Mbele na nyuma wapi tamu?

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,579
Reaction score
161,431
Tupo kwny mapumziko ya lunch tunabishana, eti mguu wa mbele na wa nyuma wa mbuzi, upi una nyama tamu?
 
nyuma kwa sababu huko kuna paja.
 
Hahaahahaaaaaa kizazi cha nyoka hiki........watu mnapenda nyuma sanaaaaaa mie naona mguu wa mbele ndio mtamu hauna mafuta sana!!! Shurti uuweka huo mguu wa mbele kwenye mapapai mabichi ili nyama iwe laini.....
 
Hakuna mguu wa mbele, inaitwa mikono hiyo kaka, labda uulize mguu wa kulia na wa kushoto upi mtamu au mguu na mkono wa mbuzi upi mtamu
 
mguu wa nyuma wa mbuzi ni mifupi lkn ndo tamu kwani ndio iko kwenye eneo la jembe na kiuno na katika nyama tamu kuliko zote ni kiuno ikifuatiwa na salala ila nyama nyingi ni jembe. miguu ya mbele ni mirefu ila haina nyama tamu manake imekaa na misuli isiyokua na mafuta kama ya nyuma. na hata location yake ni mbaya yaani karibu na shingo na mbavu.
 
Acheni kuleta mada za kitoto hapa ndani. Mnatupotezea muda. Kama huna cha kuandika, tulia, nyamaza kimya kabisa. Soma michango ya wenzako iliyoenda shule. Nasema hii tabia ikome mara moja. Toeni mada zenye tija na kuelemisha taifa letu. Ni hayo tu.
 

Lohh mi nilikuwa siyajui yote haya
 
Si mnunuwe, yote mle na jibu mtalipata hapo hapo? mijitu mingine hovyo kabisa.

Great thinker at work. Congratulations for thinkin' out the box.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Acheni kuleta mada za kitoto hapa ndani. Mnatupotezea muda. Kama huna cha kuandika, tulia, nyamaza kimya kabisa. Soma michango ya wenzako iliyoenda shule. Nasema hii tabia ikome mara moja. Toeni mada zenye tija na kuelemisha taifa letu. Ni hayo tu.

Tupo pamoja mkuu. Tatizo siku hizi hadi siye watoto wa uswazi tunaAccess ya internet ndo maana yanatokea yote haya. Kuna siku mtu atataka kuingia msalani halafu aanzishe mada yenye heading "NIKITAKA KUINGIA MSALANI NITANGULIZE MGUU WA KUUME AU WA KUSHOTO?".

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
miguu!! kwani inaotea wapi?

we kula uliowahi kula usije badilika bure mtu wa watu
 
Nyuma tamu sana pia nyama nyingi na lainiiiii, mbele kugumu
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…