DaudiAiko
JF-Expert Member
- Dec 2, 2012
- 409
- 343
Wanabodi,
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Mnapojibu kwa kusema kazi iendelee basi kweli mnapeperusha bendera ya Tanzania kwenye jua kali katika msimu huu wa kiangazi.
Kwa mtoto aliyelilia wembe, pochi na Rais Samia ipo tayari kucheua na kumliwaza mtoto huyu. Kama unahitaji kutembea Dubai na buzi lako wiki ijayo, basi piga magoti kwenye msafara wa Rais Samia ili akupe mchongo.
Nasema haya yote kwasababu ya mazoea ya Rais kugawa hela zake kiholela kwa ajili ya mambo ambayo hayana mbele wala nyuma. Je milioni kumi kwa kila goli zilizopewa vilabu vya mpira vingeweza kuwasaidia wagonjwa wangapi Muhimbili?
Je, tiketi elfu tano zilizonunuliwa na Rais kwa ajili ya fainali ya Yanga zingeweza kuwasaidia watanzania wangapi wenye changamoto mbali mbali.
Haya yote yanadhihirisha kwamba hata kama Rais anakusudia kuwasaidia watanzania, bado anapenda political mileage ambazo siku zote hutupotezea muda.
Angeweza kuwatembelea watoto yatima kwenye vituo vyao na kutoa msaada ili aweze kuonekana mtu mwema na wananchi.
Siku zote, charity nzuri hutoka moyoni na kutoka kwa watu ambao hawa dhamini sana recognition. Wahenga walisema "Tenda wema nenda zako".
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Mnapojibu kwa kusema kazi iendelee basi kweli mnapeperusha bendera ya Tanzania kwenye jua kali katika msimu huu wa kiangazi.
Kwa mtoto aliyelilia wembe, pochi na Rais Samia ipo tayari kucheua na kumliwaza mtoto huyu. Kama unahitaji kutembea Dubai na buzi lako wiki ijayo, basi piga magoti kwenye msafara wa Rais Samia ili akupe mchongo.
Nasema haya yote kwasababu ya mazoea ya Rais kugawa hela zake kiholela kwa ajili ya mambo ambayo hayana mbele wala nyuma. Je milioni kumi kwa kila goli zilizopewa vilabu vya mpira vingeweza kuwasaidia wagonjwa wangapi Muhimbili?
Je, tiketi elfu tano zilizonunuliwa na Rais kwa ajili ya fainali ya Yanga zingeweza kuwasaidia watanzania wangapi wenye changamoto mbali mbali.
Haya yote yanadhihirisha kwamba hata kama Rais anakusudia kuwasaidia watanzania, bado anapenda political mileage ambazo siku zote hutupotezea muda.
Angeweza kuwatembelea watoto yatima kwenye vituo vyao na kutoa msaada ili aweze kuonekana mtu mwema na wananchi.
Siku zote, charity nzuri hutoka moyoni na kutoka kwa watu ambao hawa dhamini sana recognition. Wahenga walisema "Tenda wema nenda zako".