April
Member
- Nov 14, 2011
- 35
- 21
Wanajamii,
Katika hali isiyo ya kawaida baada ya Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Bw.James Mbatia na wenzake kumaliza mazungumzo Ikulu hivi majuzi, habari za uchunguzi zinasema ya kuwa, mojawapo ya hoja ilikuwa ni kuiomba serikali isaidie kuhakikisha Mh. David Kafulila (Mb. Kigoma Kusini) anatenguliwa ubunge.
Chanzo kinaeleza kuwa, mwishoni mwa wiki jana James Mbatia ameandika barua ndefu kwa Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akimuomba aingilie kati suala hilo kuhakikisha Bunge linatengua tamko la awali la kuendelea kumtambua David Kafulila kama mbunge.
Barua hiyo iliyoandikwa Ofisi ya Waziri Mkuu na kupigwa chapuo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mh. William Lukuvi (kama ishara ya kuridhia pendekezo hilo la Mbatia), inaomba nguvu ya Waziri Mkuu itumike kubadili msimamo wa Bunge.
Pia imeelezwa kuwa, barua hiyo imelalamikia Ofisi ya Bunge kwa kumtambua Mh. David Kafulila kama mwakilishi wa wabunge wa NCCR kwenye msiba wa Marehemu Mh. Regia Mtema katika viwanja vya Karimjee ambapo ilipelikea Mh. Kafulila kushangiliwa na wabunge wengi pasipo itikadi.
Bw. Mbatia anasisitiza kuwa hali hiyo imemdhalilisha yeye pamoja na chama chake cha NCCR Mageuzi.
Ikiwa zimebaki siku chache tuu vikao vya Bunge kuanza..............................................:hatari:
Chanzo chetu kitaendelea kutuhabarisha juu ya ombi hilo la Mbatia kwa serikali yetu sikivu.
Nawasilisha.
CHANZO: Ofisi ya Waziri Mkuu