Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa amegeuka “mbogo” baada ya mkandarasi kutoka kampuni ya Shanx aliyekabidhiwa mradi wa maji Chalinze Mboga kudanganya vipimo vya ulazaji wa bomba huku akidai nyongeza ya gharama.
Waziri amekuta mitalo ya kulaza mabomba ikiwa mifupi mita 1.6 tofauti na makubaliano yaliopo kwenye mkataba ambao ni 1.8.
Pia amesema atakutana na mkandarasi na Dawasa ili kupitia upya maombi ya mkandarasi juu ya ongezeko la gharama za uchimbaji na ulazaji bomba.
Waziri Mbarawa amehoji gharama za uchimbaji na ulazaji bomba ya bilioni 3.9 kuwa ni kubwa, amesema ataunda tume itakayopitia upya mradi wa Chalinze Mboga
Waziri amekuta mitalo ya kulaza mabomba ikiwa mifupi mita 1.6 tofauti na makubaliano yaliopo kwenye mkataba ambao ni 1.8.
Pia amesema atakutana na mkandarasi na Dawasa ili kupitia upya maombi ya mkandarasi juu ya ongezeko la gharama za uchimbaji na ulazaji bomba.
Waziri Mbarawa amehoji gharama za uchimbaji na ulazaji bomba ya bilioni 3.9 kuwa ni kubwa, amesema ataunda tume itakayopitia upya mradi wa Chalinze Mboga