Mazishini

tofyo

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2013
Posts
2,759
Reaction score
768
Kadri siku zinavyoenda mambo yanabadilika. Unaweza kuhudhuria misiba mingine badala ya kulia ukajikuta unafyatuka kicheko.

Jamaa mmoja msibani nimemsikia analalamika kwenye simu kwamba kwanini apewe laki 5 kwa msiba wa baba yake mzazi, na atakapokufa yeye mwenyewe kama memba wa kikundi apewe milioni 1?

Sasa alikuwa anawaomba wanakikundi wenzie kwamba yeye wambadilishie iwe kama amekufa yeye kwa sasa. Halafu atakapokufa yeye mwenyewe, nafasi hiyo ifanywe kana kwamba baba yake ndiye aliyekufa.

Misiba kama hii ndo utakuta mtu analia huku anatazama sinia la michango.
 
SHEIKH:Waislaam, makaburi yetu yamekua Machafu, wapita njia wanatupa kila aina ya takataka hata taulo za kina mama "Asthakafulilai".
Nimeitisha hiki kikao niwaambieni kuna haja kujenga uzio kuzunguka makaburi yetu. Fundi amesema itagharimu million mbili mnasemaje? Muumini wa Kwanza:Tuchange buku buku, wapili: Elfu kumikumi. Mbwia unga: SHEIKH kwani kuna maiti gani ishatoroka mpaka tutumie Shs 2m kujenga uzio?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…