Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Mawaziri wa Ulinzi na Mazingira wa Ghana wamefariki katika ajali ya Helikopta ya Kijeshi katika eneo la kati la Ashanti, pamoja na watu wengine sita.
Mkuu wa Majeshi Julius Debrah aliuambia mkutano na Waandishi wa habari kwamba Waziri wa Ulinzi Edward Omane Boamah na Waziri wa Mazingira, Sayansi na Teknolojia Ibrahim Murtala Muhammed (50), waliuawa katika ajali hiyo, ambayo aliitaja kuwa janga la kitaifa.
Ilikuwa imeondoka katika mji mkuu, Accra, saa 09:12 kwa saa za huko (na GMT) na ilikuwa inaelekea katika mji wa uchimbaji dhahabu wa Obuasi.
Mamlaka haijathibitisha chanzo cha ajali hiyo.Mkuu wa Majeshi ameagiza Bendera za nchi kupepea nusu mlingoti.
Naibu Mratibu wa Usalama wa Kitaifa wa Ghana na Waziri wa zamani wa Kilimo Alhaji Muniru Mohammed pia alikuwa miongoni mwa waliofariki, pamoja na Samuel Sarpong, Makamu Mwenyekiti wa Chama tawala cha National Democratic Congress.
Mkuu wa Majeshi Julius Debrah aliuambia mkutano na Waandishi wa habari kwamba Waziri wa Ulinzi Edward Omane Boamah na Waziri wa Mazingira, Sayansi na Teknolojia Ibrahim Murtala Muhammed (50), waliuawa katika ajali hiyo, ambayo aliitaja kuwa janga la kitaifa.
Ilikuwa imeondoka katika mji mkuu, Accra, saa 09:12 kwa saa za huko (na GMT) na ilikuwa inaelekea katika mji wa uchimbaji dhahabu wa Obuasi.
Mamlaka haijathibitisha chanzo cha ajali hiyo.Mkuu wa Majeshi ameagiza Bendera za nchi kupepea nusu mlingoti.
Naibu Mratibu wa Usalama wa Kitaifa wa Ghana na Waziri wa zamani wa Kilimo Alhaji Muniru Mohammed pia alikuwa miongoni mwa waliofariki, pamoja na Samuel Sarpong, Makamu Mwenyekiti wa Chama tawala cha National Democratic Congress.