Kiroroma
JF-Expert Member
- Feb 6, 2009
- 370
- 114
Wakaazi wa Mbarali Mkoani Mbeya juzi wameamua kuwatolea uvivu kauli ya ukweli Kamati ya Bunge iliyotembelea shamba la Mbarali lililobinafsishwa katika mazingira ya kumpa mwekezaji asiye na tija kwa Taifa.Wakazi hao wemeweka bayana kwamba hawatapiga kura katika uchaguzi ujao,Kwa jinsi serikali ilivyowatendea.Je huko Kilombero, Basutu,Kahama,Chimala Ruvu,Mvomero na kwingineko ambako wananchi wamezulumiwa ardhi yao kwa kigezo cha uwekezaji watasemaje?Je wafugaji wa kimasai na kisukuma wanaohangaishwa huku na kule watasemaje?Elimu ya juu je?Wafanyakazi wanaopigwa dana dana ya kuongezewa mishahara wao watasemaje?Wamachinga wa Ilala ,Kiboroloni,Mbauda,Mwanjelwa ,Mwaloni wanatoa kauli gani?Je wakulima wadogo wadogo kule Lushoto,Mahenge,Igurusi walioahidiwa power Tillers je?Achalia mbali kauli ya maisha bora kwa kila Mtanzania.Mabango yaliyowekwa barabarani wakati ule tumeyahifadhi,Wanachi watayaweka kwenye vituo vya kupigia kura na alama ya kuuliza kulikoni???