubali kusikia Daktari amepewa maagizo kutoka juu ya kung'oa kende za mgonjwa na akafanya hivyo. Taaluma maana yake matumizi ya mafunzo na tathmini!

IGP Wambura, Jitathmini na itendee nchi haki. JITATHMINI Tafadhali ili umpe Mh Rais second Chance, bado tuna imani naye akipata usaidizi mzuri.

JokaKuu
swadakta
 
Wameonewa huruma sasa wawe makini next time ingawa mashtaka ya uchochezi bado yapo pale pale
Kwa jeshi hili la polisi kwa kushirikiana na majizi ya kura, sishangai wawe na kesi. Jana naona baada ya kuona huo uzushi wenu wa uhaini umebuma, mkaja na Hadaa eti mawakili wa kina Dr. Slaa wamuangukia Rais aingilie kati, ili wakiachiwa leo mjifanye rais aliingilia kati baada ya kuombwa.

Hakuna mtu yoyote anajitambua atawaangukia nyie majizi, labda hao wachumia tumbo wenzenu wa ccm wanaoona vyeo ni kitu cha maana.
 
Kwa jeshi hili la polisi kwa kushirikiana na majizi ya kura, sishangai wawe na kesi. Jana naona baada ya kuona huo uzushi wenu wa uhaini umebuma, mkaja na Hadaa eti mawakili wa kina Dr. Slaa wamuangukia Rais aingilie kati, ili wakiachiwa leo mjifanye rais aliingilia kati baada ya kuombwa.

Hakuna mtu yoyote anajitambua atawaangukia nyie majizi, labda hao wachumia tumbo wenzenu wa ccm wanaoona vyeo ni kitu cha maana.
Ni wale wale waliokuwa wanasema 'acheni vyombo vya dola' vifanye kazi yake!

Kwa hili, ukweli usemwe tu. IGP Wambura abebe dhamana yote ya aibu .
IGP anatangazia dunia kesi ya '' uchochezi' inayoweza kuendeshwa na sagenti wa kituo cha Mikumi!!

IGP Wambura, itendee haki serikali. Jitathmini kama bado unaaminika na unaaminiwa na viongozi na Umma.
Jitathmini kwasababu anguko hili si la kujikung'uta na kuamka, hili linahitaji kutolewa nje ya ukumbi.

Please IGP, fanya jambo la muhimu na la lazima, fikiria umma unakutaza vipi leo?
 
Ni wale wale waliokuwa wanasema 'acheni vyombo vya dola' vifanye kazi yake!

Kwa hili, ukweli usemwe tu. IGP Wambura abebe dhamana yote ya aibu .
IGP anatangazia dunia kesi ya '' uchochezi' inayoweza kuendeshwa na sagenti wa kituo cha Mikumi!!

IGP Wambura, itendee haki serikali. Jitathmini kama bado unaaminika na unaaminiwa na viongozi na Umma.
Jitathmini kwasababu anguko hili si la kujikung'uta na kuamka, hili linahitaji kutolewa nje ya ukumbi.

Please IGP, fanya jambo la muhimu na la lazima, fikiria umma unakutaza vipi leo?
Mkuu kwa bahati mbaya kwa sasa watendaji wa umma hawawajibiki kwa umma, bali kwa viongozi wanaowateua, na kwakuwa wanaowateau sio watu waadilifu, wote wanakuwa sio waadilifu, hivyo wanabaki wakilindana. Usitegemee IGP ajiuzulu aache ulaji, wakati anayofanya yana baraka ya aliyemteua.

Kwa sasa hivi sheria zote za nchi zinatekelezwa kwa utashi wa kiongozi aliyeko madarakani. Hakuna sheria yoyote itakuwa na nguvu nje ya utashi wa rais. Amri kutoka juu ndio zimegeuka kuwa na nguvu kuliko sheria na katiba.
 
Mkuu kwa bahati mbaya kwa sasa watendaji wa umma hawawajibiki kwa umma, bali kwa viongozi wanaowateua, na kwakuwa wanaowateau sio watu waadilifu, wote wanakuwa sio waadilifu, hivyo wanabaki wakilindana. Usitegemee IGP ajiuzulu aache ulaji, wakati anayofanya yana baraka ya aliyemteua.

Kwa sasa hivi sheria zote za nchi zinatekelezwa kwa utashi wa kiongozi aliyeko madarakani. Hakuna sheria yoyote itakuwa na nguvu nje ya utashi wa rais. Amri kutoka juu ndio zimegeuka kuwa na nguvu kuliko sheria na katiba.
Ni kweli unachoksema lakini tunamkumbusha IGP kwamba Umma unamwangalia kwa jicho tofauti, Umma hauna imani na kauli zake tena, na kwamba amedhalilika sana. Ameitia serikali aibu na kumweka Mh Rais mahali pagumu

Kama watalindana hilo haliondoi ukweli kwamba IGP alitakiwa ajitathmini maana kuitia nchi katika sintofahamu ya namna hii si kwamba inavunja heshima ya Jeshi la Polisi kama chombo cha umma, lakini pia anamlundikia Mh Rais matatizo yasiyo na sababu. IGP anakuwa 'distraction' badala ya kusaidia nchi.

Ndiyo maana tunasisitiza kuwa ajitahmini, hata kama atabaki ofisini ajiulize anaposimama mbele ya Umma , huo umma unamwangaliaje? Je, ataweza kutofautisha kelele za kushangiliwa au kuzomewa?
 
Ni kweli unachoksema lakini tunamkumbusha IGP kwamba Umma unamwangalia kwa jicho tofauti, Umma hauna imani na kauli zake tena, na kwamba amedhalilika sana. Ameitia serikali aibu na kumweka Mh Rais mahali pagumu

Kama watalindana hilo haliondoi ukweli kwamba IGP alitakiwa ajitathmini maana kuitia nchi katika sintofahamu ya namna hii si kwamba inavunja heshima ya Jeshi la Polisi kama chombo cha umma, lakini pia anamlundikia Mh Rais matatizo yasiyo na sababu. IGP anakuwa 'distraction' badala ya kusaidia nchi.

Ndiyo maana tunasisitiza kuwa ajitahmini, hata kama atabaki ofisini ajiulize anaposimama mbele ya Umma , huo umma unamwangaliaje? Je, ataweza kutofautisha kelele za kushangiliwa au kuzomewa?
Mkuu kwa bahati mbaya hakuna anayejali umma unamtazamaje, watu wanajali zaidi vyeo maana ndio vinawapa ulaji. Yaani kwa kiingereza wanasema he has a family to feed, not a Society to impress.
 
hi
Kama tulivyosema tangu awali , Shetani hajawahi kumshinda Mungu , hatimaye watuhumiwa wote wako huru

Masharti ya Dhamana kwa Mdude na Mwabukusi haya hapa .

View attachment 2720869

====

UPDATES; 1800HRS

=====

Mdude Nyagali na Boniface Mwabukusi waachiwa kwa dhamana.

Watuhumiwa wa kesi ya uhaini wakili Boniface Mwakubukusi na Mdude Nyagali waliokuwa wakishiliwa na jeshi la polisi Mkoa wa Mbeya wameachiwa huru wakibadilishiwa mashtakana na kuwa kesi ya uchochezi.

Wakili Mwambukusi na Mdude wamechiwa majira ya saa 11:30 jioni huku wakiwashukuru watanzania pamoja na mashirika mbalimbali huku wakieleza kuwa watatoa msimamo wao baada ya kukutana na Balozi Dk Wilbroad Slaa.

Wakili Philip Mwakilima anayewatetea Wakili Boniface Mwambukusi na Mdude Nyagali amesema kutoka na dhamana hiyo kosa la uhaini halipo tena hivyo wateja wake wamedhamiwa kwa kosa la uchochezi

Mwabukusi hivi karibuni aliwawakilisha wadai wanne katika kesi iliyofunguliwa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya kupinga mkataba wa ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai (IGA), akiwa kiongozi wa jopo la mawakili.

Kesi hiyo ya kikatiba namba 5 ya mwaka 2023 ilifunguliwa na Alphonce Lusako, Emmanuel Chengula, Raphael Ngonde na Frank Nyalus dhidi ya Serikali.

Agosti 10, mwaka huu Mahakama ilitoa hukumu ya kuitupa kesi hiyo ikisema haina mashiko.

Baada ya kesi kutupiliwa mbali, Jeshi la Polisi lilionya wanaoandaa maandamano ya nchi nzima ili kuiangusha Serikali kabla ya mwaka 2025, likisema waandaaji wanayahusisha na kushawishi jumuiya ya Watanzania kuwaunga mkono katika hoja kuhusu Bandari.

Bila ya kutaja majina au kikundi cha watu, Mkuu wa jeshi hilo (IGP), Camillius Wambura akizungumza na waandishi wa habari alisema kuna taarifa zinasambaa katika mitandao ya kijamii inayohusu maandamano hayo.

Hata hivyo, baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya kutoa hukumu katika kesi ya IGA, wakili Mwabukusi alitangaza uwepo wa maandamano.

Polisi: Tumemkamata Mwabukusi, Mdude kwa mahojiano

Jeshi la Polisi nchini lilithibitisha kuwakamata Wakili Boniface Mwabukusi na Mpaluka Said Nyagali maarufu kama Mdude kwa tuhuma za kutoa maneno ya uchochezi.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, SACP -David Misime ilisema wawili hao wamekatwa kwa mahojiano ambayo yanaendelea.

“Jeshi la Polisi kama lilivyo eleza jana tarehe 11 Agosti 2023 linawafuatilia ili liwakamate watuhumiwa walioandaa na kutoa maneno ya uchochezi, kazi hiyo inaendelea kufanyika kwa mujibu wa sheria.



Mwabukusi alikuwa mmoja wa wanasheria waliofungua kesi ya kupinga mkataba uliofumgwa kati ya serikali na Dubai.


Kukamatwa kwa Mwabukusi kulikuja muda mfupi baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi kuutangazia ulimwengu, kwamba “kuna njama za kumuangusha Rais wa Jamhuri, Dk. Samia Suluhu Hassan.
yo ni huruma tu ya rais na watulize matako yao hayo, umesahau wakili wao alivyokuwa anampigia magoti rais awaonee huruma maana Mwabukusi ana mishono na Slaa ni mzee. Rais wetu ana huruma na mcha Mungu wa kweli amewasikia sasa kuna lipi la ajabu. Mpongeze rais kwa utu alionao, watulie wawe raia wema. Ukweli tumeusikia wa kauli walizikuwa wanatoa hadharani, naamini hatarudia kutoa kauli za ajabu km zile za kugawa nchi na kuchochea chuki
 
hi

yo ni huruma tu ya rais na watulize matako yao hayo, umesahau wakili wao alivyokuwa anampigia magoti rais awaonee huruma maana Mwabukusi ana mishono na Slaa ni mzee. Rais wetu ana huruma na mcha Mungu wa kweli amewasikia sasa kuna lipi la ajabu. Mpongeze rais kwa utu alionao, watulie wawe raia wema. Ukweli tumeusikia wa kauli walizikuwa wanatoa hadharani, naamini hatarudia kutoa kauli za ajabu km zile za kugawa nchi na kuchochea chuki
hio huruma na ucha Mungu hakua nao wakati anawakamata 😅 halafu tangu lini wahaini wakakamatwa na polisi kina sajenti 😂 hayo ni mambo ya tiss eti mtu ambae mwisho wa silaha yake ni Ak47 anaenda daka wahaini 😅 watoto wa ssh wanasema ni huruma.Tangu lini mtuhumiwa akaonewq huruma kisa ya umri au ugonjwa acheni janja janja bhna hili limewachemsha mattercore 😂 na kwanza shughuli ndo imeanza.
 
Hembu na tuwasikie tena wakizungumzia waliyokuwa wakiyazungumza, hai Shughuli yao imeisha, waliyoona na kuyajua wakiwa huko ndani hawatakaa wawe na hamu tena ya maandamano
 
Back
Top Bottom