Maxmalipo mhujumu namba moja wa UDART

Maxmalipo mhujumu namba moja wa UDART

nabiitz

Senior Member
Joined
Jan 29, 2014
Posts
157
Reaction score
32
Takribani sasa ni zaidi ya wiki tatu nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu sana sakata na kile kinachotaka kionekana kana kwamba kuna mgogoro ama mkwamo wa uendeshaji wa mradi wa basi yaendayo kasi "UDART" ambayo kimsingi huduma hii imeendelea kuwa ni msaada mkubwa kwa wananchi wengi wa kawaida na umeendelea kuongeza kasi yaw ukuaji wa uchumi wa wananchi wa Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.

Awali niliwahi kusema na pongezi serikali kwa uamuzi wake wa kuanzisha mfumo wa malipo wa serikali wa kieletroniki - GePG (Government electronic Payment Gateway system) wakati wa uzinduzi pale Kijitonyama, lakini nikatahadharisha baadhi ya changamoto na hujuma watakazokutana nazo pindi Utekelezaji wake utakapoanza kwa sababu mafisadi yaliyokuwa yanaiibia serikali hayatakubali kirahisi kuruhusu hili litokee.

Kinachoendelea pale UDART ni mwanzo wa hujuma zinazosababishwa na kuanzishwa mfumo huu ambao sasa umefinya na kuziba mianya ya kuendelea kuiibia serikali yetu.

Hujuma ndani ya UDART inafanywa na taasisi/watu/makundi kama manne. Leo nitaanza na hawa waliokuwa wanakusanya fedha kwa niaba ya UDART, mosi hii taasisi imekuwa ikiibia sana serikali yetu kupitia uwakala wa ukusanyaji wa mapato ya taasisi mbalimbali za umma lakini kwenye hili la UDART wameamua kufanya hujuma baada ya kujua kwamba sasa ni lazima mfumo mpya wa GePG utumike.

Wanahujumu UDART kwa kuanzisha na kuchochea migogoro ya wafanyakazi, hawa wazabuni wa kukusanya malipo ndio wamekuwa ma_mastermind kwa kuonesha Udart imeshindwa kuendesha mradi ambapo kimsingi mradi umeendelea kuwa imara pamoja na changamoto za mafuriko ambayo yameikumba zaidi ya mara nne.

Hawa wazabuni ndio waliandaa mgomo wa wale wakatisha ticket kwa kuwaambia kwamba mfumo mpya ukija basi na wao watakosa kazi wakati jambo kama hilo linazungumzika na Udart naamini ilikuwa tayari na mipango kabambe ya kuangalia namna ya kuwa_accomodate watumishi wale.

Rai yangu ni kuiomba tena serikali yetu sikivu, kupitia vyombo vyake mbalimbali vya ulinzi na usalama na wawaangalie kwa umakini sana hawa wazabuni / wakala wa kukusanya malipo wa UDART na hujuma zao mbalimbali.
 
Watu wenye mawazo ya "KIJIMA"kama huyu mleta mada ndio wanavuruga uchumi wetu na kuua sekta Binafsi! Akili za kipumbavu zinazotegemea ajira ya kuajiriwa ama teuzi utazijua tu! Mtu ameokotwa kwenye "Slaves Market "sorry wao wanapenda kudanganywa eti "Labour Market" anajifanya kujua biashara na uchumi! Popote Duniani kuna "Ma-Agent"kwenye business! Mtu useless anataka kujifananisha na akina Juma Rajabu wa Maxcom.
 
Kila kitu kipya lazima kije na changamoto zake,GePG kwenye UDARt ilikurupuka sana,mbona kwenye umeme mambo MSWANO?
 
Watu wenye mawazo ya "KIJIMA"kama huyu mleta mada ndio wanavuruga uchumi wetu na kuua sekta Binafsi! Akili za kipumbavu zinazotegemea ajira ya kuajiriwa ama teuzi utazijua tu! Mtu ameokotwa kwenye "Slaves Market "sorry wao wanapenda kudanganywa eti "Labour Market" anajifanya kujua biashara na uchumi! Popote Duniani kuna "Ma-Agent"kwenye business! Mtu useless anataka kujifananisha na akina Juma Rajabu wa Maxcom.
fumadilu naona unakurupuka elewa mada uzi vizuri tuendeleee kwa sasa huu mradu nautabibilia mafanikio kwan pesa itakua salama muda wote hao maxcome wakafanya shuhul ingine sio waaminifu awamu hii serikali ipo maikin sana.
 
Takribani sasa ni zaidi ya wiki tatu nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu sana sakata na kile kinachotaka kionekana kana kwamba kuna mgogoro ama mkwamo wa uendeshaji wa mradi wa basi yaendayo kasi "UDART" ambayo kimsingi huduma hii imeendelea kuwa ni msaada mkubwa kwa wananchi wengi wa kawaida na umeendelea kuongeza kasi yaw ukuaji wa uchumi wa wananchi wa Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.

Awali niliwahi kusema na pongezi serikali kwa uamuzi wake wa kuanzisha mfumo wa malipo wa serikali wa kieletroniki - GePG (Government electronic Payment Gateway system) wakati wa uzinduzi pale Kijitonyama, lakini nikatahadharisha baadhi ya changamoto na hujuma watakazokutana nazo pindi Utekelezaji wake utakapoanza kwa sababu mafisadi yaliyokuwa yanaiibia serikali hayatakubali kirahisi kuruhusu hili litokee.

Kinachoendelea pale UDART ni mwanzo wa hujuma zinazosababishwa na kuanzishwa mfumo huu ambao sasa umefinya na kuziba mianya ya kuendelea kuiibia serikali yetu.

Hujuma ndani ya UDART inafanywa na taasisi/watu/makundi kama manne. Leo nitaanza na hawa waliokuwa wanakusanya fedha kwa niaba ya UDART, mosi hii taasisi imekuwa ikiibia sana serikali yetu kupitia uwakala wa ukusanyaji wa mapato ya taasisi mbalimbali za umma lakini kwenye hili la UDART wameamua kufanya hujuma baada ya kujua kwamba sasa ni lazima mfumo mpya wa GePG utumike.

Wanahujumu UDART kwa kuanzisha na kuchochea migogoro ya wafanyakazi, hawa wazabuni wa kukusanya malipo ndio wamekuwa ma_mastermind kwa kuonesha Udart imeshindwa kuendesha mradi ambapo kimsingi mradi umeendelea kuwa imara pamoja na changamoto za mafuriko ambayo yameikumba zaidi ya mara nne.

Hawa wazabuni ndio waliandaa mgomo wa wale wakatisha ticket kwa kuwaambia kwamba mfumo mpya ukija basi na wao watakosa kazi wakati jambo kama hilo linazungumzika na Udart naamini ilikuwa tayari na mipango kabambe ya kuangalia namna ya kuwa_accomodate watumishi wale.

Rai yangu ni kuiomba tena serikali yetu sikivu, kupitia vyombo vyake mbalimbali vya ulinzi na usalama na wawaangalie kwa umakini sana hawa wazabuni / wakala wa kukusanya malipo wa UDART na hujuma zao mbalimbali.
Weka picha ya huo Uhujumu tuhakikishe
 
Tuhuma zako zina ushahidi wowote? Au pengine ni hisia zako kama sio 'wivu wa kike'?
 
Tuhuma zako zina ushahidi wowote? Au pengine ni hisia zako kama sio 'wivu wa kike'
jambo ilo lipo wazi walizoea awamu ya nne nw wamegonga jiwe na hujuma zao ndani ya mradi unahohusisha serikali
 
Mada kama hii yenye tuhuma nzito kiasi hiki inatakiwa kuwa na vithibitisho, ukiandika mada kama hii bila uthibitisho wa hoja zako utaitwa mchochezi, mnafiki etc.

Yapo makundi manne, umeanza na Maxcom, leta uthibitisho ni kwa vipi wanahujumu na kulumbanisha UDART na wafanyakazi wake. Kwa sisi ambao hatuhusiki huko, tunaona UDART inafeli kwa sababu haitoi huduma stahiki, usipokuja na uthibitisho wa hizo allegations tunakuona mchochezi tu.
 
Mada kama hii yenye tuhuma nzito kiasi hiki inatakiwa kuwa na vithibitisho, ukiandika mada kama hii bila uthibitisho wa hoja zako utaitwa mchochezi, mnafiki etc.

Yapo makundi manne, umeanza na Maxcom, leta uthibitisho ni kwa vipi wanahujumu na kulumbanisha UDART na wafanyakazi wake. Kwa sisi ambao hatuhusiki huko, tunaona UDART inafeli kwa sababu haitoi huduma stahiki, usipokuja na uthibitisho wa hizo allegations tunakuona mchochezi tu.
usiwe na haraka huu ndio wakati mwafaka wa kujulikana madudu yao
 
Hongera kwa kufuatilia kwa karibu, Nakushauri ufuatilie zaidi uje na details za kutosha.

Abiria/ wananchi wanahitaji taarifa za kutosha kujua nini tatizo na wataondokana vipi na kero zilizopo kwenye UDART
 
Hongera kwa kufuatilia kwa karibu, Nakushauri ufuatilie zaidi uje na details za kutosha.

Abiria/ wananchi wanahitaji taarifa za kutosha kujua nini tatizo na wataondokana vipi na kero zilizopo kwenye UDART
asante mkuu kila kitu kitakwenda sawa ishala!
 
Watu wenye mawazo ya "KIJIMA"kama huyu mleta mada ndio wanavuruga uchumi wetu na kuua sekta Binafsi! Akili za kipumbavu zinazotegemea ajira ya kuajiriwa ama teuzi utazijua tu! Mtu ameokotwa kwenye "Slaves Market "sorry wao wanapenda kudanganywa eti "Labour Market" anajifanya kujua biashara na uchumi! Popote Duniani kuna "Ma-Agent"kwenye business! Mtu useless anataka kujifananisha na akina Juma Rajabu wa Maxcom.
Wewe ni mjinga nambari moja
 
Pia sidhani kama mtandao wa serikali ndiyo utakuwa suluhu. Hiyo ni kazi ya private sector. Serikali ikusanye pesa zake tu na sio kuingiza private sector kwake.

Siku mambo yakikwama mtakuja kuona shida yake. Nashangaa uchumi unakuwa lkn service provider wamakuwa centrallized hii sio dalili nzuri. Tunahitaji akina max malipo wengi tanzania ili kuleta ushindani na sio kuua hata kamoja kalikopo

Mwendo kasi umeachwa wenyewe tiyari majibu tumeyaona. Tunafanya makosa tena kwenye mfukoni ya jamii ambapo inaunganishwa baadala ya kuacha ishindane . Na tunaona serikali inajipanda kutoa huduma kila mahali. Jambo hili sio nzuri acheni private sector iongoze uchumi
 
Hongera kwa kufuatilia kwa karibu, Nakushauri ufuatilie zaidi uje na details za kutosha.

Abiria/ wananchi wanahitaji taarifa za kutosha kujua nini tatizo na wataondokana vipi na kero zilizopo kwenye UDART
asante mkuu kila kitu kitakwenda sawa ishala!
 
Umeongelea vyoote hivyo ila hujagusia malipo/maslahi kwa wafaanyakazi wa huo mradi ambacho ndo kiini cha mgomo.
 
Yaani ulipoandika tu "hii serikali ni sikivu" ndo nikagundua moja kwa moja kuwa na wewe ni miongoni mwa wale wanaoimba mapambio ya sifa ili angalau mpate uteuzi.
Hii serikali ni sikivu kwa lipi hasa?
 
maxcom wametumika vibaya sana awamu ya msoga awamu hii hakuna wakuhujumu uchumi uwizi niwatakie ukusanyaji mzuri serikali kodi zetu ziendelee kua mikono salama
 
Maxmalipo hawapo huu mradi toka mwezi wa sita, ila mauza uza bado yapo kibao. Hivyo ni wazi wababaishaji wakuu ni udart.
 
Back
Top Bottom