Maziko ya babu yake mwanajf sipo

Maziko ya babu yake mwanajf sipo

pakajimmy asante sana kwa kutuwakilisha ama kweli wewe mfano wa kuigwa.tunakushukuru sana kwa kuwakilisha JF na labda mkuu Sipo alizidiwa na shughuli za msiba akashindwa kukutana na mungu akijalia mtafanikiwa kukutana mjuane zaidi.


tunakushukuru tena kwa kutuwakilisha wana-JF kwenye msiba huu.
 
Fanya ya KiJF zaid basi Kiongozi!

Thanx alot Fidel180.Nawashukuru kwa kunipa moyo, nimeamini kuwa kumbe together we can move mountains here!...BBlessed!
Yes we can!

Nimejisikia raha saana, Utadhani mimi ndo mfiwa!
PJ endelea na moyo huo wa upendo, Mungu atakubariki, lakini hii yote ni kupitia JF.
Nami nimeguswa pia. PakaJimmy umefanya jambo la kipekee, shukrani kwa kutuwakilisha. Nimefurahia kusoma ujumbe uliotuletea kutoka huko Arusha kwa akina Sipo.

Sipo nimewahi kuwa na interaction naye hapa JF. Moja kati ya mambo ninayokumbuka ni siku nilipofungua JF na kukuta ujumbe wake alioniandikia kwenye PM. (Sikuwa mlengwa pekee, aliandika copy kwa member wengine wanne pia) ....Alinisabahi na kuelezea kwa ufupi maendeleo ya shughuli zake. Mwishowe aliandika hivi:
Nimesema nikujulie hali ndugu yangu
kazi njema na kila la kheri
best regards
Sipo
Kwangu huu ulikuwa ni ujumbe wa aina ya kipekee. Nimezoea kuandikiwa pale mtu anapokuwa na shida fulani. Ni mfano wa kuigwa kwa kweli - sina shaka kwamba Sipo ni mtu anayeishi vizuri na ndugu na jamaa.

Kwa mara nyingine ndugu Sipo, pole sana kwa msiba. Mungu akubariki sana!
 
hahaaa, kama kawaida.
ujue kwasasa JF ni kama familia kubwa iliyotapakaa kila kona. wazo langu ni kwamba hata wamikoani wajikusanye na kufanya get tugeza zao itasaidia kufahamiana nje ya JF kama wapwa na mabinamu wa hapa dar ndani ya zero pub, chawote bar na kwingineko utatukuta tu!.
Sasa mbona unatubagua? How about ambao tupo ughaibuni ???
Hatualikwi???? just joking but tukumbukwe vile vile..ahahhhaaa
Anyway ubarikiwe sana kwa moyo wako.....long live JF.
 


Ndugu WanaJF,kama mlivyoona hiyo introduction hapo juu, ni kwamba muda huu ndo nawasili mjini Arusha tokea eneo yalikofanyika mazishi ya Babu Mpendwa wa mwanaJF wetu mahiri, SIPO.

Mimi kama mjuavyo niko huku Arusha, na baada ya kukutana na thread hiyo hapo juu, nilim`PM huyu bwana SIPO nikimsihi anijulishe kuhusu tarehe na Eneola mazishi mara atakapowasili Arusha, ambapo kweli alinifahamisha kwamba wangemzika leo [j3,23/11/2009], katika eneo liitwalo Bangata, umbali wa KM10 toka Arusha mjini, miguuni mwa Mlima Meru.

Nami bila ajizi nimeaga kazini kwangu mapema, na kuelekea pande za eneo hilo geni kwangu, huku nikijiamini kuwa naenda kuiwakilisha JAMII-FORUMS katika mazishi hayo, japo kwa uhakika simjui kabisa kwa sura mwenyeji wangu SIPO!

Kikwetu wanasema "Nyumba yenye matanga haijifichi"! Kwa Neema za Mungu niliwasili mahala huko baada ya kuulizia njia kwa kila niliyemwona usoni akikatiza!

Misa rasmi ya kumwombea Marehemu huyo, Mzee Michael Tomito(81), ambaye alikuwa pia Mchungaji wa KKKT, ilianza mida ya saa 7mchana katika kanisa dogo la kijijini hapo, ambapo ilihudhuriwa na Maaskofu wa2, Askofu Thomas Laizer wa Dayosisi ya Arusha na Askofu Akyoo wa Meru. Pamoja na wakuu hao, alikuwepo pia EL, Wachungaji tele toka mji mzima wa Arusha, na ujumbe wa vyama vya siasa na wa kiserikali.

Lakini kikubwa zaidi nilichoshuhudia na kupigwa nacho butwaa ni umati wa watu, ambapo kwa hesabu za haraka walizidi 2000.

Baada ya Misa hiyo, Msafara wa kuelekea Kaburini umeanza, ambapo ni shambani kwake Marehemu, na muda wa saa 9.00mchana Mzee huyo amepumzishwa mahala pake pa kudumu, na kuachana moja kwa moja na dhiki za dunia hii!

Aidha, Mzee huyo Mchungaji Veterani hapa Arusha ameacha watoto 7, wajukuu 16(INCLUDING SIPO), na vilembwe 2, ambapo mkewe alishatangulia kunako haki mwaka2007.

Katika salamu za rambirambi zilizotolewa na vikundi, mbalimbali vya kijamii, vimeeleza kuwa Mzee huyu aliyezaliwa mwaka 1928 alikuwa msomi wa wakati wake, na kabla ya kuanza kusomea Uchungaji katika chuo cha Makumira, alisomea na kufanya kazi katika fani za Kilimo, Afya Chama tawala na sekta nyingine lukuki.

Aidha ameelezewa kuwa alikuwa Mfano wa kuigwa katika jamii na Taifa kwa ujumla.MUNGU AILAZE PEMA ROHO YA MAREHEMU MZEE HUYU!

Hadi najipanga kuondoka eneo hilo, kwa hakika sijafanikiwa kumfahamu Mwanaharakati SIPO, japo nimesalimiana na watu kadha MBAPO HUENDA MMOJAWAPO NDIYE. Anyway, labda ndiyo raha/Karaha ya JF!

Lakini naamini nimetimiza wajibu wangu kama MwanaJF, wa KUWAWAKILISHA, ipasavyo, na nadhani wanaJF mtanisupport na kunipa BIG-UP kwa kazi hiyo!.

NAWASASILISHA .[/QUOTE

pamoja mkuu hiyo ni safi sana, sasa nakumbuja jamaa moja aliwahi kuongea hapa kuwa wakati unatoa maoni yako lazima uwe mwangalifu sana maana unaweza kuwa unamtukana hata mzazi wako, na huwezi jua mtu atakuja kukusaidia lini na nini sasa kama hata njiani unaweza kuwa unapita ukapata tatizo hata kama uko na gari inaweza kupata shida na pengine ni usiku au ni karibu na vibaka akajitokeza mwana jf mmoja akakusaidi hata kwa kukupatia fundi tayari ni msaada lakini kwavile tu hamjuani kwamba wote ni wana jf na pengin e mlikwishakuwa na tofauti katika huku mtandao. nimeona somo kubwa sana hapa la kujifunza, many thanks pj n b blesi
 
PJ ahsante sana kwa kuiwakilisha jamii nzima ya JF,Mungu akubariki.Na kwako SIPO pole sana kwa msiba huu, Mungu na akupe tumaini la uzima ule wa milele Amen.
 
mkuu PJ hakika unastahili pongezi, huu ni moyo halisi wa kitanzania, upendo na ushirikiano, hongera na pole kwa mwenzetu SIPO
 
Jamani nakosa cha kuandika kusema kweli nimefarijika sana. Ninachoweza kusema PakaJimmy Mungu akubariki sana kwa kufika, ilikuwa bahati mbaya tu hatukuonana. Nashukuru sana tena sana kwa WanaJF wote. Nimepungukiwa na maneno kabisa ya kusemea wema wa mioyo yenu. Be blessed all the days
 
Jamani nakosa cha kuandika kusema kweli nimefarijika sana. Ninachoweza kusema PakaJimmy Mungu akubariki sana kwa kufika, ilikuwa bahati mbaya tu hatukuonana. Nashukuru sana tena sana kwa WanaJF wote. Nimepungukiwa na maneno kabisa ya kusemea wema wa mioyo yenu. Be blessed all the days

Pole sana mkuu. Yote mipango ya Mungu. PJ ni shujaa wetu. Kuna thread ya PJ shujaa wa JF. Nenda ukatundikie nishani yako kule. Tuko pamoja mkuu
 
Ndugu WanaJF,kama mlivyoona hiyo introduction hapo juu, ni kwamba muda huu ndo nawasili mjini Arusha tokea eneo yalikofanyika mazishi ya Babu Mpendwa wa mwanaJF wetu mahiri, SIPO.

Mimi kama mjuavyo niko huku Arusha, na baada ya kukutana na thread hiyo hapo juu, nilim`PM huyu bwana SIPO nikimsihi anijulishe kuhusu tarehe na Eneola mazishi mara atakapowasili Arusha, ambapo kweli alinifahamisha kwamba wangemzika leo [j3,23/11/2009], katika eneo liitwalo Bangata, umbali wa KM10 toka Arusha mjini, miguuni mwa Mlima Meru.

Nami bila ajizi nimeaga kazini kwangu mapema, na kuelekea pande za eneo hilo geni kwangu, huku nikijiamini kuwa naenda kuiwakilisha JAMII-FORUMS katika mazishi hayo, japo kwa uhakika simjui kabisa kwa sura mwenyeji wangu SIPO!

Kikwetu wanasema "Nyumba yenye matanga haijifichi"! Kwa Neema za Mungu niliwasili mahala huko baada ya kuulizia njia kwa kila niliyemwona usoni akikatiza!

Misa rasmi ya kumwombea Marehemu huyo, Mzee Michael Tomito(81), ambaye alikuwa pia Mchungaji wa KKKT, ilianza mida ya saa 7mchana katika kanisa dogo la kijijini hapo, ambapo ilihudhuriwa na Maaskofu wa2, Askofu Thomas Laizer wa Dayosisi ya Arusha na Askofu Akyoo wa Meru. Pamoja na wakuu hao, alikuwepo pia EL, Wachungaji tele toka mji mzima wa Arusha, na ujumbe wa vyama vya siasa na wa kiserikali.

Lakini kikubwa zaidi nilichoshuhudia na kupigwa nacho butwaa ni umati wa watu, ambapo kwa hesabu za haraka walizidi 2000.

Baada ya Misa hiyo, Msafara wa kuelekea Kaburini umeanza, ambapo ni shambani kwake Marehemu, na muda wa saa 9.00mchana Mzee huyo amepumzishwa mahala pake pa kudumu, na kuachana moja kwa moja na dhiki za dunia hii!

Aidha, Mzee huyo Mchungaji Veterani hapa Arusha ameacha watoto 7, wajukuu 16(INCLUDING SIPO), na vilembwe 2, ambapo mkewe alishatangulia kunako haki mwaka2007.

Katika salamu za rambirambi zilizotolewa na vikundi, mbalimbali vya kijamii, vimeeleza kuwa Mzee huyu aliyezaliwa mwaka 1928 alikuwa msomi wa wakati wake, na kabla ya kuanza kusomea Uchungaji katika chuo cha Makumira, alisomea na kufanya kazi katika fani za Kilimo, Afya Chama tawala na sekta nyingine lukuki.

Aidha ameelezewa kuwa alikuwa Mfano wa kuigwa katika jamii na Taifa kwa ujumla.MUNGU AILAZE PEMA ROHO YA MAREHEMU MZEE HUYU!

Hadi najipanga kuondoka eneo hilo, kwa hakika sijafanikiwa kumfahamu Mwanaharakati SIPO, japo nimesalimiana na watu kadha MBAPO HUENDA MMOJAWAPO NDIYE. Anyway, labda ndiyo raha/Karaha ya JF!

Lakini naamini nimetimiza wajibu wangu kama MwanaJF, wa KUWAWAKILISHA, ipasavyo, na nadhani wanaJF mtanisupport na kunipa BIG-UP kwa kazi hiyo!.

NAWASASILISHA .
hongera sana kaka!
tunashukuru kwa kutualika.
karibu get tugedha yetu ya december tukufanyie maisha
 
Jamani nakosa cha kuandika kusema kweli nimefarijika sana. Ninachoweza kusema PakaJimmy Mungu akubariki sana kwa kufika, ilikuwa bahati mbaya tu hatukuonana. Nashukuru sana tena sana kwa WanaJF wote. Nimepungukiwa na maneno kabisa ya kusemea wema wa mioyo yenu. Be blessed all the days

Sipo,pole sana kwa kufiwa na babu yako,nadhani uliposoma thread ya PJ ulifarijika sana,PJ amefanya kitendo ambacho kimetugusa wote ni kitendo cha kiungwana na kinadhihirisha UPENDO,tunaungana nawe kusema Mungu ambariki sana.
 
Jamani nakosa cha kuandika kusema kweli nimefarijika sana. Ninachoweza kusema PakaJimmy Mungu akubariki sana kwa kufika, ilikuwa bahati mbaya tu hatukuonana. Nashukuru sana tena sana kwa WanaJF wote. Nimepungukiwa na maneno kabisa ya kusemea wema wa mioyo yenu. Be blessed all the days

Usijali Mkuu SIPO,
Tuko pamoja sana.
Karibu tena rasmi kwenye mapambano, YA KALE YAMEPITA, TAZAMA SASA NI MAPYA!
 
Back
Top Bottom