Katika umoja huu wa UKAWA upande wa NCCR mpaka sasa ndio wamesikika hadharani kutoa maneno na kuonesha pingamizi kwa baadhi ya mambo katika Umoja huu.
Kwa mfano miezi iliyopita tumesikia matamshi toka kwa viongozi wachache na wajumbe wa chama chako.
Vile vile katika uchaguzi uliopita wa serikali za mitaa, wananchi wa Mtwara mjini walishuhudia CCM kushinda katika sehemu nyingi ambazo UKAWA hawakusimamisha mgombea mmoja. Ikumbukwe kwamba kwa Mtwara UKAWA walikubaliana kufanya hivyo. Hata hivyo, mwishoni NCCR iliamua kusimamisha wagombea kwa baadhi ya mitaa ambayo tayari walikubaliana kuachia chama kingine. Hivyo, ikapelekea CCM kushinda katika mitaa hiyo.
Jana Mbatia kama mwenyekiti ametoa kauli ile. Hapa sasa ndipo wananchi tutajiuliza, je, ndani ya UKAWA ni NCCR tu ndio wanakwazika na huu mchakato? Je, NCCR wana nia ya dhati na huu UKAWA? Je, NCCR ina uongozi dhaifu kushindwa kukabiliana na changamoto za huu umoja ndani ya chama chao? Je, CCM wamepata kichochoro cha kujaribu kuuvuruga huu umoja?
Bado NCCR mna muda wa kuangalia haya mambo kwa mapana kwa manufaa ya sisi WATANZANIA. Tumaini letu ni UKAWA.
Mh. Mbatia yaangalie haya kwa jicho lako la busara na karama za uongozi ulizopewa.
Kwa mfano miezi iliyopita tumesikia matamshi toka kwa viongozi wachache na wajumbe wa chama chako.
Vile vile katika uchaguzi uliopita wa serikali za mitaa, wananchi wa Mtwara mjini walishuhudia CCM kushinda katika sehemu nyingi ambazo UKAWA hawakusimamisha mgombea mmoja. Ikumbukwe kwamba kwa Mtwara UKAWA walikubaliana kufanya hivyo. Hata hivyo, mwishoni NCCR iliamua kusimamisha wagombea kwa baadhi ya mitaa ambayo tayari walikubaliana kuachia chama kingine. Hivyo, ikapelekea CCM kushinda katika mitaa hiyo.
Jana Mbatia kama mwenyekiti ametoa kauli ile. Hapa sasa ndipo wananchi tutajiuliza, je, ndani ya UKAWA ni NCCR tu ndio wanakwazika na huu mchakato? Je, NCCR wana nia ya dhati na huu UKAWA? Je, NCCR ina uongozi dhaifu kushindwa kukabiliana na changamoto za huu umoja ndani ya chama chao? Je, CCM wamepata kichochoro cha kujaribu kuuvuruga huu umoja?
Bado NCCR mna muda wa kuangalia haya mambo kwa mapana kwa manufaa ya sisi WATANZANIA. Tumaini letu ni UKAWA.
Mh. Mbatia yaangalie haya kwa jicho lako la busara na karama za uongozi ulizopewa.