Mbarali wametoa kauli wengine je?

Kiroroma

JF-Expert Member
Feb 6, 2009
370
114
Wakaazi wa Mbarali Mkoani Mbeya juzi wameamua kuwatolea uvivu kauli ya ukweli Kamati ya Bunge iliyotembelea shamba la Mbarali lililobinafsishwa katika mazingira ya kumpa mwekezaji asiye na tija kwa Taifa.Wakazi hao wemeweka bayana kwamba hawatapiga kura katika uchaguzi ujao,Kwa jinsi serikali ilivyowatendea.Je huko Kilombero, Basutu,Kahama,Chimala Ruvu,Mvomero na kwingineko ambako wananchi wamezulumiwa ardhi yao kwa kigezo cha uwekezaji watasemaje?Je wafugaji wa kimasai na kisukuma wanaohangaishwa huku na kule watasemaje?Elimu ya juu je?Wafanyakazi wanaopigwa dana dana ya kuongezewa mishahara wao watasemaje?Wamachinga wa Ilala ,Kiboroloni,Mbauda,Mwanjelwa ,Mwaloni wanatoa kauli gani?Je wakulima wadogo wadogo kule Lushoto,Mahenge,Igurusi walioahidiwa power Tillers je?Achalia mbali kauli ya maisha bora kwa kila Mtanzania.Mabango yaliyowekwa barabarani wakati ule tumeyahifadhi,Wanachi watayaweka kwenye vituo vya kupigia kura na alama ya kuuliza kulikoni???
 
Maneno tu hayo mkuu, subuiri ,atokeo ya kura unaweza kushangaa kuwa huko Mbarali ndiko chama kinachoongoza serikali wanayoichukia ndicho kitaongoza kwa kupata kura nyingi
 
Maneno tu hayo mkuu, subuiri ,atokeo ya kura unaweza kushangaa kuwa huko Mbarali ndiko chama kinachoongoza serikali wanayoichukia ndicho kitaongoza kwa kupata kura nyingi
MN,

Tatizo ni kwamba hata barua au matamko kama hayo hutayarishwa na wanasiasa badala ya kuacha ownership kwa wananchi wenyewe.

Kama tunataka mabadiliko ni lazima tuwashirikishe wananchi; wao ndio waelemishwe kuhusu kupotea kwa haki zao na kama wanaona kuna dhuluma basi waandike hizo barua au matamko.

Hizi barua za kuandikwa na kundi dogo huku wakijifanya wanawakilisha wananchi wote ndio zinadanganya watu na baadaye matokeo yanakuwa tofauti.

Sina uhakika na hili la Mbarali lakini kwa taarifa kama hizi kwa sehemu zingine uzoefu ni kwamba zinaandikwa na kundi dogo na kunakuwa hakuna uwakilishi wa kutosha wa wananchi wa kawaida.
 
Mkuu Kiloloma, Chimala ni sehemu ya Mbarali na wananchi wa hapo ndio hasa wenye mgogoro na serikali kuhusu kuuzwa kwa shamba la Kapunga. Hata hiyo kauli ni wananchi hao wa Chimala.

wakulima hao wadogo wilayani Mbarali, hususani wale wa Chimala wamehangaika sana kupigania hilo shamba la kapunga lakini serikali ilitia pamba masikioni, na hata ilipobaini kuwa mwekezaji huyo ni mbabaishaji bado imeendelea kumlinda.

Baada ya kuuzwa kwa mashamba ya Mbarali na Kapunga, uchumi wa wilaya hiyo umeshuka sana, miji ya Rujewa, Ubaruku, Igurusi na Chimala imedorora kutokana na kupungua kwa mzunguko wa pesa uliokuwa ukichochewa zaidi na kilimo cha mpunga.

Mathalani, kabla ya shamba la Kapunga kuuzwa, SACCOS ya wakulima wa Chimala ilifikia hatua ya kuchukua mkopo wa hadi shilingi bilioni tatu kutoka CRDB kupitia utaratibu wa stakabadhi ghalani, lakini hivi sasa hawana uwezo huo.

Ni wazi hiyo kauli itakuwa ya wakulima wadogo wilayani humo na sio ya kikundi kidogo kwani hawajaanza leo kupigania haki yao, walianza tangu serikali kutangaza kuyauza mashamba hayo lakini walikandamizwa na viongozi walafi wa serikali ya CCM wakiwemo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Dorolo, Mungai na Ngasongwa.
 
Maneno tu hayo mkuu, subuiri ,atokeo ya kura unaweza kushangaa kuwa huko Mbarali ndiko chama kinachoongoza serikali wanayoichukia ndicho kitaongoza kwa kupata kura nyingi

Toka lini kutokupiga kura kukabadilisha hali? ilitakiwa waseme hatutakipa CCM kura ndio tutawaelewa.Halafu ndugu zangu hawa wa vijijini musiwaamini hata siku 1,kanga na fulana hasira zote kwisha.Kumbukeni 95 hapohapo Mbarari mbunge aliopita alivunja rekodi kwa kupata kura nyingi nchi nzima(zaidi ya 90%)pamoja na juhudi za kina Mrema.
 
Hao wakazi hawajasikia "bailout' inakuja nini?Wanajuaje mwekezaji wao yupo 'accommodated' kwenye hiyo stimulus plan inayokuja?

Watulie waache kelele!
 
Kanga na nguzo za umeme zikitandikwa barabarani,fulana na shilingi elfu kumi kila mmoja watatoa tu kura kunakazi sana angalau wameonyesha hasira zao
 
Wakaazi wa Mbarali Mkoani Mbeya juzi wameamua kuwatolea uvivu kauli ya ukweli Kamati ya Bunge iliyotembelea shamba la Mbarali lililobinafsishwa katika mazingira ya kumpa mwekezaji asiye na tija kwa Taifa.Wakazi hao wemeweka bayana kwamba hawatapiga kura katika uchaguzi ujao,Kwa jinsi serikali ilivyowatendea.Je huko Kilombero, Basutu,Kahama,Chimala Ruvu,Mvomero na kwingineko ambako wananchi wamezulumiwa ardhi yao kwa kigezo cha uwekezaji watasemaje?Je wafugaji wa kimasai na kisukuma wanaohangaishwa huku na kule watasemaje?Elimu ya juu je?Wafanyakazi wanaopigwa dana dana ya kuongezewa mishahara wao watasemaje?Wamachinga wa Ilala ,Kiboroloni,Mbauda,Mwanjelwa ,Mwaloni wanatoa kauli gani?Je wakulima wadogo wadogo kule Lushoto,Mahenge,Igurusi walioahidiwa power Tillers je?Achalia mbali kauli ya maisha bora kwa kila Mtanzania.Mabango yaliyowekwa barabarani wakati ule tumeyahifadhi,Wanachi watayaweka kwenye vituo vya kupigia kura na alama ya kuuliza kulikoni???

Mkuu hakuna kitu. Somo la Busanda liko kila mahali katika nchi hii. CCM watachukua na Biharamulo mashariki pamoja na fyongo zote wanazowafanyia Watanzania. Maadamu hao watu wote wamefanywa ndondocha kwa kutojua hatua za kuchukua pale ambapo watawala wao wamewatelekeza, watarudishwa kundini kilaini na kuipa CCM ushindi wa kishindo iwekwenye chaguzi ndogo, 2010 au 2015!!

Kwa wale ambao tulikuwa vyuoni miaka ya 1990, nani aliamini kuwa ipo siku wanavyuo wanaweza kufaa jezi za kishenzi za kijani? Lakini baada ya kudanganywa na mikopo ya 100% mwaka 2005 kilitokea nini? Watanzania ni kama watoto wadogo. Unamchapa sana hata pale ambapo hajakosea au unamdanganya kuwa ukirudi mjini utamletea pipi ila baada ya muda mfupi bila kutimiza ahadi hata moja anakengeuka na kuanza kukuimbia nyimbo za shuleni kwao. Sina imani tena na watu wa dizaini ya Busanda!!
 
wakaazi wa mbarali mkoani mbeya juzi wameamua kuwatolea uvivu kauli ya ukweli kamati ya bunge iliyotembelea shamba la mbarali lililobinafsishwa katika mazingira ya kumpa mwekezaji asiye na tija kwa taifa.wakazi hao wemeweka bayana kwamba hawatapiga kura katika uchaguzi ujao,kwa jinsi serikali ilivyowatendea.je huko kilombero, basutu,kahama,chimala ruvu,mvomero na kwingineko ambako wananchi wamezulumiwa ardhi yao kwa kigezo cha uwekezaji watasemaje?je wafugaji wa kimasai na kisukuma wanaohangaishwa huku na kule watasemaje?elimu ya juu je?wafanyakazi wanaopigwa dana dana ya kuongezewa mishahara wao watasemaje?wamachinga wa ilala ,kiboroloni,mbauda,mwanjelwa ,mwaloni wanatoa kauli gani?je wakulima wadogo wadogo kule lushoto,mahenge,igurusi walioahidiwa power tillers je?achalia mbali kauli ya maisha bora kwa kila mtanzania.mabango yaliyowekwa barabarani wakati ule tumeyahifadhi,wanachi watayaweka kwenye vituo vya kupigia kura na alama ya kuuliza kulikoni???


kususia uchaguzi sio suluhisho...
Dawa ni kutoipigia kura ccm kwa kuwa imeshindwa kutukomboa kutoka kwenye lindi la umaskini
 
Kwa vile bado wana hamu na sisiemu yao wacha wakome na shida zao.
Tutaungana nao katika malalamiko yao watakapoonekana kuonyesha kwa vitendo kukerwa na vitendo vya mabosi wao sisiemu. Napo ni kwa kuwanyima kura 2010. Mbali na hivyo wasiwe na tegemeo lolote zaidi tu ya kuona wananyanyaswa katika nchi yao.
 
Back
Top Bottom