Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 2,208
- 4,705
Maziko ya Waliokufa kwa Mlipuko wa Bomu Afghanistan Yafanyika.
Mazishi yameanza kwa waathirika wa milipuko kadhaa karibu na shule ya sekondari huko Kabul Jumamosi, ambayo sasa inadaiwa kuua zaidi ya watu 50.
Milipuko hiyo ilitokea wakati wanafunzi wakitoka kwenye jengo hilo. Waathiriwa wengi walikuwa wasichana, maafisa walisema.
Hakuna mtu aliyekiri kutekeleza shambulio hilo huko Dasht-e-Barchi - eneo ambalo mara nyingi hushambuliwa na wanamgambo wa Kisunni.
Maafisa wa serikali ya Afghanistan waliwalaumu wanamgambo wa Taliban kwa shambulio hilo, lakini kundi hilo lilikana kuhusika.
Mshindi wa Tuzo ya Nobel na mwanaharakati Malala Yousafzai - ambaye alipigwa risasi kichwani na Taliban mnamo 2012 - alichapisha ujumbe kuhusu "shambulio baya" kwenye mtandao wa Twitter.
"Moyo wangu uko pamoja na familia za wahanga wa shule ya Kabul," aliandika.
Lengo hasa la umwagaji damu wa Jumamosi halieleweki. Milipuko hiyo inakuja wakati ambapo kuna kuongezeka kwa vurugu wakati Marekani inataka kuondoa askari wake wote kutoka Afghanistan ifikapo tarehe 11 Septemba.
Mazishi yameanza kwa waathirika wa milipuko kadhaa karibu na shule ya sekondari huko Kabul Jumamosi, ambayo sasa inadaiwa kuua zaidi ya watu 50.
Milipuko hiyo ilitokea wakati wanafunzi wakitoka kwenye jengo hilo. Waathiriwa wengi walikuwa wasichana, maafisa walisema.
Hakuna mtu aliyekiri kutekeleza shambulio hilo huko Dasht-e-Barchi - eneo ambalo mara nyingi hushambuliwa na wanamgambo wa Kisunni.
Maafisa wa serikali ya Afghanistan waliwalaumu wanamgambo wa Taliban kwa shambulio hilo, lakini kundi hilo lilikana kuhusika.
Mshindi wa Tuzo ya Nobel na mwanaharakati Malala Yousafzai - ambaye alipigwa risasi kichwani na Taliban mnamo 2012 - alichapisha ujumbe kuhusu "shambulio baya" kwenye mtandao wa Twitter.
"Moyo wangu uko pamoja na familia za wahanga wa shule ya Kabul," aliandika.
Lengo hasa la umwagaji damu wa Jumamosi halieleweki. Milipuko hiyo inakuja wakati ambapo kuna kuongezeka kwa vurugu wakati Marekani inataka kuondoa askari wake wote kutoka Afghanistan ifikapo tarehe 11 Septemba.