Mawazo ya biashara kianzio chini ya shilingi 500,000/=

Mtu Poa 2013

Member
Mar 26, 2013
86
45
Habari zenu

Kuna watu wamekuwa wakiniulizia ideas za biashara lakini wakiwa na mitaji midogo chini ya 500,000 sasa nimeona ni share ideas chache nilizonazo ili vijana wengi waweze kujiajiri na kupunguza uhalifu mitaani.

1. Kutengeneza mishumaa - mashine sido sh. 350,000/=
2. Mama lishe ya kisasa - sido wana masufuria mazuri ya kisasa 90,000/=
3. Kufyatua matofali - mashine zinaanzia 150,000 - 450,000

Kwa watu wengine wenye ideas, msisite ku share nasi.

Asanteni
 
si useme tu unaipigia upatu SIDO.

Anyway acha nikusapoti mkuu, other ajira ni kama ifuatavyo;

1. Kumpokea Eddo airport ya kisongo na kuandamana naye hadi A. town (10000 kwa trip)

2. Kupost thread za kuiponda CDM kwenye mitandao ya jamii (5000 kwa thread ilokomentiwa na at least 20 people)

3. Kurekodi chochote unachozungumza na kiongozi wa upinzani (50000 per clip)
 
si useme tu unaipigia upatu SIDO.

Anyway acha nikusapoti mkuu, other ajira ni kama ifuatavyo;

1. Kumpokea Eddo airport ya kisongo na kuandamana naye hadi A. town (10000 kwa trip)

2. Kupost thread za kuiponda CDM kwenye mitandao ya jamii (5000 kwa thread ilokomentiwa na at least 20 people)

3. Kurekodi chochote unachozungumza na kiongozi wa upinzani (50000 per clip)

Lame! Ndo maana watanzania hatuendeleagi. Yaani mwenzio kaanzisha thread kusaidia wenzake, wewe unaweka utani ambao hata hauchekeshi! Aisee!
 
Nunua camera ya picha 450,000 then sajili blog then ingia mtaani na jichanganye kwenye matukio, piga picha na weka kwenye blog yako. Sasa kwasababu blogs za aina hii ziko nyingi bongo, wewe fikiria ni content za aina gani utaweza ili kujitofautisha na hao wengine.
 
Si dhani kama tuna jua Mahara ya Aidea za Kupewa, nazani tunajua Faida tu ila mahara hatujui, The best Aidea ni ile unayo develop wewe mwenyewe,
 
Si dhani kama tuna jua Mahara ya Aidea za Kupewa, nazani tunajua Faida tu ila mahara hatujui, The best Aidea ni ile unayo develop wewe mwenyewe,
Ni kweli...lakini unaposikia idea nzuri na kwa mtazamo wako unaona unaweza kuifanya we ifanye ila ifanye katika ubunfu zaidi ya orgnal idea cz somtyms kuna wa2 wanaothnk of good ideas za biashara lakin ni wazto au sio doers..lakin kuna wale wanaochukua ideas za wa2 wengne na kuzboresha na kutoa ktu kizuri.....sometimes with a little bt of creativity that old or someone else idea will give you millions,tusiogope jaman kujaribu.
 
Nunua camera ya picha 450,000 then sajili blog then ingia mtaani na jichanganye kwenye matukio, piga picha na weka kwenye blog yako. Sasa kwasababu blogs za aina hii ziko nyingi bongo, wewe fikiria ni content za aina gani utaweza ili kujitofautisha na hao wengine.
Wazo zuri...
 
1 - Kuwa wakala wa pesa wa mitandao ya simu, kama wale wanaokaa vituo vya mabasi na miamvuli wakiuza vocha, line za simu, na kutoa huduma za kutoa pesa, kuweka pesa nk. Mtaji wao hata laki 3 haufiki na baada ya muda wanatoka.
2 - nenda kwenye minada ya kuuza nguo kwa bei nafuu kisha uuze kwa wafanyakazi maofisini na walio ktk biashara zao. Mfano kwa Dar Es Salaam, nenda pale shule ya uhuru na ilala boma sokoni alfajiri utapata nguo za ukweli kwa bei nafuu sana kisha ukawauzia masistaduu na mabrazamen, wadada na wakaka walio maofisini na walio ktk biashara zao ambao wengi wao hukosa muda wa kwenda kununua nguo kutokana na ubize. (suruali, mashati, sketi, suruali, skafu na mashati ya kike na blauzi hulipa sana)
 
balo zuri la mtumba ni 250000, hapo unayo mawili tayari. kila balo kwenye mnada faida ni 15000 hadi 30000. kazi ni kwako. mia
 
asanteni nimependa hzo za mitumba ,pia asante kwa wazo la sido kweli nashida na mashine ya kusaga nyama hasa za kutengenezea sambusa ntawacheki labda ntapata
 
asanteni nimependa hzo za mitumba ,pia asante kwa wazo la sido kweli nashida na mashine ya kusaga nyama hasa za kutengenezea sambusa ntawacheki labda ntapata

Aisee sido wana mashine za kila aina, kama uko dar wazukie kulee vingunguti ujionee mashine
 
Back
Top Bottom