Waridi
JF-Expert Member
- Mar 30, 2008
- 1,025
- 174
Na hivi ndivyo alivyonukuliwa na waandishi wengine
JAMES MBATIA AMPINGA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI PROFESA MUHONGO KUHUSU UVUNAJI WA GESI MTWARA [h=3]JAMES MBATIA AMPINGA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI PROFESA MUHONGO KUHUSU UVUNAJI WA GESI MTWARA[/h]
Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha NCCR-Mageuzi James Mbatia (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati akitoa taarifa kwa umma wa watanzania kuhusu mtazamo wake wa mgawo wa rasilimali za taifa na hali ya uchumi wa taifa la Tanzania. Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Ulinzi na Usalama wa Chama hicho Sebasitian Thomas. (Picha habari na www.mwaibale.blogspot.com)
Na Dotto Mwaibale
WENYEKITI wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, ameipinga kauli iliyotewa na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo ya kuwa wananchi wa mkoa wa Mtwara walishirikishwa katika mchakato wa uvunaji wa gesi badala yake ameitaka Serikali kutumia busara kuongea na wananchi hao ili kutatua mgogoro wa usafirishaji gesi hiyo asilia kutoka Mkoani Mtwara humo kwenda jijini Dar es salaam.
Mbatia alitoa kauli hiyo leo jijini Dar es salaam, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mgogoro huo ulioibuliwa hivi karibuni na wakazi wa Mkoa wa Mtwara waliopinga usafirishaji huo wa gesi kutoka mkoani mwao.
Mbatia ambaye pia ni Mbunge, alisema kwamba Serikali haipaswi kuwabeza wananchi hao kwa kitendo cha kuandamana, kwakuwa hiyo ilikuwa haki yao na wanastahili kupewa ufafanuzi wa rasilimali hiyo.
Alisema kuwa watanzania wa karne ya sasa, hawafai kuulizwa na watawala kuwa wanataka nini, bali ni swala la watawala na wananchi kukaa na kushirikiana kwa pamoja hili kufahamu namna ya kutatua changamoto mbalimbali na kutafuta ufumbuzi.
Alifafanua kuwa maandamano na madai ya wananchi wa Mtwara, yamedhihirisha ni kwa namna gani watu wamepata uamuko wa kutaka kutambua faida ya rasilimali walizo nazo.
Mbatia alisema kwamba kinachoteokea hivi sasa ni matokeo ya mfumo mbovu ambao haukuwa shirikishi, uliowafanya wananchi kutofahamu namna ya matumizi ya rasilimali katika nchi yao.
"Toka awali kulijengeka dhana ya kutokuwa na ushirikishaji wa wananchi katika maendeleo kupitia rasilimali, kinachotokea sasa wananchi wamepata ufahamu na wanapaswa kusikilizwa kwakuwa wana uelewa na wanahitaji kufahamu juu ya mali zao"alisema Mbatia
Aliongeza kuwa Serikali inapaswa kufurahia kuwa wananchi kwasasa wanajitambua, na kwamba wapo tayari kushirkiana na Serikali yao katika kuendeleza uchumi wa nchi hii.
JAMES MBATIA AMPINGA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI PROFESA MUHONGO KUHUSU UVUNAJI WA GESI MTWARA [h=3]JAMES MBATIA AMPINGA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI PROFESA MUHONGO KUHUSU UVUNAJI WA GESI MTWARA[/h]
Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha NCCR-Mageuzi James Mbatia (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati akitoa taarifa kwa umma wa watanzania kuhusu mtazamo wake wa mgawo wa rasilimali za taifa na hali ya uchumi wa taifa la Tanzania. Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Ulinzi na Usalama wa Chama hicho Sebasitian Thomas. (Picha habari na www.mwaibale.blogspot.com)
Na Dotto Mwaibale
WENYEKITI wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, ameipinga kauli iliyotewa na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo ya kuwa wananchi wa mkoa wa Mtwara walishirikishwa katika mchakato wa uvunaji wa gesi badala yake ameitaka Serikali kutumia busara kuongea na wananchi hao ili kutatua mgogoro wa usafirishaji gesi hiyo asilia kutoka Mkoani Mtwara humo kwenda jijini Dar es salaam.
Mbatia alitoa kauli hiyo leo jijini Dar es salaam, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mgogoro huo ulioibuliwa hivi karibuni na wakazi wa Mkoa wa Mtwara waliopinga usafirishaji huo wa gesi kutoka mkoani mwao.
Mbatia ambaye pia ni Mbunge, alisema kwamba Serikali haipaswi kuwabeza wananchi hao kwa kitendo cha kuandamana, kwakuwa hiyo ilikuwa haki yao na wanastahili kupewa ufafanuzi wa rasilimali hiyo.
Alisema kuwa watanzania wa karne ya sasa, hawafai kuulizwa na watawala kuwa wanataka nini, bali ni swala la watawala na wananchi kukaa na kushirikiana kwa pamoja hili kufahamu namna ya kutatua changamoto mbalimbali na kutafuta ufumbuzi.
Alifafanua kuwa maandamano na madai ya wananchi wa Mtwara, yamedhihirisha ni kwa namna gani watu wamepata uamuko wa kutaka kutambua faida ya rasilimali walizo nazo.
Mbatia alisema kwamba kinachoteokea hivi sasa ni matokeo ya mfumo mbovu ambao haukuwa shirikishi, uliowafanya wananchi kutofahamu namna ya matumizi ya rasilimali katika nchi yao.
"Toka awali kulijengeka dhana ya kutokuwa na ushirikishaji wa wananchi katika maendeleo kupitia rasilimali, kinachotokea sasa wananchi wamepata ufahamu na wanapaswa kusikilizwa kwakuwa wana uelewa na wanahitaji kufahamu juu ya mali zao"alisema Mbatia
Aliongeza kuwa Serikali inapaswa kufurahia kuwa wananchi kwasasa wanajitambua, na kwamba wapo tayari kushirkiana na Serikali yao katika kuendeleza uchumi wa nchi hii.
You might also like:


