UZUSHI Maziwa ya kwanza ya Mama yenye rangi ya manjano ni hatari kwa mtoto

Baada ya tathmini, tumebaini kuwa taarifa hii ni ya uzushi
Kumekuwa na mtazamo kuwa maziwa ya kwanza ambayo mama huyapata mara baada ya kujifungua si maziwa yafaayo kwa mtoto. kutokana na mtazamo huu wanawake wengine huyakamua na kuyamwaga mpaka yanapotoka maziwa ya rangi nyeupe.

1667453954617.png
 
Tunachokijua
Wataalamu wa Afya wanaeleza kuwa jambo hili halina ukweli wowote.

Maziwa ya njano ni maziwa ya mwanzo, mazito yenye rangi ya njano ambayo hutoka siku chache za mwanzo baada ya kujifungua.

Maziwa ya kwanza ya mama kwa kitaalamu huitwa colostrum, ndiyo maziwa muhimu zaidi kuliko maziwa yoyote yale mama atakayokuja kuyatoa.

Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa haya ni maziwa ya kwanza ambayo hufanya kazi kama chanjo ya kwanza kabisa kwa mtoto. Maziwa haya ni chakula kamili chenye virutubishi vingi, na pia yanatoa kinga maalum dhidi ya maradhi.

Maziwa ya njano humsaidia mtoto kutoa kinyesi cha mwanzo chenye rangi ya kijani au nyeusi ambacho humfanya mtoto aumwe tumbo siku za mwanzo kama hatanyonya.
Hilo linahitaji utafiti wa kina kwa mtu na mtu kwa sababu hata miili ya binadamu imebadika mno kutokana usasa mwingi nao binadamu tumekuwa kama ni wa kisasa.
 
YALE MAZIWA YANGEKUA SIO BORA SIDHANI KAMA MANESI WANGEWARUHUSU WAZAZI WAWANYONYESHE WATOTO MARA TU BAADA YA KUJIFUNGUA.
 
Wewe uliyatumia? Kama uliyatumia ulipata athari/hatari gani?

Si kila unachoambiwa na mzungu ni sahihi.
 
Yale ndo maziwa yanayotengeneza kinga mwili ya mtoto na akikosa yale afya yake udhoofu

Yale ndo maziwa buana
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom