Mawaziri wanaongoza kwa wizi serikalini - Deo Filikunjombe

Filikunjombe kausema ukweli ambao wote hapo mjengoni wanaujua...Mashujaa kama Deo wamechoshwa na serikali yao isiyo na haya kwa walipa kodi wake
Deo Filikunjombe ana machungu ya kweli kwa sababu juhudi za kuyatetea magamba zimemfedhesha. Si mnakumbuka mangumi aliyokungutwa na wapigania uhuru wa BAWACHA kwenye viwanja vya bunge? Deo BAWACHA walikuwa wamesha ishitukia serikali yenu tangu siku nyiiingi!!!!
 
Namfahamu sana huyu mnyalukolo Fili lazima ana ushahidi wa kutosha. Istoshe wapo watu wakubwa serikalini nyuma yake wanaompa takwimu hizo achilia mbali yeye kuwa TISS
 
Muhimu ni kama anayo hiyo orodha na akaiwasilisha panapohusika litakuwa jambo la kheri hata kama magazeti yatauza.

Mimi ningetegemea awataje moja kwa moja ili kuepuka kuchakachua taarifa yake, ofisi ya spika haiaminiki sana kwa masuala serious and sensitive.

Hayo mambo ya kuwataka wabunge wapeleke uthibitisho wala hayana maana kwani wakiona wataumbuka taarifa inaishia kwa madame speaker kimya kimya. Lukuvi mjanja anatumia hiyo mbinu ili mbunge asiendelee kuongea asije akatamka hadharani.
 
Nilishamwona muda mrefu huyu Kijana Filikunjombe uwezo wake, uchungu kwa wapiga kura wake na kwa taifa. Hapa JF mmenishambulia kwa sana tu kuhusu mbunge huyu, na leo wenyewe mnaona alivyo mtetezi mkubwa ndani ya bunge bila kujali itikadi za kichama.

Juzi tu nilifanya utalii Mkoa mpya wa Njombe, tofauti ya majimbo ya uchaguzi yanayoongozwa na wabunge wa CCM Njombe Kusini la Spika Anna makinda na la Ludewa la Filikunjombe utaona tofauti kubwa. Kijana kaanza juzi tu barabara zinaakisi kushughulikiwa tofauti na kwa Makinda. Stand ya mabasi Njombe ikinyesha mvua ni matope na kukiwa Jua ni jangwa la vumbi unatakiwa vaa kitambaa na maski vinginevyo mafua yatakuanzia hapo hapo uwanjani.

Tuachane na ushabiki, Kijana Filikunjombe yuko Mtanzania halisi asiye mbinafsi na mwoga na anayejali utaifa na ni mzalendo wa kweli. Hawa ndio tunaowataka na kesho wakiamua kujing'oa CCM na kujiunga na kambi ya akina Tundu Lisu, ndo kasi ya maendeleo ya nchi yetu itakavyopiku mataifa yote ya afrika mashariki.
 
Mwenyewe (Deo) kasema ushahidi upo na wakitaka atawapa. Akitoa ushahidi najua mwaka huu concussion itaua wengi lol
 
Huo ni ukweli ulio wazi cjui kwa nn wananyamaziana mjengoni labda wawakilishi wameenda kuwakilisha matumbo yao na sio matatizo ya watanzania.
 
Mwenyewe (Deo) kasema ushahidi upo na wakitaka atawapa. Akitoa ushahidi najua mwaka huu concussion itaua wengi lol

FILIKUNJOMBE awasiliane na Wabunge wa Chadema watamsaidia orodha ya mawaziri wala rushwa, lini, saa dakika na mazingira waliyofanya uuaji huo watamdsaidia sana. Pia awe shujaa ikiwezekana kama noma na iwe noma ahamie CDM cccmmm wasimbabaishe wanakumbatia wezi halafu wanakutishia kukuvua uanachama/ubunge. MAKAMANDA MLIOPO DODOMA BUNGENI MPENI MOYO HUYO NI KAMANDA MWENZETU SEMA HAJAJIUNGA NASI BADO
 
Sio mawaziri, rais ndiye anayeongoza kwa kuibaka nchi na safari zake nyiiiingiiii zisizo na maana yoyote. Kaenda Brazil kumsalimia rais mstaafu Lula na kupewa jezi na Maximo, rais anachemka sijaona!
Hizi safari zina tija gani? Kwa nini serikali haitaki kutupa mchanganuo wa gharama zote za safari tangu Dec. 2005 alipoingia Magogoni mpaka sasa na tulichokipata kutokana na hizi safari ili tujue kama ni kweli anakwenda kutalii tu au la?!
Mbona naye hatembelewi kama anavyowatembelea? Sanasana amekuja Waziri Mkuu wa Somalia tena kwa masaa tu na kuondoka zake!
Kama baba anafuja unategemea watoto wafanye nini?

Sio hivyo tu kampeleka......kutibiwa uzee India. Pia na katoto kakipeleka.........ameteguka mkono. Hao wote wapo katika familia yake. Nilikuwa nasikiliza hotuba yake moja alipotembelea wizara ya maliasili alisema hakuna mbuga ya wanyama hapa nchini ambayo hajatembelea- ni vizuri kwa utalii wa ndani. Nahisi anataka kusema baadae kuwa hakuna nchi ambayo hajatembelea katika maisha yake. Masuala ya biashara Brazil angeenda waziri husika ila mimi nahisi anaenda kumtafuta mtu atakayejifanya anakuja kuwekeza lakini kwa mgongo wake (akiwa na share nae).
 
Nchi inawahitaji viongozi vijana ili kuleta ukombozi wa kweli, CCM wamebakia kutuibia tu ili wanufaike baada ya kupigwa chini.
 
Yaani hakuna kazi rahisi tanzania kama kuthibitisha viongozi wezi.

Filikunjombe kama upo jf nipm nikupe data.
 
Hizi ngonjera zao za kulithibitishia bunge zimeshapitwa na wakati na zinazidi kutuchosha kwan serikali inatumia mwanya huo kama mwamvuli wao wa kujikinga na mvua ya gadhabu ya wananchi. Dawa ya vithibitisho kama hivi ni kuvileta kwenye BUUNGE LA WANANCHI, wengine wanaita mahakama ya wananchi, ili wenyewe waamue kitu cha kufanya, kwani huku miongozo yao na zaratibu zao za kubunge na kiserikali hazitumiki bali sheria zetu na taratibu zetu za wananchi, tunazozijua wenyewe.

Ndugu zangu wana JF, hebu tujikumbushe kidogo,
ZITTO alipolithibitishia Bunge juu ya ufisadi na ukiukwaji mkubwa wa taratibu katika mkataba wa BUZWAGI nini kilitokea? Alifukuzwa Bungeni.
LEMA alipolithibitishia bunge kuwa waziri mkuu, amedanganya juu ya MAUAJI ya Januari 05 huko Arusha, nini kilitokea? Wamekalia uthibitisho
DR. SLAA, alipowathibitishia wananchi juu ya ufisadi mkuu ( EPA, MEREMETA, KIWIRA ...) katika nchi yetu katika viwanja vya mwembeyanga na kuzaa LIST OF SHAME nini kilitokea?...
DEO FILIKUNJOMBE, nakushauri, hivyo vithibitisho vilete kwa wananchi, ili waamua walitakalo
 
Back
Top Bottom