Maxmalipo, Samsung, hamjawatendea haki Tecno

Maxmalipo, Samsung, hamjawatendea haki Tecno

Mbuzi anakula kutokana na urefu wa kamba yake. Tajiri na SAMSUNG, masikini na TECNO
 
Kama zote matumizi yanafanana huo ni uchuro tu na kutaka kujionyesha mbele za watu... Zote zinafaa kuandika thread JF inatosha Tofauti ni uwezo wa Camera tu
 
samsung wanabifu na tecno.tecno kaharibu biashara ya samsung
 
Sumsung washazoea hayo walikua na kesi na iphone kwa kukopi baadhi ya vtu ktk simu zao iphone walishinda iyo kesi marekani,mwaka jana.wanasheria ni hela hizo wafateni techno mfanye kazi.
 
Yani hio techno unakua unasikia raha kuitumia ukiwa alone ila ukiwa na washkaj afu wakakuuliza hio ni simu gani unatumia unaanza kujibu ooh hii techno afu usiione hivi ina speed kali, ram kubwa, camera ya kutosha yan lazima utoe maelezo ya kutosha wkt ukitoa Samsung au iPhone huna haja ya kujieleza, hahah
 
Wabongo bhana, mtu kapanga, anapanda daladala kila siku, mlo mara mbili au moja, kijijini kwenu hata bati umeshindwa kuwanunulia wazee wako, chumba chenyewe ulichopanga hata marafiki kuwapeleka unaona aibu, leo hii unasema Tecno is inferior, too low, haina hadhi. Hizi tabia za kimaskini tuziache we kama unaona haikufai n wewe lakini usikashifu wengine wakati unaishi kwa kujionyesha tu.

Note: walengwa wanajijua sio wote.

Inferior goods ni inferior goods tu regardless umewanunulia bati wazaz kijijini au umepanga geto kwa mfuga mbwa, hio hai justify techno kuwa 1st priority kwa Samsung, hahah
 
Inferior goods ni inferior goods tu regardless umewanunulia bati wazaz kijijini au umepanga geto kwa mfuga mbwa, hio hai justify techno kuwa 1st priority kwa Samsung, hahah

umeona mkuu yani hayabadilishi chochote!!
 
Mi na itel yangu naperuzi JF bila shida. Huku nikiwa na Oking pembeni......
 
Inferior goods ni inferior goods tu regardless umewanunulia bati wazaz kijijini au umepanga geto kwa mfuga mbwa, hio hai justify techno kuwa 1st priority kwa Samsung, hahah

Inferior goods haimaanishi kuwa mmiliki ni inferior na mmiliki wa super brand kuwa ni superior.
 
Habari zenu wakuu,

Naomba niingie moja kwa moja kwenye huu uonezi wa kibiashara unaofanywa na hawa Maxmalipo wakiwa kama wakala wa kuuza simu za Samsung.

Kuna tangazo lao linaonekana kwenye Runinga likimuonyesha mwanadada mmoja akimwambia mkaka wewe mpakaleo unatumia simu zisizofaa yule kaka amekaa juu ya ya bodaboda ameshika simu wameonyesha mpaka brand yake kabisa ni Tecno.

Nimeshindwa kupata picha lakini wanajamvi kwa hili sio sawa kibiashara. "Waswahili wanasema kimfaacho mtu chake".

Hata kamaTecno ndo hivyo hawakupaswa kuwafanyia vile wahusika waliangalie hili kwa undani.. Sio sawa
Wala usijali mkuu kimpe hii siyo hapa tu hapo zamani za miaka ya 80 magari ya kijapani yalipigwa vita sana kwenye matangazo ya biashara huko Marekani mimi niliona matangazo ya wazi kabisa yanasema don't buy Japannese.,lakini miaka ilivyozidi kwenda pumba zilijulikana ni zipi na ngano ni ipi magari ya kijapani soko lake lilikua kiasi cha baadhi ya viwanda vya magari ya kimarekani kufunga matawi yao na kuuzwa kwa makampuni ya nje.
Tecno simu zao ziliingia hapa nchini watu wakadhani ni michina ile iliyokuwepo wakati rule lakini mda ulivyozidi kwenda ziliendelea kuzoeleka sasa hivi tunapoyaongea haya simu za tecno zimekamata asilimia kubwa katika soko la simu kuna baadhi ya brand kama Siemens,motorola n.k zimepotezwa kabisa na myama Tecno, Samsung wajiandae kunyolewa kiwembe kikali kinakaribia.
 
Hahahaa, wamejilinganisha na TECNO sababu hivyo ndiyo viwango vyao! Mwisho wa simu ni iPhone tu, Samsung ni waigizaji, wanatengeza matakataka na kuwasokomeza watumiaji....jinga sana! Hata waigeje kwa iPhone watangoja sana, Samsung simu za wanafunzi na mamburula!

Masikini ndo zetu kashifa
 
Niseme tuu samsung Org zinazokuja huku kwetu kutoka china na india nazo haziko kwenye kiwango kizuri ni tofauti kabisa na zile zinazotoka Korea zinazopelekwa ulaya,Marekani na canada.

Ukaaaji wa chaji betri zake ni dhaifu, ni bora Tecno, Hili soko la tecno hata wakilifanyia fitna wameshachelewa, hawa jamaa wa tecno wamejipanga kikweli kweli na wanatoa model mpya kila baada ya miezi 3.

Hapa kwetu Nokia, samsung wote kwa saivi wanajiendesha kihasara ila kwa huwaei kwakua nao wanabadilika tutegemee mafanikio kwao
 
Masikini ndo zetu kashifa

Maskini ananunua samsung? Maskini ni yule ambaye hajuwi leo atakula nini, na usiku anaomba usiingie kwa sababu hajuwi atalala wapi! Msimamo wangu uko palepale, SAMSUNG SIMU ZA WANAFUNZI! Wamekalia kudesa kwa Apple na kujisogezasogeza ili nao wafanane na tufaa wakati ni madonga tu!
 
Hahahaa, wamejilinganisha na TECNO sababu hivyo ndiyo viwango vyao! Mwisho wa simu ni iPhone tu, Samsung ni waigizaji, wanatengeza matakataka na kuwasokomeza watumiaji....jinga sana! Hata waigeje kwa iPhone watangoja sana, Samsung simu za wanafunzi na mamburula!

Usiseme hivyo mkuu, wengine tumetumia Samsung kusoma madongo yako hatukuangalii vizuri sana... Samsung Oyee!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom