Mawazo ya biashara za mitaji midogo rahisi kwa wafanyakazi kuzifanya

ndege JOHN

JF-Expert Member
Aug 5, 2015
19,579
44,825
Wafanyakazi tumenongwa sana tuache kutegemea single source, yaani hela za makazini tujiongeze kidogo na shughuli nyingine. Yaani kweli mtumishi inafika tarehe mshahara hujatoka unakosa hata 5000 aisee hii sio sawa kabisa kwanza yafaa katika account yako pasikose million 1 walau kidogo ili ikitokea hata dharura fasta unaisolve japo pesa ya kijinga sana sijui kwanini haitaki kukaa mfukoni.

Sasa mimi nimekuja na products ambazo ni rahisi kuzitengeneza hata ukiamua umetoka zako kazini ukiwa nyumbani unazitengeneza kisha unazisambaza madukani mnakubaliana na mwenye duka jinsi mtakavyogawana pesa na hasa bidhaa nzuri ni zile ambazo hata zikikaa muda mrefu dukani haziharibiki.

1. Juice za matunda: Hizi usiku unatengeneza hata lita tatu tu unaziweka kwenye friji asubuhi unampelekea mtu dukani unampa na vi take away, atleast hata akipata faida ya Tsh. 5,000/- mpe hata Tsh. 2,000/- utakuwa hujapoteza kitu kwa mwezi hukosi Tsh. 90,000/-.

2. Karanga za kukaanga: Hizi ni dakika chache unakaanga na kuzifunga katika packages unasambaza maduka yasikuwa nazo, hata ukipata faida ya Tsh. 20,000/- kwa mwezi ni safi kabisa.

3. Visheti na kashata: Hivi ni kama karanga tu, hata ukipata faida ya Tsh. 7,000/- kwa mwezi sio mbaya.

4. Icecream na ubuyu: Hii ukimpata dogo mmoja akawa anawauzia wanafunzi shuleni si ajabu ukapata faida mpaka ya Tsh. 25,000/-.

5. JIK: hizi unanunua bei ya jumla Dar unazipack kwenye vichupa unauza hata maofisini kwenu, sio mbaya ukipata hata faida ya Tsh. 10,000/- kwa mwezi.

6. Showergel, sabuni za kipande, sabuni za maji, za unga: Zote hizi ukiamua kuacha usingizi mmoja tu usiku unatengeneza na usazambaza sample chache.

7. Ufugaji wa kuku wa mayai wa kienyeji: Wasiwe wengi, hata wakiwa watano tu makoo inatosha, ukipata mayai 20 kila mwezi ukayauza umepata sio mbaya.

8. Asali: Ukinunua dumu ukaja kufungasha unapeleka maduka tofauti tofauti hata sample 5 tu kila duka.

Kikubwa ndugu zangu maisha yanazidi kuwa magumu, tujifunze kupunguza matumizi. Vitu vingine tunajikuta tunanunua halafu hata hatuvitumii kivile mfano nguo, viatu n.k.

Tuongezee na idea nyingine wadau ambazo rahisi kuzitengeneza, yaani hazili muda sana lakini pia rahisi kuzifungasha, na pia haziharibiki hata zikikaa muda mrefu dukani.
 
Wafanyakazi tumenongwa sana tuache kutegemea single source yaani hela za makazini tujiongeze kidogo na shughuli nyingine.yaani kweli mtumishi inafika tarehe mshahara hujatoka unakosa hata 5000 aisee hii sio sawa kabisa kwanza yafaa katika account yako pasikose million 1 walau kidogo ili ikitokea hata dharura fasta unaisolve japo pesa ya kijinga sana sijui kwanini haitaki kukaa mfukoni.

Sasa mimi nimekuja na products ambazo ni rahisi kuzitengeneza hata ukiamua umetoka zako kazini ukiwa nyumbani unazitengeneza kisha unazisambaza madukani mnakubaliana na mwenye duka jinsi mtakavyogawana pesa na hasa bidhaa nzuri ni zile ambazo hata zikikaa muda mrefu dukani haziharibiki.


1.juice za matunda hizi usiku unatengeneza hata lita tatu tu unaziweka kwemye friji asubuhi unampelekea mtu dukani unampa na vi take away atleast hata akipata faida ya 5000 mpe hata 2000 utakuwa hujapoteza kitu kwa mwezi hukosi 90000

2.karanga za kukaanga hizi ni dakika chache unakaanga na kuzifunga katika packages unasambaza maduka yasikuwa nazo.hata ukipata faida ya 20000 kwa mwezi ni safi kbs.

3.visheti na kashata hivi ni kama vikaranga tu hata ukipata faida ya 7000 kwa mwezi sio mbaya

4.icecream na ubuyu hii ukimpata dogo mmoja akawa anawauzia wanafunzi shuleni si ajabu ukapata faida mpaka ya 25000

5.JIK hizi unanunua bei ya jumla dar unazipack kwenye vichupa unauza hata maofisini kwenu sio mbaya ukipata hata faida ya 10000 kwa mwezi

6.SHOWERGEL,sabuni za kipande sabuni za maji,za unga zote hizi ukiamua kuacha usingizi mmoja tu usiku unatengeneza na usazambaza sample chache.




Kikubwa ndugu zangu maisha yanazidi kuwa magumu tujifunze kupunguza matumizi vitu vingine tunajikuta tunanunua halafu hata hatuvitumii kivile mfano nguo,viatu n.k

Tuongezee na idea nyingine wadau
Wote tukifanya hivo wateja wa tatoka wapi?........tatizo la watumishi wengi ni poor spending habit or lack of financial literacy, mtu anapokea 1.3m, lakini kati kati ya mwezi pesa imeisha loh.
 
Wote tukifanya hivo wateja wa tatoka wapi?........tatizo la watumishi wengi ni poor spending habit or lack of financial literacy, mtu anapokea 1.3m, lakini kati kati ya mwezi pesa imeisha loh.
Mkuu uko sahihi kweli watumishi tunafanya overspending sana ila pia ndo inasaidia mzunguko kuweko mtaani assume tumebana hela tunachomoa bukubuku tu ya mboga je wenye bar na wauzaji wao wataishi vipi..hahahaha

Tukija kwenye ujasiriamali mkuu serikali yenyewe inasisitiza soko lipo la uhakika kwamba tufanye sana issue za uzalishaji.halafu pia huu ushauri nimelenga kwa wana jf pekee na bado sio wote wataufuata haohao wachache wafaidike
 
Mkuu uko sahihi kweli watumishi tunafanya overspending sana ila pia ndo inasaidia mzunguko kuweko mtaani assume tumebana hela tunachomoa bukubuku tu ya mboga je wenye bar na wauzaji wao wataishi vipi..hahahaha

Tukija kwenye ujasiriamali mkuu serikali yenyewe inasisitiza soko lipo la uhakika kwamba tufanye sana issue za uzalishaji.halafu pia huu ushauri nimelenga kwa wana jf pekee na bado sio wote wataufuata haohao wachache wafaidike
Mkuu katika uchumi illogical spending haileti high circulation of money kwenye economy ila inasababisha increase in income inequality btn poor and Rich how? ni somo lefu
 
Bila kuuza ngada bmw tutazisikia tu! Kuna namna lazima tuishike serikali masikio na macho!, magendo na ukwepaji Kodi ni dhambi lakini ni mafanikio yakiwa upande wako!.. mtaji wa 30000 huo wakuuza juice unaisha kwa simu Moja tu toka kijijini ukiambiwa bibi kameza chemli!
 
Mkuu katika uchumi illogical spending haileti high circulation of money kwenye economy ila inasababisha increase in income inequality btn poor and Rich how? ni somo lefu
Kama nakupata hivi yaani kifupi kwa mfano tunazidi kuwa masikini huku maboss wa konyagi na tbl wakiendelea kuona mabillion yanavyoingia...aisee kuanzia leo hawanipati tena
 
Bila kuuza ngada bmw tutazisikia tu! Kuna namna lazima tuishike serikali masikio na macho!, magendo na ukwepaji Kodi ni dhambi lakini ni mafanikio yakiwa upande wako!.. mtaji wa 30000 huo wakuuza juice unaisha kwa simu Moja tu toka kijijini ukiambiwa bibi kameza chemli!
Hahahahahahah mkuu umeua...yaani unapambana kutolala usiku then kweli unefanikiwa kupata faida ya ka 70000 kisha ghafla unakuja mchango wa kifamilia rambirambi ama dada yako anaolewa na ni shughuli ya kijamii Huna jinsi
 
Bila kuuza ngada bmw tutazisikia tu! Kuna namna lazima tuishike serikali masikio na macho!, magendo na ukwepaji Kodi ni dhambi lakini ni mafanikio yakiwa upande wako!.. mtaji wa 30000 huo wakuuza juice unaisha kwa simu Moja tu toka kijijini ukiambiwa bibi kameza chemli!
Ujinga wa hela unapenda kweli point ya kutorokea yaani me naona labda uwe na kibubu ambacho huwezi kabisa kukifungua uwe unatupia vi coin coin hivi utakifungua baada ya miezi sita kucheki ulichopata...unajua kuna ka feeling fulani unakuwa nacho na unajiamini ukiombwa hela na Huna.. jibu ni simple sina ila ukiwa nazo asee roho inakusuta unafikiria jinsi mlivyokula pilau na nyama na ndugu zako enzi hizo leo kweli wewe ndo wakuwanyima 50000??????hahahah
 
Kama nakupata hivi yaani kifupi kwa mfano tunazidi kuwa masikini huku maboss wa konyagi na tbl wakiendelea kuona mabillion yanavyoingia...aisee kuanzia leo hawanipati tena
Naona umesha nielewa kabisa, na wanapo pata pesa nyingi hao maboss wa bar hotel na guest wana itunza haingii kwenye circulation au wananunua vitu luxrious vya kutoka nje ya nchi au kujenga majumba ya kifahari inao wafaidi tu wao.
 
Naona umesha nielewa kabisa, na wanapo pata pesa nyingi hao maboss wa bar hotel na guest wana itunza haingii kwenye circulation au wananunua vitu luxrious vya kutoka nje ya nchi au kujenga majumba ya kifahari inao wafaidi tu wao.
Sasa covax imagine watumishi tugomee kufanya spending yaani means tutembee na miguu badala ya bodaboda,tu stop pombe na ku bet..ndani ya mwezi tu kweli maisha yatasonga kweli maana wafanyabiashara ni wagumu kutumia pesa. .hawa wa sekta zisizo rasmi watapataje pesa si watazidi kukata tamaa kabisa
 
Sasa covax imagine watumishi tugomee kufanya spending yaani means tutembee na miguu badala ya bodaboda,tu stop pombe na ku bet..ndani ya mwezi tu kweli maisha yatasonga kweli maana wafanyabiashara ni wagumu kutumia pesa. .hawa wa sekta zisizo rasmi watapataje pesa si watazidi kukata tamaa kabisa
Hamna tutumie pesa kwenye basic needs apropriately kama food (corn milk meat fruits) clothing, public transport, medications and tuition fees......kwa kutumia hivo pesa itafika kwenye sector zote za uchumi na kila biashara itakua na mzunguko, investors wata invest in basic need bussiness kwa sabb ndo zitakua na wateja, kuliko kukuta mta moja una guest na bar zaidi ya 10, ila hamna day care centre au nursary school au dispensary kwasbb poor priortising of preferences kwa watumishi wa ummah.
 
Hamna tutumie pesa kwenye basic needs apropriately kama food (corn milk meat fruits) clothing, public transport, medications and tuition fees......kwa kutumia hivo pesa itafika kwenye sector zote za uchumi na kila biashara itakua na mzunguko, investors wata invest in basic need bussiness kwa sabb ndo zitakua na wateja, kuliko kukuta mta moja una guest na bar zaidi ya 10, ila hamna day care centre au nursary school au dispensary kwasbb poor priortising of preferences kwa watumishi wa ummah.
Shukrani mkuu umenifungua akili leo
 
Wote tukifanya hivo wateja wa tatoka wapi?........tatizo la watumishi wengi ni poor spending habit or lack of financial literacy, mtu anapokea 1.3m, lakini kati kati ya mwezi pesa imeisha loh.
Ni watumishi wachache sana wanaopokea hiyo 1.3m per month, iwe basic au take home. Fuatilia rates especially serikalini ambako ndiko kuna waajiriwa wengi utarudi hapa kushuhudia.

Mtoa mada yuko sahihi. Tatizo la watumishi wengi ni kuwa na chanzo kimoja cha mapato, ambacho ni mshahara.
 
Ni watumishi wachache sana wanaopokea hiyo 1.3m per month, iwe basic au take home. Fuatilia rates especially serikalini ambako ndiko kuna waajiriwa wengi utarudi hapa kushuhudia.

Mtoa mada yuko sahihi. Tatizo la watumishi wengi ni kuwa na chanzo kimoja cha mapato, ambacho ni mshahara.
Kweli mkuu plus mamikopo haya wengi sana tunachezea 300000-600000
Ambazo hazitoshi ukisema una watoto unasomesha ada hizi za million lazima uwe na source nyingine ya kukuwezesha kula tu ili hizi nyingine laki sita uziweke na ada
 
Aisee inafikirisha Sana HONGERA ila jaribu kukopa na kufungua baishara ya kubwa ambayo itahesabika Kama side hustle Kama bar , au duka zuri la matumizi n.k
 
Back
Top Bottom