Maziko ya "Ngosha" aliyebuni Nembo ya Taifa utata

Maziko ya "Ngosha" aliyebuni Nembo ya Taifa utata

Hapa michango ya rambi rambi kwa kiongozi wetu wa mkoa inamuhusu,ngoja mbio za mwenge ziishe
 
Yaani hao ndugu zake watakuwa wanaona aibu kwa kumtelekeza ndugu yao miaka yote hiyo, maskini babu wa watu ndio kusema hakuwa na mke wala watoto
 
Tatizo watu wanaogopa gharama za mazishi....serikali iseme itagharamia uone kama ndg hawajitokezi
 
Siku nyingine wawe wabunifu mnapoita ndugu wa marehemu ambao wamesusia maiti.

Semeni serikali inatambua mchango wa mzee huyu katika taifa hili, hivyo tunawaomba ndugu wasiiachie serikali pekee msiba huu mzito hususani ukusanyaji wa rambirambi ambazo zinaendelea kutolewa. Ni vyema ndugu wajitokeze ili wakabidhiwe kilichopatikana na waendelee kusimamia wenyewe kitakachopatikana.

Kesho ukoo mzima upo hospitali.
 
kwani
Hapo ingekuwa wanatafutwa ndugu wa marehemu ili wakabidhiwe pesa za kumtunza mzee basi pasingetosha ila kwa sababu ni msiba watu wamepiga kimya.


Anyway ndivyo binadamu tulivyo
msiba hauna pesa?,tembelea Arusha ujue yanayojiri, RIP ngosha, RIP Philemon kiwelu ndesapesa
 
Labda wamwulize mbunge wa Geita mjini Mh. Constantine Kanyasu atakuwa ndugu yake? Au wamwulize Sianga wa madawa ya kulevyesha!!
 
Ni jambo la aibu sana na si la Kistaarabu hasa kwa Watanzania ambapo Mtu unajua kabisa kuwa Ndugu yako amefariki dunia halafu mnatafutwa mnanyamaza. Na usikute hao hao ambao wamenyamaza Mzee ndiyo alitumia Pesa zake zote za Kiinua mgongo kuwasomesha hadi wengi wao leo hii wamefanikiwa Kimaisha. Waafrika sijui nani alituroga hakyanani!
Sio waafrika bali watanzania
 
Nukuu kutoka ktk nyimbo ya Afande sele
"Sasa ni mambumbumbu,
hatuna ata kumbukumbu,
Waafrika kama manyumbu.

Au laana za mababu ndio zinazotupatabu,
Maana hatuna haya wala haibu.
Walimfukuza mkoloni na kumwita mnyonyani,na sisi tumemrudisha na kumwita mwekezaji ,wanatuona vichwa maji."
 
Siku nyingine wawe wabunifu mnapoita ndugu wa marehemu ambao wamesusia maiti.

Semeni serikali inatambua mchango wa mzee huyu katika taifa hili, hivyo tunawaomba ndugu wasiiachie serikali pekee msiba huu mzito hususani ukusanyaji wa rambirambi ambazo zinaendelea kutolewa. Ni vyema ndugu wajitokeze ili wakabidhiwe kilichopatikana na waendelee kusimamia wenyewe kitakachopatikana.

Kesho ukoo mzima upo hospitali.
🙂🙂🙂🙂🙂🙂 very interesting wakuchague uwe msemaji waserikali mkuu.
 
Siku nyingine wawe wabunifu mnapoita ndugu wa marehemu ambao wamesusia maiti.

Semeni serikali inatambua mchango wa mzee huyu katika taifa hili, hivyo tunawaomba ndugu wasiiachie serikali pekee msiba huu mzito hususani ukusanyaji wa rambirambi ambazo zinaendelea kutolewa. Ni vyema ndugu wajitokeze ili wakabidhiwe kilichopatikana na waendelee kusimamia wenyewe kitakachopatikana.

Kesho ukoo mzima upo hospitali.

I see! Kama nakuona vile umepewa kitengo cha Msigwa, unatoa taarifa kwa niaba ya Serikali...
 
basi serikali itangaze kuwa inatafuta ndugu ili wapewe rambi rambi ione kivumbi chake....
kwa serikali ipi ya kupeleka rambirambi kwa wafiwa? ..nani ataamini? wala hawatajitokeza kwakuwa wanaijua serikali hii, badala yake wanaweza wakachangishwa wao kisha michango hiyo ikachukuliwa na serikali!
 
Ndugu zake wana aibu ya kujitokeza maana walimtelekeza ila kwa kuwa kuna waliotajwa itakuwa wameumbuka.
 
Bila shaka humu ndani kuna wanaJF waishio Sengerema.
Wachukue picha za marehemu Ngosha wafanye kuulizia nduguze hapo mitaa ya Ibisabageni ndipo zilipo nyumba za NHC.
 
Back
Top Bottom