Nape ni moja ya viongozi wa ccm wanaofanya kazi kama upepo kufuata bendera,wizara ya kilimo matatizo yake si ya kuyaongelea majukwaani,ni swala la serikali kuipa wizara pesa ili iweze kusimamia kile ilichokipanga na si kazi ya waziri kwenda hazina na kuomba pesa ambazo zilishwa pitishwa bungeni.Ninani aliyebinafsisha viwanda vya korosho? tulikuwa na viwanda vingi vya korosho vilivyokuwa vikiongeza dhamani ya zao hilo,kilichotokea ni kwamba,wamepeana viwanda na kuviuwa,ili tu waweze kuinunua korosho ambayo haijaongezwa ubora na kwenda kuiuza kwa bei kubwa,hapa wao wanaangalia faida yao binafsi na si wakulima.Nape alitakiwa kuitaka serikali na si waziri,kuwekeza pesa ktk ujenzi wa viwanda vya kuongeza dhamani ya korosho,na kuwataka wale wote wanaowakopa wakulima korosho kuwalipa pesa zao kwa wakati.kwani kun a watu hawajakopa pesa bank,lakini wamewalipa wakulima wa korosho pesa yao yote na wale waliokopa pesa bank,mpaka sasa hawajawalipa wakulima salio lililobaki.Nape-wizara ya kilimo inahitaji pesa ili mambo yaende,na si propaganda za siasa.