Tetesi: Mawaziri wa Kikwete: Lazaro Nyalandu, na Jumba la karibu milioni 600 Arusha!

Acheni wivu wakipuuzi..fanya kaz kwa bidii sio kuanzisha uzi wa kumuonea gere aliyepata.baba yako angepata nafas angetumia pia vizur na usingekua hapa unaandika vitu vya wenzio bila udhibitisho.

Fight with your condition..
:D:D:D:D:D:D:D
 
Wapmb-- nyie lazaro kumtembelea lissu imekuwa shidaaaa .....andikeni khsu jaji mkuu mstaafu piaaa

Ova
Mkuu huu uzi ni wa 2012 na uliwekwa na mwana chadema mwenzako. Sasa kwa kuwa amepiga picha na ndg zako ndiyo maana unatoa mapovu!! Chagadema ni shidaaaa!!
 
Kama asingejenga mngemcheka, mngesema alifuja fedha kwa starehe, amejenga mnaanza maneno. Tafuteni pesa na maisha.
 
dah huu Uzi umenikumbusha huyu nzi (Enigma), huyu alikuwa nzi wa ukweli kipindi chake. Pia mkuu Kichuguu, mmepotelea wapi jamani?
 
Lumumba jibuni hoja Nyarandu kashasema" shida sio kasi mwelekeo upi tunaelekea"
Mwenzenu ameshaona hakuna mwelekeo wowote na uyu sizonje
 
Mkuu huu uzi ni wa 2012 na uliwekwa na mwana chadema mwenzako. Sasa kwa kuwa amepiga picha na ndg zako ndiyo maana unatoa mapovu!! Chagadema ni shidaaaa!!
Suala hapa ni lazaro ni kumtembelea lissu imekuwa shidaaaa kwa wana ccm

Ova
 
Sema tu ni Nyalandu..kwani vipi?! Lazima ayalipe yote haya, labda akimbilie chama kingine! Lakini badotuhuma zipo..
 
Sasa waziri kumilki jumba la 600 milioni imekuwa issue (ndo inatakiwa hivi sasa viongozi wetu waishi pasipo unafiki yaani kama una jumba lako mambo hadharani)...ana trip ngapi za kwenda nje ya nchi, ana safari ngapi za ndani ya nchi na ana marafiki wangapi ambao kwa namna moja ama nyingine wanaweza wakawa partner wake wa biashara...angekuwa ana nyumba kama hizo 10 hao sawa lakini moja naweza nikasema tuache wivu kwani hata huku uraiani watu wa kawaida tu wana nyumba za kuanzia milion 30 mpaka 100 mbona hatuwashangai au kwa kuwa dirisha za nyumba zao ni za nyavu na fence za matete lakini ukiwafuatilia vipato vyao hata kama ni nyumba ya milioni 50 lakini bado hawatabaki salama
 
Baada ya mawaziri wawili wa JK kuhusishwa na umiliki wa majumba/makazi ya mamilioini ya shilingi muda mfupi tu baada ya kushika nafasi zao Waziri mwingine anatajwa kumilimi jumba kubwa ambalo vyanzo vyetu vinakisia thamani yake kuwa ni zaidi ya nusu bilioni. Kutokana na vyanzo hivyo vya kuamika jumba hilo liko kwenye Elkirevi, Kitongoji cha Olorukwa.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya ndani kabisa eneo hilo linadaiwa kuwa lilipatikana baada ya Bw. Nyalandu kununua ardhi yenye eneo la Eka 3 hivi kutoka kwa wanavijiji watano. Jumba lenyewe limejengwa chini ya mwaka mmoja na kukamilikama mwishoni mwa 2011. Jumba limezungushwa na ukuta wa karibu futi 10 na juu yake inadaiwa limewekwa waya wa umeme (electric fence)

Ni kwenye jumba hili ambapo Bw. Nyalandu alifanyia Sherehe ya Mwaka mpya na bila ya shaka ilikuwa ni 'house warming' party. Taarifa hizi zinaendana na zile za mawaziri wengine ambao tayari habari zao za umiliki wa majumba yenye thamani kubwa kuliko vipato vyao na walizopata ndani ya muda mfupi baada ya kuingia madarakani. Mawaziri wengine ni Bw. Maige na Ngeleja ambao wote thamani ya nyumba zao zinakaribia shilingi bilioni 1!


Hata hivyo hadi hivi sasa Tume ya Maadili ya Viongozi haijaonesha kujua mambo haya wala kufuatilia na kuyaweka wazi kama wanazo taarifa na kama kweli vyote hivyo vinaendana na mishahara yao.
Yote haya ni kwa sababu kaenda kumsalimia Tundu Lissu !!! Wa ngapi wana majumba yasiyolingana na vipato vyao, ukiwemo were mwenyewe ? Toa boliti jichoni kwako kwanza...
 
Hizo ni nyuzi zenu chadema....ndiyo maana huwa tunawashaurini muweke akiba ya maneno.
Una uhakika mimi chadema? Unaweza nitajia namba ya kadi yangu? Nawewe uweke akiba ya maneno usihukumu mtu kama humjui itikadi yake wala hujawahi kutana naye kwenye mikutano. Sina chama na sihitaji chama chochote kuishi nchini mwangu.
 
zaidi ya mshahara wa waziri na posho zake ambazo haziwezi zidi m7 kwa mwezi. Kuna kipato gani zaidi cha kumuwezesha mtu kujenga nyumba ya b1 kwa kuzingatia na maisha mengine yanaendelea?
acha ujinga ww, hiyo M7 ndio mshahara.
Posho zinaweza zidi mshahara. Akiandaa safari za mikoani hiyo posho sio ya kitoto.

Acha ubunge alionao, mshahara na posho zake.
 
Mimi sishangai kwa huyu Lazaro kuwa jumba la thamani hiyo,kwasababu ana pesa ndefu kabla hata hajawa mbunge na hatimaye waziri,japo hili halimzuhii kufuja mali za umma.Na kama mchangiaji mmoja alivyododosa tatizo ni utumiaji rasilimali za nchi kufanya mambo binafsi kama hayo.kama mleta uzi ana ushahidi hata wa kimazingira tu,aumwage hapa ili huu uzi usikae kiswaziswazi.
tupe na ww ushahid wa hzo pesa ndefu kabla hajawa waziri tupe vitu alivyokuwa anamiliki kabla na thaman yake. bila shaka cc n watu wa singida
 
Back
Top Bottom