Mambo yamezidi kuwa mabaya kwa Mbatia jimboni Vunjo baada Ya wana ukawa kuanza kupigana baina Ya Chadema Na Nccr Mageuzi Kwenye Mkutano wake uliofanyika stendi Ya njia panda, Himo.
Tukumbuke kwamba takribani mwezi mmoja uliopita madiwani wa Chadema wanaogombea kata za Vunjo waligoma kumfanyia kampeni mgombea wa ukawa James Mbatia kwa madai kwamba anaua Chadema Vunjo Na kwa sababu aligoma kuwaachia Chadema kata 8 jimboni humo. Nccr Mageuzi waliweka wagombea udiwani katika kata zote 16 za jimbo hilo bila kuwaachia Chadema ilihali wenyewe walimwachia Mbatia agombee ubunge.
Mbowe alivyokuja Vunjo siku chache zilizopita Alitoa maelekezo kwamba kufanyike kura za maoni katika kata zote za jimbo la Vunjo baina Ya wagombea udiwani wa Nccr Na Chadema Na atakayeshinda apeperushe bendera Ya chama hicho.
Kura hizo zilibidi zifanyike Leo katika kata zote, Mbatia akisimamia uchaguzi huo katika kata Ya Njia panda wana Chadema walimuona live akiipendelea Nccr kitu kilichowapandisha hasira wana Chadema Na kuanza vurugu. Mbatia kuona ngumi Zinarushwa alikimbilia Kwenye Gari lake huku bodigadi wake akitumia nguvu za ziada asidhurike. Vijana walimrushia Matusi Ya nguoni Mbatia Na kumwambia hawamtaki.
Majeruhi walipelekwa polisi ili wapate pf3 ili wakimbizwe hospitalini, lakini wakati wakiwa polisi wagombea ubunge Augustino Mrema wa TLP Na Shirima wa CCM walitinga hapo polisi. Viongozi wa Nccr Na wao walifika polisi Na kuanzisha vurugu Mpaka polisi wakalazimika kupiga risasi hewani kuwatawanya watu.
Pia, kata Ya kirua Vunjo kusini nako ngumi zilitawala baada Ya wana Chadema kuona Nccr wakipendelewa ili mgombea wao apite.
Nitaendelea kuwajuza kilichotekea Kwenye kata nyingine Pindi habari zitapozipata.
Mbatia Mwenyewe alienda kujificha Kwenye ofisi Za chama hicho Njia Panda huku Vijana wa Chadema wakiendelea kumporomeshea Matusi
Na kusema hawamtaki aonekane Vunjo.
Tukumbuke kwamba takribani mwezi mmoja uliopita madiwani wa Chadema wanaogombea kata za Vunjo waligoma kumfanyia kampeni mgombea wa ukawa James Mbatia kwa madai kwamba anaua Chadema Vunjo Na kwa sababu aligoma kuwaachia Chadema kata 8 jimboni humo. Nccr Mageuzi waliweka wagombea udiwani katika kata zote 16 za jimbo hilo bila kuwaachia Chadema ilihali wenyewe walimwachia Mbatia agombee ubunge.
Mbowe alivyokuja Vunjo siku chache zilizopita Alitoa maelekezo kwamba kufanyike kura za maoni katika kata zote za jimbo la Vunjo baina Ya wagombea udiwani wa Nccr Na Chadema Na atakayeshinda apeperushe bendera Ya chama hicho.
Kura hizo zilibidi zifanyike Leo katika kata zote, Mbatia akisimamia uchaguzi huo katika kata Ya Njia panda wana Chadema walimuona live akiipendelea Nccr kitu kilichowapandisha hasira wana Chadema Na kuanza vurugu. Mbatia kuona ngumi Zinarushwa alikimbilia Kwenye Gari lake huku bodigadi wake akitumia nguvu za ziada asidhurike. Vijana walimrushia Matusi Ya nguoni Mbatia Na kumwambia hawamtaki.
Majeruhi walipelekwa polisi ili wapate pf3 ili wakimbizwe hospitalini, lakini wakati wakiwa polisi wagombea ubunge Augustino Mrema wa TLP Na Shirima wa CCM walitinga hapo polisi. Viongozi wa Nccr Na wao walifika polisi Na kuanzisha vurugu Mpaka polisi wakalazimika kupiga risasi hewani kuwatawanya watu.
Pia, kata Ya kirua Vunjo kusini nako ngumi zilitawala baada Ya wana Chadema kuona Nccr wakipendelewa ili mgombea wao apite.
Nitaendelea kuwajuza kilichotekea Kwenye kata nyingine Pindi habari zitapozipata.
Mbatia Mwenyewe alienda kujificha Kwenye ofisi Za chama hicho Njia Panda huku Vijana wa Chadema wakiendelea kumporomeshea Matusi
Na kusema hawamtaki aonekane Vunjo.