Mbele ya Urusi, Marekani lazima ale kona!

Mbele ya Urusi, Marekani lazima ale kona!

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,910
Reaction score
18,558
Nina uhakika SAA hii Trump atakuwa anajutia mkwara wake wa kuitishia urusi kuwa ijiandae maana ataishambulia Syria kwa makombora mazuri, mapya na janja!! (nice, new and smart)). Saa hii anajiuliza nisiposhambulia kama nilivyoahidi dunia yote wataniona mwoga! na nikishambulia maana yake nitegemee urusi kujibu mapigo kwa nguvu zote kama walivyoonya!!
Kitakachotokea ni marekani kutafuta upenyo wa kula kona kistaarabu kwa kuja na ngonjera hii: "Tumethibitisha kuwa hakuna silaha za kemikali alizotumia Syria kwa hiyo ule mpango wa kuishambulia tumeusitisha". Kwa namna hiyo atakuwa amekula kona kiaina!!!
Mshirika wake namba moja uingereza keshaonyesha dalili za kuingia mitini tayari na amesema itabidi marekani iwe na uthibitisho kwanza!!
Timu trump jiandaeni kisaikologia kumwona kinara wenu akila kona!! Kwanza alisema masaa 48 na yameisha!! Mdogo wake ufaransa akasema masaa 72 watakuwa wameshambulia nayo yanaishia!!! Timu trump jiandaeni kwa fedheha!!! Huwezi kumtishia nyau Putin!!
 
Kukaa kimya nako huwa ni kuzuri sana, trump anapenda sana Taarabu
 
Habari za asubuhi ndugu na marafiki, nadhabu mko njema na mungu anazidi kuwasaidia.

Kwa kweli mimi(nkobhe255) nilikuwa bonge la shabiki kwa udharimu unaofanywa na Marekani kwa baadhi ya mataifa madogo duniani. Marekani alijulikana kama mbabe wa dunia ambaye alikuwa na mamlaka ya kufanya chochote kile na asifanywe chochote kile na yeyote yule including UN. Lakini ubabe wa Marekani kimataifa umefikia mwisho siku hizi za karibuni. Nitatumia mifano ifuatayo:

(1)Mgogoro na N. Korea. Kila mtu alifuatilia juu ya sakata lililotishia kuzuka kwa vita kati ya USA na N. Korea, ilifikia kipindi USA wakapeleka kila aina ya Silaha katika mipaka ya N. Korea. Hapa niliamini huo utakuwa ndo mwisho wa N. Korea. Lakini kila mtu alijionea jinsi USA alipoamua kuyarudisha majeshi yake nyuma baada ya kupima urefu wa maji. Hapa niliumia na nilitumia zaidi ya siku 2 bila kula wala kunywa, mpaka watu wakanishangaa.

(2)Mgogoro wa Ukraine. Kabla Urusi haijainyakua CRIMEA ambalo ni jimbo la UKRAINE lililopo mpakani na Urusi, tuliona jinsi Marekani alivyotishia kusambaratisha utawala wa CREMRINE, Mpaka ikafikia hatua bunge la CONGRESS la Marekani kupitisha mswaada wa kupeleka silaha nzito kule Ukraine, lakini kila mtu anajua kilichotokea, mpaka sasa jimbo hilo la Crimea lilishanyakuliwa na Urusi.

(3)Mgogoro wa Syria. Yaani hapa ndo nimechanganyikiwa kabisa, hii ni baada ya Marekani kuahidi majibu kwa serikali aliyoiita dhalimu duniani ndani ya saa 24 to 48, halafu baadae akatweet eti baada ya saa 72.Chakushangaza ni baada ya haya masaa 72 kuyoyoma ndipo washirika wa Marekani walipoona mambo ni mazito wote wakakacha. Mfano, mpaka mda huu, UK, France na Germany wamegoma kufanya shambulizi la pamoja huko Syria wakishirikiana na Marekani. Kwakweli nimechanganyikiwa kinoma, yaani USA ndo anatufanyia sisi TEAM mawigi hivi? Nimechoka kuumia aisee, sasa lasmi najiunga na TEAM mbilikimo(Putin). Huyu USA amezidiwa na Israel, Israel kamuanzishia ili kumuonyesha njia ila cha kushangaza USA kabweka weeeee mwishowe akarudi nyuma, Pumbavu TEAM Mawigi na HONGERA TEAM Mbilikimo(Putin) kwa ushindi.

MY TAKE.

Ukweli ni kwamba, japo Marekani wana Silaha nyingi na nzito lakini ni waoga kupigana vita, ndo maana wanashindwa kuthubutu chochote, Trump kashindwa kuamrisha tu? Mbona Putin kashayapa makeshi yake yote ruhusa na kujibu mapigo? Kwanini Mawigi kashindwa?

Huu ubabe wa Marekani kila mwaka unaenda unapungua, kijeshi na kiuchumi. Baada ya hili, washirika wengi wa Marekani wataanza kukimbilia Urusi ili kujihakikishia usalama wao baada ya kushindwa kuona msaada wa Marekani. Pia mataifa mengi yaanza kukimbilia China kiuchumi ili kulinda masoko yake ya fedha duniani hapo baadae.

Bye bye Team Mawigi, nadhani teaam Mbilikimo mtanikaribisha.
 
Nilicho ona mm sio kwqmba marekani wanashindwa ila hawataki kufanya kama yaliyo fanywa kipindi cha hiroshima na nagasaki...

OVA..

Hama salama mkuu....
 
Nilicho ona mm sio kwqmba marekani wanashindwa ila hawataki kufanya kama yaliyo fanywa kipindi cha hiroshima na nagasaki...

OVA..

Hama salama mkuu....
Sio hawataki Bali wanaogopa!! Huwezi ukatumia Bomu LA nyuklia halafu ukabaki salama!! Kabla halijatua la kwako unajibiwa na mengine kumi dhidi yako!!
 
Habari za asubuhi ndugu na marafiki, nadhabu mko njema na mungu anazidi kuwasaidia.

Kwa kweli mimi(nkobhe255) nilikuwa bonge la shabiki kwa udharimu unaofanywa na Marekani kwa baadhi ya mataifa madogo duniani. Marekani alijulikana kama mbabe wa dunia ambaye alikuwa na mamlaka ya kufanya chochote kile na asifanywe chochote kile na yeyote yule including UN. Lakini ubabe wa Marekani kimataifa umefikia mwisho siku hizi za karibuni. Nitatumia mifano ifuatayo:

(1)Mgogoro na N. Korea. Kila mtu alifuatilia juu ya sakata lililotishia kuzuka kwa vita kati ya USA na N. Korea, ilifikia kipindi USA wakapeleka kila aina ya Silaha katika mipaka ya N. Korea. Hapa niliamini huo utakuwa ndo mwisho wa N. Korea. Lakini kila mtu alijionea jinsi USA alipoamua kuyarudisha majeshi yake nyuma baada ya kupima urefu wa maji. Hapa niliumia na nilitumia zaidi ya siku 2 bila kula wala kunywa, mpaka watu wakanishangaa.

(2)Mgogoro wa Ukraine. Kabla Urusi haijainyakua CRIMEA ambalo ni jimbo la UKRAINE lililopo mpakani na Urusi, tuliona jinsi Marekani alivyotishia kusambaratisha utawala wa CREMRINE, Mpaka ikafikia hatua bunge la CONGRESS la Marekani kupitisha mswaada wa kupeleka silaha nzito kule Ukraine, lakini kila mtu anajua kilichotokea, mpaka sasa jimbo hilo la Crimea lilishanyakuliwa na Urusi.

(3)Mgogoro wa Syria. Yaani hapa ndo nimechanganyikiwa kabisa, hii ni baada ya Marekani kuahidi majibu kwa serikali aliyoiita dhalimu duniani ndani ya saa 24 to 48, halafu baadae akatweet eti baada ya saa 72.Chakushangaza ni baada ya haya masaa 72 kuyoyoma ndipo washirika wa Marekani walipoona mambo ni mazito wote wakakacha. Mfano, mpaka mda huu, UK, France na Germany wamegoma kufanya shambulizi la pamoja huko Syria wakishirikiana na Marekani. Kwakweli nimechanganyikiwa kinoma, yaani USA ndo anatufanyia sisi TEAM mawigi hivi? Nimechoka kuumia aisee, sasa lasmi najiunga na TEAM mbilikimo(Putin). Huyu USA amezidiwa na Israel, Israel kamuanzishia ili kumuonyesha njia ila cha kushangaza USA kabweka weeeee mwishowe akarudi nyuma, Pumbavu TEAM Mawigi na HONGERA TEAM Mbilikimo(Putin) kwa ushindi.

MY TAKE.

Ukweli ni kwamba, japo Marekani wana Silaha nyingi na nzito lakini ni waoga kupigana vita, ndo maana wanashindwa kuthubutu chochote, Trump kashindwa kuamrisha tu? Mbona Putin kashayapa makeshi yake yote ruhusa na kujibu mapigo? Kwanini Mawigi kashindwa?

Huu ubabe wa Marekani kila mwaka unaenda unapungua, kijeshi na kiuchumi. Baada ya hili, washirika wengi wa Marekani wataanza kukimbilia Urusi ili kujihakikishia usalama wao baada ya kushindwa kuona msaada wa Marekani. Pia mataifa mengi yaanza kukimbilia China kiuchumi ili kulinda masoko yake ya fedha duniani hapo baadae.

Bye bye Team Mawigi, nadhani teaam Mbilikimo mtanikaribisha.

Nashindwa kuelewa umewaza nini ndugu, hivi kama muhanga(Syria) ingekua ndio nchi yako ungethubutu kuandika hivi, unaona ni jambo la mchezo kwa vile ww haikuathiri. Kumbuka kuna watu kule km ww wenye malengo km ya kwako wanaopenda kuishi kwa amani km unavyoishi wewe. Haikusadii chochote kwa Marekani ama Urusi akiwa mbabe kwa kuvuruga maisha ya wengine sisi sote ni Binadamu. Tafakari.
 
Back
Top Bottom