Mbatia amwomba Waziri Mkuu amsaidie kumtoa Kafulila bungeni

April

Member
Nov 14, 2011
35
21

Wanajamii,

Katika hali isiyo ya kawaida baada ya Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Bw.James Mbatia na wenzake kumaliza mazungumzo Ikulu hivi majuzi, habari za uchunguzi zinasema ya kuwa, mojawapo ya hoja ilikuwa ni kuiomba serikali isaidie kuhakikisha Mh. David Kafulila (Mb. Kigoma Kusini) anatenguliwa ubunge.

Chanzo kinaeleza kuwa, mwishoni mwa wiki jana James Mbatia ameandika barua ndefu kwa Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akimuomba aingilie kati suala hilo kuhakikisha Bunge linatengua tamko la awali la kuendelea kumtambua David Kafulila kama mbunge.

Barua hiyo iliyoandikwa Ofisi ya Waziri Mkuu na kupigwa chapuo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mh. William Lukuvi
(kama ishara ya kuridhia pendekezo hilo la Mbatia), inaomba nguvu ya Waziri Mkuu itumike kubadili msimamo wa Bunge.
Pia imeelezwa kuwa, barua hiyo imelalamikia Ofisi ya Bunge kwa kumtambua Mh. David Kafulila kama mwakilishi wa wabunge wa NCCR kwenye msiba wa Marehemu Mh. Regia Mtema katika viwanja vya Karimjee ambapo ilipelikea Mh. Kafulila kushangiliwa na wabunge wengi pasipo itikadi.
Bw. Mbatia anasisitiza kuwa hali hiyo imemdhalilisha yeye pamoja na chama chake cha NCCR Mageuzi.




Ikiwa zimebaki siku chache tuu vikao vya Bunge kuanza..............................................:hatari:
Chanzo chetu kitaendelea kutuhabarisha juu ya ombi hilo la Mbatia kwa serikali yetu sikivu.
Nawasilisha.


CHANZO: Ofisi ya Waziri Mkuu
 
Kafulila kaza buti baba but kama vp rudi 2 home CDM 2takupokea lakini ukirudi plz...... Acha zile ishu za kiburi koz we mwenyewe uliwahi kumwambia chacha wangwe dat' uongozi bila demokrasia ni udikteta lakini demokrasia bila nidhamu ni fujo" so take care men na ukumbuke kauli yako.
 
Kwa maana hiyo inadhihirisha kuwa serikali inacheza na sheria/katiba,kwa upande wa bunge watatumia kujuana kutekeleza ombi hilo na kwa vile spika walimweka wao wanaweza kufanikiwa ila ili wasionekane kuwa wanaingilia bunge hasa ikizingatiwa kuwa bunge lilishatoa kauli,watacheza na mahakama ambazo wanazimudu kuliko kawaida,tusubiri hukumu ya fasta tofauti na watu walivyokuwa wanategemea!!!.
 
Me nilidhani nccr wangeachana na huyo kafulila. Kama amewazidi nguvu kwenye jimbo lake waelekeze majimbo mengine wana wabunge na kama mkoa mzima umeasi watengeneze mkoa mwingine kama dodoma au morogoro. Ipo mingi tu haina upinzani. Kuendelea kumfuatilia ni kumjenga kafulila na kunaidhofisha nccr. Ningeshauri wapige siasa hata mwaka mzima bila kumtaja kafulila waone kama atasikika.huu ni ushauri wa bure. Kuendelea kumfuatilia ni kumfanya aonekane muhimu bila sababu. Huyu sio shujaa kwanin mnataka aonekane shujaa?
 
ukiwa na wivu kwa wenzako kila jambo linafanywa na wengne unaona kama vle we unpitwa,mbatia kapoteza dira,hajitambui,anapenda mambo ya kijamii yafanyike kadri ya hisia zake,kumfuatia kafulila ni kupoteza muda,kesi ipo mahakamani kwanin asisubiri maamuz ya mahakama.dah!pole mbatia kwa kuonesha uwezo wako wa kuona kwa jicho la tatu ni mdogo.unataka kulipwa bilion 5 na bank ya nbc kisa walisema mbumbumbu wa mambo ya kibenki,unataka upewe ushndi wa halima mdee na then unagombania madaraka ya kafulila aliyopewa na wananchi wa kigoma.mbatia jitafakari then jipange mzee!
 
Tulipokwenda Ikulu tulizungumza na Mhe. Rais pamoja na baadhi ya mawaziri wake na Mwanasheria mkuu wa serikali kuhusu, mambo mawili; Mchakato wa kuipata katiba mpya, na ongozeko la gharama za umeme.

JF haina budi kulinda heshima yake dhidi ya upotoshaji. Barua inayotajwa na mwanzisha mada, si miongoni mwa hoja zilizopelekwa ikulu
 
JF haina budi kulinda heshima yake dhidi ya upotoshaji. Barua inayotajwa na mwanzisha mada, si miongoni mwa hoja zilizopelekwa ikulu
Mkuu zipo tuhuma za kupika zinazoweza kushusha credibility ya JF lakini si hii.sipendi viongozi wakiguswa humu wasivyopendwa wanakimbilia kusema heshima ya JF inashuka.

Nafikiri majibu ya hoja kama ulivyofanya ni vizuri zaidi maana watu watachambua pumba na mchele! Lakini pia bado hujajibu hoja Mbatia amemuandikia barua waziri mkuu kama mtoa mada anavyosema au ni uongo?
 
JF haina budi kulinda heshima yake dhidi ya upotoshaji. Barua inayotajwa na mwanzisha mada, si miongoni mwa hoja zilizopelekwa ikulu
Ndugu yangu Kahangwa, mimi naweza kuthibitisha niliyoyaandika. Je, nikithibitisha unaahidi utathibitisha unachotetea wewe?
 

Wanajamii,

Katika hali isiyo ya kawaida baada ya Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Bw.James Mbatia na wenzake kumaliza mazungumzo Ikulu hivi majuzi, habari za uchunguzi zinasema ya kuwa, mojawapo ya hoja ilikuwa ni kuiomba serikali isaidie kuhakikisha Mh. David Kafulila (Mb. Kigoma Kusini) anatenguliwa ubunge.

Chanzo kinaeleza kuwa, mwishoni mwa wiki jana James Mbatia ameandika barua ndefu kwa Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akimuomba aingilie kati suala hilo kuhakikisha Bunge linatengua tamko la awali la kuendelea kumtambua David Kafulila kama mbunge.

Barua hiyo iliyoandikwa Ofisi ya Waziri Mkuu na kupigwa chapuo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mh. William Lukuvi
(kama ishara ya kuridhia pendekezo hilo la Mbatia), inaomba nguvu ya Waziri Mkuu itumike kubadili msimamo wa Bunge.
Pia imeelezwa kuwa, barua hiyo imelalamikia Ofisi ya Bunge kwa kumtambua Mh. David Kafulila kama mwakilishi wa wabunge wa NCCR kwenye msiba wa Marehemu Mh. Regia Mtema katika viwanja vya Karimjee ambapo ilipelikea Mh. Kafulila kushangiliwa na wabunge wengi pasipo itikadi.
Bw. Mbatia anasisitiza kuwa hali hiyo imemdhalilisha yeye pamoja na chama chake cha NCCR Mageuzi.




Ikiwa zimebaki siku chache tuu vikao vya Bunge kuanza..............................................:hatari:
Chanzo chetu kitaendelea kutuhabarisha juu ya ombi hilo la Mbatia kwa serikali yetu sikivu.
Nawasilisha.


CHANZO: Ofisi ya Waziri Mkuu

Katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania haimpi Waziri Mkuu wala Spika wa Bunge mamlaka ya kufanya hivyo kwa sababu hakuna kipengelea kinachoelezea hatima ya mbunge anayefukuzwa au kuachishwa uanachama ni nini. Inazungumzia hatima ya mbunge aliyeacha nafasi hiyo kutokana na sababu nyingine zozote nje ya ile ya kuachishwa uanachama wa chama chake cha siasa. Mambo haya yaliwezekana wakati wa Chama Kimoja walipofukuzwa Hamad Rashid na Maalim Seif kutoka CCM, lakini ilikuwa possible kwa sababu utawala ule haukuwa unaendeshwa kwa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bali kwa katika ya CCM.

Kutokana na mapungufu haya ya katiba, kafulila ataendelea kuwa mbunge, huku akiendelea kuvutana na uongozi wa chama chake mpaka aidha, akijiunga na Chama kingine cha siasa au akiamua mwenyewe kujiuzulu nafasi yake ya ubunge. Vinginevyo kwa hali ya sasa, atachokosa sana sana ni ushirikiano na Chama Chake, lakini heshima yake kama mbunge, posho na mishahara, ipo pale pale mpaka mwaka 2015.
 
Ndugu yangu Kahangwa, mimi naweza kuthibitisha niliyoyaandika. Je, nikithibitisha unaahidi utathibitisha unachotetea wewe?

April, ninachokubishia wewe ni uongo kwamba hiyo hoja ni miongoni mwa tuliyoyapeleka Ikulu. Nilikuwepo Ikulu. Kama umeona barua ofisini kwa waziri mkuu sema hivyo, usiundanganye umma kwamba tulienda ikulu kuzungumza mambo ya Kafulila
 
April, ninachokubishia wewe ni uongo kwamba hiyo hoja ni miongoni mwa tuliyoyapeleka Ikulu. Nilikuwepo Ikulu. Kama umeona barua ofisini kwa waziri mkuu sema hivyo, usiundanganye umma kwamba tulienda ikulu kuzungumza mambo ya Kafulila
Kwa maelezo yako issue ya Kafulila hamkuizungumzia Ikulu ila mmemuomba Waziri Mkuu ashughulike nayo!
 
Mkuu zipo tuhuma za kupika zinazoweza kushusha credibility ya JF lakini si hii.sipendi viongozi wakiguswa humu wasivyopendwa wanakimbilia kusema heshima ya JF inashuka.

Nafikiri majibu ya hoja kama ulivyofanya ni vizuri zaidi maana watu watachambua pumba na mchele! Lakini pia bado hujajibu hoja Mbatia amemuandikia barua waziri mkuu kama mtoa mada anavyosema au ni uongo?

Nashauri usome tena nilichotofautiana na mtoa mada
 

Wanajamii,

Katika hali isiyo ya kawaida baada ya Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Bw.James Mbatia na wenzake kumaliza mazungumzo Ikulu hivi majuzi, habari za uchunguzi zinasema ya kuwa, mojawapo ya hoja ilikuwa ni kuiomba serikali isaidie kuhakikisha Mh. David Kafulila (Mb. Kigoma Kusini) anatenguliwa ubunge.

Chanzo kinaeleza kuwa, mwishoni mwa wiki jana James Mbatia ameandika barua ndefu kwa Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akimuomba aingilie kati suala hilo kuhakikisha Bunge linatengua tamko la awali la kuendelea kumtambua David Kafulila kama mbunge.

Barua hiyo iliyoandikwa Ofisi ya Waziri Mkuu na kupigwa chapuo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mh. William Lukuvi
(kama ishara ya kuridhia pendekezo hilo la Mbatia), inaomba nguvu ya Waziri Mkuu itumike kubadili msimamo wa Bunge.
Pia imeelezwa kuwa, barua hiyo imelalamikia Ofisi ya Bunge kwa kumtambua Mh. David Kafulila kama mwakilishi wa wabunge wa NCCR kwenye msiba wa Marehemu Mh. Regia Mtema katika viwanja vya Karimjee ambapo ilipelikea Mh. Kafulila kushangiliwa na wabunge wengi pasipo itikadi.
Bw. Mbatia anasisitiza kuwa hali hiyo imemdhalilisha yeye pamoja na chama chake cha NCCR Mageuzi.




Ikiwa zimebaki siku chache tuu vikao vya Bunge kuanza..............................................:hatari:
Chanzo chetu kitaendelea kutuhabarisha juu ya ombi hilo la Mbatia kwa serikali yetu sikivu.
Nawasilisha.


CHANZO: Ofisi ya Waziri Mkuu

Mkuu umeangalia factor gani ya kusema sirikali yetu ni sikivu?
 
Kaahangwa, go and tell Mbatia. NCCR must rethink itself.....

Tell your colleagues that Tanzania is no linger the teritory of the great man.........

and that if NCCR sticks to its dirty politics as it was not written to disturb reforms as it was started

and if it continues to be the personal property of Mr Mbatia....

then its going to die very soo.....n......

ni hayo tu. leave kafulila alone! hamumuwezi, umma hauwezi kukubali, serekali haiwezi kukubali, mahakama haiwezi kukubali, wala bunge haliwezi kukubali..........

acheni siasa za kishoga... huu ni wakati wa kufanya kazi.....you better find some business to do if you cannot politics...
 
April, ninachokubishia wewe ni uongo kwamba hiyo hoja ni miongoni mwa tuliyoyapeleka Ikulu. Nilikuwepo Ikulu. Kama umeona barua ofisini kwa waziri mkuu sema hivyo, usiundanganye umma kwamba tulienda ikulu kuzungumza mambo ya Kafulila

Naomba nirudie kama hujanielewa, nimesema hivii, mojawapo ya mliyoyazungumzia Ikulu ilikuwa ni pamoja na kumwomba Waziri Mkuu aingilie kati suala la Kafulila pamoja na kuwa ya kwamba kwa maandishi mmekwishaliwakilisha hilo kwake. And yes, barua ofisini kwa Waziri Mkuu nimeiona.
Sijaudanganya umma kama ninyi ndugu zangu washirika wa CCM mnavyotudanganya wakati upinzani wenu una mushkeli.


 
Back
Top Bottom